Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Albert Ntabaliba Obama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. ALBERT O. NTABALIBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuwapongeza Mawaziri wote wa Wizara hii kwa kazi nzuri wanayoifanya.
Napenda kusisitiza kwamba kwa kazi nzuri mnayoifanya ingawa bajeti yako ni ndogo sana kulingana na mahitaji ya nchi hii, ninayo machache ya kuchangia:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, reli ya kati ni ukombozi wa wananchi wengi ndani ya nchi hii. Tunaomba Serikali ilifanyie kazi kwani sasa ni hitaji kwa wananchi na kusafirisha mizigo mikubwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Mnamila – Kasulu – Kibondo – Nyakanazi, tunaomba ipewe umuhimu wa kipekee kwani ni kero kubwa sana. Kigoma nayo ipewe kipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, Mheshimiwa Rais aliahidi kutupatia fedha za kupasua barabara mpya za Nyakimue hadi Muhinda, Rusaba hadi Nyamboze, Kibande hadi Nyamugali, Kilelema hadi Mugera, Munzeze hadi Kwitanga, Kajana hadi Kasumo, Mwayaya hadi Buhigwe. Tunaomba fedha za kupunguza urefu kwenda makao makuu ya Wilaya, kwani ni kero kubwa sana, bajeti ya Wilaya hairuhusu kupasua barabara mpya. Tunaomba mtusaidie na ahadi ya Rais iweze kutekelezwa. Tunaomba special fund na wataalam waje wapitie barabara hizi na cost analysis iweze kufanyika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho tunawatakia mafanikio mema.