Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2021 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunivumilia. Nimeomba sana nichangie mapema, na umenivumilia ukanipa fursa hii. Nakushukuru sana.

NAIBU SPIKA: Sasa vipi, umekasirika uondoke au?

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, niko vizuri.

NAIBU SPIKA: Aah, okay. Ahsante.

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, naanza kwa kumpongeza Mheshimiwa Rais wetu kwa kutuletea bajeti ambayo ni nzuri sana kusema kweli. Pia nampongeza Mheshimiwa Waziri wetu mchumi msomi Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Mchemba, Naibu wake, Katibu Mkuu, Manaibu Katibu Wakuu na timu nzima ya Wizara kwa kazi nzuri. Niseme kwamba wamefikiria sana nje ya box wakati huu, ndiyo sababu unaona kwamba sera wanazotuletea ya matumizi na mapato ni sera ambayo ina vitu vipya, vitu ambavyo hatukuviona huko nyuma. Nasema kwamba, kweli ninyi mmechapa kazi vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka niseme kwamba, nitaendelea kuwapongeza endapo watakumbuka kwamba tuna wananchi kule Kahe Mashariki ambao wanadai shilingi bilioni 5.2 kwa thamani ya mwaka 2013 ambao wametoa maeneo ya kujenga One Stop Inspection Center pale Njiapanda Himo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye bajeti yenyewe. Niseme kwamba, hii bajeti ni bajeti ambayo kweli imetengenezwa kwenye mazingira ambayo mimi nasema ni magumu kwa sababu kuna vihatarishi vingi ambavyo havitabiriki kutokana na uchumi wa dunia na uchumi hata huu uchumi wetu. Kwa hiyo, naamini kwamba tutapitisha hii bajeti, lakini mimi naamini ni vizuri utekelezaji wake ukawa unafanywa continuous risk assessment ili kujua kwamba, je, ni kweli kwamba, zile assumptions zitakuwa fulfilled?

Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba bajeti imebana, inaonesha kuwa na fiscal measures ambazo ni nzuri na ndiyo sababu unaona kwamba financing ukiondoa ile rollover, financing inayokuwa required na angalau 3% ya GDP ambapo kusema kweli kwa hivyo naona kwamba tumeji-tighten.

Mheshimiwa Naibu Spika, niseme kwamba, kwa viashiria hivi tunavyoona kule Ulaya sasa hivi, UK wanatangaza inflation ya 11%, Marekani inflation iko juu 7% na viashiria hivi vya interest rate kupanda kuendana na inflation; na kule Marekani sasa hivi riba kwenye hizo third reserve rate ni 3.5%. Kwa hiyo, inaonekana kwenye masoko ya kukopa, masoko ya International Re-capital Market riba zitapanda sana. Zitapanda sana kwa maana kwamba sio wakati wa kukopa nje kwenye masharti ya biashara kwa sababu ni lazima tujiangalie.

