Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Fedha na Mipango

Hon. Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Fedha na Mipango

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, nianze kwa kumpongeza Waziri wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Mwigulu Lameck Nchemba kwa kazi kubwa anayofanya hasa katika kuhakikisha kuwa uchumi wa nchi yetu unaendelea kuwa imara. Nampongeza pia Mheshimiwa Hamad Hassan Chande - Naibu Waziri, Ndugu Emmanuel Tutuba – Katibu Mkuu Fedha na Mipango, pamoja na Naibu Katibu Mkuu pamoja na timu yote ya Wizara. Kwa namna ya pekee nimpongeze mwenye fedha mkuu Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan - Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, nina maombi yafuatayo; naomba mtupitishie maombi yetu ya fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa ofisi ya Halmashauri ya Nyasa, taarifa za ngazi zote zipo tayari na imebakia ruksa yenu. Hata hivyo natoa shukrani nyingi kwa hatua iliyofikiwa.

Mheshimiwa Spika, ili kuboresha huduma za kikodi tunashauri Wilaya ya Nyasa nayo ijitegemee ki-TRA badala ya kuwa mtoto wa Mbinga.

Mheshimiwa Spika, nawasilisha.