Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ya kuongea. Nianze kwanza kwa kusema kwamba bajeti tuliyopewa ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, ni bajeti nzuri, na mimi kwa Jimbo la Musoma Vijijini miradi yote tuliyoiomba imekubaliwa. Kwa hiyo, hii bajeti naiunga mkono kwa niaba ya wananchi wa Musoma Vijijiji. Kwa hiyo kinachofuata ni namna ya kuboresha au kudumisha uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nitachukua picha kubwa zaidi kwa sababu Jimbo limeshapata kila kitu, sasa nifanye kitu cha kutafuta fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo. Mheshimiwa Waziri amefanya presentation nzuri sana na akatuonesha hali ya uchumi ilivyo duniani. Nitaongezea tu kwamba, kwa hali tuliyonayo ya uchumi sasa hivi, wataalam wabobezi wa uchumi duniani wanasema ni hali kama ilivyokuwa mwaka 1973 na 1974 ambapo mafuta yalipanda bei mara nne. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 1979 na 1980 mafuta yalipanda bei mara mbili, na watu wa umri wangu wanakumbuka hii ya pili ya mwaka 1980 ndiyo mapinduzi yaliyomtoa Shah, kwa hiyo, Iran haikutoa mafuta vilivyo. Kwa hiyo, mwaka 1973/1974 tulikuwa na hali ngumu, mwaka 1979/1980 tulikuwa na hali ngumu, lakini Mheshimiwa Rais wa wakati huo, Baba wa Taifa aliweza kutuvusha. Nami nina imani kwa hali tuliyonayo sasa hivi, Rais wetu Mheshimiwa atatuvusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nampa pongezi nyingi sana kwa bidii anayoifanya. Uchumi wa sasa hivi wana neno la Kiingereza linaitwa Stagflation. Stagflation ni uchumi ambao uwekezaji unapungua, investments hazipo. Ndiyo hali tuliyonayo sasa hivi duniani na Watanzania tuko hapo hapo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ndugu zangu tutatokaje hapo kwenda mbele? Mimi nachukua mambo tuliyokuwa tumekubalina kwenye Dira yetu ya Maendeleo na Mipango ya Miaka Mitano. GDP per capital yetu kwa sasa ni Dola 1,260, tunataka tufike GDP per capital Dola 3,000 mwaka 2025. Mwaka 2025 tutakuwa Watanzania karibu asilimia 70.1. Kwa hiyo, tunachokifanya ni kwamba GDP yetu sasa hivi ambayo ni ya Dola za Marekani 62 billion, tukichukua GDP per capital ya Dola 3,000 kwa kila mmoja, kwa hiyo, mwaka 2025 tunapaswa kuwa na GDP ya Dola bilioni 210. Angalieni kazi hiyo, kutoka Dola bilioni 62 kwenda Dola bilioni 210.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo hapa nakuja kutoa ushauri. Umasikini kwa mwaka 2020, poverty rate ilikuwa asilimia 27.1 na mwaka jana 2021 imepungua ikafika asilimia 27. Kwa hiyo, speed ya kupunguza umasikini bado iko chini na inaendana na uchumi. (Makofi)

Mheshimia Mwenyekiti, matumizi ya umeme nadhani niliwahi kuwaeleza kwamba kipimo kizuri kinachotumika Kimataifa siyo kwamba umeme umefika kijijini, umeme umefika kwenye Kata, umeme umefika sijui wapi? Swali watu wanalotaka kujibiwa, ni watu wangapi kwenye eneo hilo wanatumia umeme; na ni umeme kiasi gani? Sasa records ambazo ziko huko duniani zinaonesha hivi, sisi electricity energy consumption per capital Tanzania ni Kilowatt 95. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jirani yetu Kenya ni Kilowatt 170. Sasa Kilowatt 95 yaani ni umeme ambao unaweza ukautumia ndani ya saa moja, ndiyo kipimo cha Kilowatt hour. Kwa hiyo, sisi ni Kilowatt 95, Kenya ni Kilowatt 170. Ndiyo maana wakati ule nilijadili mambo ya energy mix na leo nimesikia Wabunge wengine wamesema wanataka umeme wa upepo na umeme wa jua.

