Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi. Kwanza kabisa nampongeza Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan kwa bajeti yake ya kwanza ambayo ni nzuri sana. Nampongeza pia Waziri wa Fedha, Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Nchemba, mwananchi; Mheshimiwa Naibu Waziri, Bwana Shemeji; na timu yote ya Wizara hii ikiongozwa na Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu na Wataalam wote kwa kazi nzuri ambayo mmefanya. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, bajeti hii tunaipongeza kwa sababu ifuatayo: Moja, kuhusu kilimo. Kilimo fedha imeongezeka sana, shilingi bilioni 954. Ni ongezeko la Shilingi bilioni 660 ukilinganisha na bajeti ya mwaka 2021. Pia bajeti hii imezungumza kuajiri vijana 3,000,000 wa kilimo na itatenga karibu hekta 8,500,000 kwa ajili ya umwagiliaji. Vile vile wanazungumza habari ya kuanzisha viwanda vya saa 24. Twenty-four hours a day na seven days in a week, hii itaongeza kasi ya ajira. Kwa hiyo, kwa kweli ni nzuri sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile kuhusu mifugo, mmezungumka habari ya kuongeza bajeti ya mifuko kwa shilingi bilioni 40 zaidi. Pia kuhusu TASAF, kuanzisha dirisha maalum kwa ajili ya vijana wanaotokana na familia ambazo zimejiandikisha kwenye TASAF, itaongeza sana sana sana ari ya wananchi. Kwa kweli vijana hawa wamekuwa wanateseka sana, hawawezi ku-compete. Usipowawekea dirisha maalum la kwao kwa kweli hasingeweza ku-compete kupata mikopo ile. Kwa hiyo, big up. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye sekta ya mifugo mmezungumza habari ya kuanzisha incubation centers na kuajiri vijana 1,000 wawe na miradi ya kunenepesha, very nice. Ila nina angalizo vilevile baada ya pongezi zote hizo. Kuhusu tani za vyakula vya mifugo; Ilani ya Chama cha Mapinduzi Mheshimiwa Waziri wa fedha I hope unanisikiliza. Tulisema hivi ukurasa wa 52, tani za vyakula vya mifugo ni 8,000,000 kwa miaka mitano, lakini kwa trend sasa tumetoka 900,000 tukaenda milioni moja, na tani laki mbili, na sasa tunazungumza habari ya milioni mojam tani laki tatu na themanini. Kwa hiyo, tukiendelea kwenda na trend ya laki mbili, laki tatu hatutaweza kufikia tani milioni nane. Kwa hiyo, in average actually ilitakiwa kwa miaka mitano kuwe na average kila mwaka tuongeze tani 1,420,000. Kwa hiyo we are not doing so well. Kwa hiyo, tujaribu kuongeza bidii ili tufanye vizuri zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, vile vile nimefurahi sana kuona VETA kuna fedha zimetafutwa kwa ajili ya VETA na Mheshimiwa Waziri mimi niliuliza swali la kwanza Bungeni hapa, namba 13 kuhusu Kiteto kutokuwa na VETA. Majibu niliyopata kutoka Wizara husika wanasema wanatambua Kiteto haina VETA, lakini itakuwa kwenye priority list. Wakileta zile lists zao la VETA 36, Kiteto isipokuwepo usi-approve huo mradi, kwa sababu majibu tuliyowapa wananchi ni kwamba lazima Kiteto iwepo, lakini kwa sababu mmesema mtajenga kwenye Wilaya zote ambazo hazina, Kiteto I am sure itakuwepo tena inatakiwa iwe namba moja. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo, naomba sasa nizungumzie kitu kinachoitwa carbon credits ambayo ndiyo msingi wa hotuba yangu leo. Carbon credit ni new source ya finance ambayo itaiongoezea nchi mapato zaidi. Kwa Afrika nzima, Tanzania ni nchi ya tatu kwa kuwa na eneo kubwa lenye mapori, baada ya DRC na Angola. Kwa hiyo, potential ya carbon credit kwa Tanzania ni kubwa zaidi, na kuna study zimefanyika na natural conservancy zinaonesha kwamba tangu Tanzania mmeanzisha mradi wa Red Plus Project na Tanzania imekuwa pioneers, tumeanza kufanya vizuri na tumeanza kuvuna fedha zinazotokana na carbon credit. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukimwuliza Mheshimiwa Kakoso kule kwao, Mbunge wa Mbulu kule kwao na Kiteto vile vile, sisi tumeanza miradi ya carbon credit na kwa kweli inasaidia sana wananchi. Nilitoa mfano siku moja hapa kwamba Kiteto, internal revenue ni 2.2 billion, lakini sisi baada tu ya kuanzisha mradi wa carbon, vijiji vitano tu vinatengeneza one billion a year. Kwa hiyo, sasa tunge-utilize vile vijiji vyote, maana yake carbon credit ni new financing area ambayo ni lazima Wizara ya Fedha, Wizara ya Makamu wa Rais, Mazingira, na Wizara ya Viwanda na TRA lazima sasa mje strongly mtengeneze policy.

Mheshimiwa Naibu Spika, alipokwenda Rais wetu kwenye baadhi ya safari za Kimataifa alisema hivi, baadhi ya wawekezaji, yaani wawekezaji wanaokuja kwa wingi sana ni watu wanaokuja na miradi ya carbon credit. Kwa hiyo, mtegemee kupata watu wengi sana wa carbon credit. But it is a shame, we don’t have a law and we don’t have a policy. Hakuna mtu atakuja hapa bila kuwa na framework na legislation for certainty purposes. Kwa hiyo, ni lazima sasa muanze ku-speed.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye Bunge hili, Mheshimiwa Mbunge wa Vunjo Dkt. Kimei aliuliza swali hapa la cardon credit, Mheshimiwa Mbunge wa Kilolo aliuliza vile vile, lakini majibu tunayoyapata hapa, tunaambiwa bado Serikali inatengeneza policy. Honestly! Six years, ten years down the line? Mheshimiwa Rais anawaleta watu sasa waje kwa ajili ya wawekezaji...

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, taarifa.

NAIBU SPIKA: Taarifa.

T A A R I F A

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, sina nia ya kumvurugia mtitiriko Wakili Msomi, lakini naomba kumpatia taarifa kwamba kupitia mifuko mbalimbali ya mabadiliko ya tabianchi kama Adaptation Fund, Climate Fund na kadhalika, tungeweza kunufaika sana, lakini nchi yetu ina taasisi mbili tu ambazo zimekuwa accredited ambayo ni NEMC na CRDB na hizi fedha nyingi na grants, wala siyo mikopo. Kwa hiyo, naomba kumpa hiyo taarifa. Nchi kama Kenya ina taasisi 18, sisi tunazo mbili tu wakati hii ni fursa kubwa sana. (Makofi)

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Kisau.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na nakubaliana na mchango mzuri sana huo, sana! Kwamba hii biashara ya carbon credit siyo tu kwamba ni biashara as business per-se, lakini pia inaongezea nchi fursa za kupata climate change financing. Kwa hiyo, ni lazima tujikite zaidi kutokana na biashara hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, in fact, tunaambiwa tuna mapori between 48 to 50 million hectors nchi hii zipo protected. How much we get it for this forest? Ni rasilimali iliyopo, in fact watu wengine wanasema ni business for doing nothing. Yaani mapori yapo tu, which is good for climate na itakuletea mvua, acha kukatakata mapori, halafu utapata cardon financing. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nchi zinazoongoza sasa duniani on cardon financing na wanao-produce carbon, ya kwanza ni India; ya pili, Marekani; ya tatu, ni China; ya nne, Indonesia, Peru, Kenya, Brazil, Guatemala, Uganda and Zimbambwe. Zinazoongoza kununua, market ni United States, France, United Kingdom, German and Switzerland. Kwa hiyo, najua hii carbon financing ni new area hata Wabunge wengi hawafahamu. Naomba hata Bunge litafute mjadala wa siku moja ili Wabunge wafundishe Habari ya carbon financing. It is a new sources of funding ili tuje tupate mjadala, wataalam waitwe, waje watufundishe ili nchi sasa ianze kukimbia mbele zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Afrika kwa mfano, projects ambazo zimekuwa registered on carbon financing ni miradi karibu 234. Asia and Pacific 6,580; Europe and Central Asia 89; Latin America 1,139; Middle East ni 87 ambazo ni worth 190 billion USD, ni fedha nyingi sana. Tusiache Mheshimiwa Waziri hii ni gold ambayo imekaa ili tuweze kui-utilize.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema haya, nakushukuru sana, ahsante sana. (Makofi)