Mheshimiwa Mwenyekiti na ndugu zangu, tukitaka kufanikiwa kwenye mambo ya umeme, lazima twende kwenye umeme wa jua na umeme wa upepo. Kwa mfano, kwa umeme wa jua, China wana Gigawatt 252. Yaani Megawatts 2,250; kwenye upepo wana Megawatt 281,000. Kwa hiyo, kuendana na uchumi wetu ili tuongeze power per capital, lazima tuzalishe umeme mwingi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kazi tuliyonayo na Mheshimiwa Waziri aliieleza vizuri, uchumi ulishuka ukaja 4.9 percent, mwakani unataka kwenda 5.3 percent, lakini kupunguza umasikini lazima uchumi uende kati ya percent nane na kumi. Tutafikaje huko?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pendekezo la kwanza, kwa ajili ya muda sitaingia ndani, na ndiyo maana nataka mje mwangalie percent ninazoziweka mimi. Growth; kilimo, uvuvi na ufugaji, tuwekeze pale na itatoa ajira mpya na tuseme growth yake iwe kati ya percent moja na mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, namba mbili, tuwekeze kwenye utalii ambayo tunaheshimu mama amefanya film ambayo ina-promote utalii, iwe percent moja. Tatu, ni madini. Twende kwenye gold na msisahau gold reserve, nilishaiongelea gold reserve; tuweke kwenye gemstones, tuweke kwenye critical technical metals, technology metals; hili nalo nilishawaeleza na tutumie gesi yetu ya Helium. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, madini yachangie growth ya 3.4 percent halafu tuuze umeme. Cha muhimu sasa ambacho nataka nikiongee, leo nilitoa ahadi, ni uchumi wa gesi. Uchumi wa gesi unaweza ukachangia growth ya five to six percent. Nini maana ya uchumi wa gesi? Gesi ina uchumi mzuri kwa sababu mbili; kwa sababu gesi unaweza kuitumia kama malighafi, halafu gesi unaweza ukaitumia kama source of heat. Ni vitu viwili vinafanya gesi inakuwa muhimu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa uchumi wa gesi; kwa hiyo, gesi asilia tutatengeneza mbolea, tutazalisha umeme, kutakuwa na plastics na fabrics, hii SNG waliyokuwa wanaongea ya kwenye magari; tutakuwa na kemikali kama LPG, gesi mnayotumia kupikia, ammonia ambayo iko kwenye mbolea na kwenye ma-refrigeration; methanol ambayo inatumika kwenye plastics, ascetic acid ambayo inatumika kwenye kutunzia vyakula. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali linakuja: Je, hiyo gesi tunayo ya kutosha? Kuzalisha umeme unahitaji thousand cubic feet kuzalisha one Kilowatt Hour. Unahitaji seven thousand cubic feet kuzalisha one megawatt hour. Je, hiyo gesi tunayo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, mbolea. Unahitaji 0.57 tons of ammonia ku-produce one ton of urea. Tatu, unahitaji 33 metric million British thermal unit ya natural gas ku-produce one ton of ammonia. Nne, tunaenda vizuri Serikali, mkataba wa awali umewekwa, bei ya LNG tungekuwanayo sasa hivi, Januari mwaka jana 2021 ilikuwa US Dollar sita kwa 1MMBTU (Metric Million British Thermal Unit).

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Waheshimiwa kuna simu inalia mpaka huku tunasikia jamani. Naomba mpunguze au mzime.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nitunzie muda wangu nami nimesimama.

MWENYEKITI: Mheshimiwa kengele ilikuwa imeshalia na huku simu zinalia.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, sawa, naomba basi nimalizie hizo dakika mbili. Kwa hiyo, sasa hii gesi ndiyo maana napendekeza TPDC ibaki kwenye kazi hii, kwa sababu sasa hivi tumeshagundua 57.54 TCF. Jirani yetu Mozambique ambaye yuko kwenye Ruvuma Basin ameshagundua a hundred TCF na huenda ana two hundred. Kwa hiyo, TPDC isipoweka mkazo huko Ruvuma, tutajua tuna gesi kiasi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hiyo ni conventional, kuna aina nyingine ya gesi inaitwa shell gas. Hii shell gas ni nyingi sana, ndiyo Marekani inatumia sasa hivi, wala hatujawahi kuanza exploration. Lake Tanganyika inabidi TPDC ieleze kuna mafuta au gesi? Halafu lazima tujadiliane na Kongo na Zambia. Lake Nyasa kuna mafuta na gesi, lazima tujadiliane na Malawi. Halafu kwenye Lake Eyasi na huku baharini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, ndiyo maana mapendekezo yangu nasema kwamba TPDC wana kazi kubwa, kubwa, kubwa, tuwaache watutafutie hii gesi kwa ajili ya uchumi wetu. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa Prof. Sospeter Muhongo. (Makofi)

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya, ahsante. Mengine nitaongea siku nyingine tena. Ahsanteni. (Makofi)