Mheshimiwa Naibu Spika, ndiyo sababu nikasema kwamba, cha kwanza ni kuona kwamba kweli kuna mambo ambayo tumeweka. Kwa mfano, ukopaji wa about three trillion kutoka kwenye masoko ya nje, inawezekana baadaye tukaona kwamba pengine tusitishe au tupunguze miradi ile ya maendeleo, hususan ununuzi wa ndege nyingi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, nafikiri ndege tunazozitaka sasa hivi ni lazima tumwombe Mheshimiwa Rais atuletee ndege ya mizigo kwa sababu inahitajika, ndio big constraint ya ku-export bidhaa za bustani (hot culture products). Ni hazina, ni kwamba hatupati kutoka nje flights za kutosha kwa sababu pia uzalishaji wetu hautoshelezi kwa ndege za nje ziweze kuja na zitue mahali pamoja, lakini tukiwa na ya kwetu itatua Mbeya, ije Dar es Salaam, iende Arusha, itajaa itapeleka nje. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika ubunifu nilioona hapa ni kwamba Serikali na timu ya finance wamegundua kwamba, sasa hivi nadharia ya kuongeza tu kodi siyo njia pekee ya kuongeza mapato ya Taifa. Pia unaweza ukahamasisha matumizi kwa mfano, kama ni wanywa bia wanywe kwa wingi zaidi, kama ni watumia simu, watumie kwa wingi. Kwa hiyo, this time tunaona wamejaribu kuangalia ni namna gani waongeze volume. I think tutapata mapato makubwa zaidi kwa kupunguza au kwa kutokuongeza kodi za vinywaji; bia na vinywaji vingine pamoja na vinywaji vya baridi, hawakuongeza. Nawapongeza kwa sababu watu watatumia na volumes zitaongezeka, kwa hiyo, naamini mapato yatakayotokana na ile volume itakuwa ni vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, naona ile ya tozo tuliyozungumza mwaka 2021, wamepunguza, lakini pamoja na kupunguza kidogo baada ya mkutano wa mwaka 2021, na mwaka huu 2022 wamepunguza ile tozo ya miamala. Ninaamini kwamba, hiyo imetokana na ukweli kwamba, matarajio ya makusanyo kutoka kwenye tozo hayakufikiwa by more than 70% I think kutokana na takwimu. Kwa hiyo, hiyo kupunguza huko kutasababisha watu waendelee kutumia hiyo financial improvement iendelee kupatikana kupitia hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia hatua nyingi zilizochukuliwa kwenye bajeti hii zinalenga zaidi kuwapunguzia wananchi makali ya mfumuko wa bei ambao tunaona unatoka nje. Nataka niseme hivi, nitoe angalizo kwamba tusipeleke matarajio ambayo hatutaweza kuyafikia. Matarajio kwamba tunaweza tukadhibiti mfumuko wa bei kwa sasa hivi, naomba tujaribu kuwaelimisha watu kwamba kwa nini huu mfumuko ni mgumu?

Mheshimiwa Naibu Spika, huu mfumuko siyo ule wa kawaida ambao Benki Kuu wanaweza wakaenda tu wakasema tunapunguza ujazo wa fedha kwenye mzunguko wa uchumi wetu. Hawawezi, kwa sababu wakifanya vile siyo source yake. Source ya huu mfumuko ni ugavi; ni upungufu au uhaba wa bidhaa duniani, na uhaba wa bidhaa unachukua muda. Kwanza kuongeza uzalishaji kunachukua muda, kwa hiyo, hata ufanyaje ni kitu kinachukua muda.

Mheshimiwa Naibu Spika, pili, ili kuongeza uzalishaji ni lazima tuweze kutoa mikopo. Hiyo mikopo ni ya kuwasaidia wale watu waweze kuanzisha miradi ile na kama kilimo wafanye. Ila ukweli ni kwamba, ukiongeza hiyo mikopo maana yake unaongeza fedha kwenye mzunguko, na unachochea demand. Kwa hiyo, hiyo inasababisha mfumuko wa bei uwe mgumu sana kuudhibiti kwa sababu, ukiingiza hela ili watu wazalishe, lazima itasababisha mfumuko. Ila ukweli hatuwezi kuepuka hilo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ina maana kwamba, tukubali, hata kama mfumuko utaongezeka kidogo, lakini itakuwa ni temporary transitory, baada ya muda kidogo uzalishaji utakuja, tutapata mawese, na kadhalika halafu tutaanza sasa kushusha tena ule mfumuko. Kwa sasa hivi tusing’ang’anie sana hiyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine, kuna suala zima la stabilization fund ya bei za commodities. Nafikiri badala ya kufanya vile, mimi niende haraka niseme kwamba, nashauri Wizara iangalie mfumo wa commodity pricing insurance. Sisi tulifanya kwa kushirikiana na IFC pamoja na Rabobank pale wateja wetu wakafaidi sana. Tutumie huo mfumo badala ya kuanza funds na kadhalika. Hilo linawezekana sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine kuna issue hii ya kutengeneza Dar es Salaam kama hub, na jana au juzi uliizungumza, naamini kitu cha msingi, hizi measure zilizochukuliwa sasa hivi ni za kupunguza ushuru ili watu waweze ku-trade kutoka Dar es Salaam zaidi badala ya kwenda jirani halafu mizigo inarudi kwetu, naamini kwamba hiyo itasaidia. Ila kwenye issue ya changamoto…

(Hapa, kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, aah, time keeper naona, huyu time keeper huyu!

NAIBU SPIKA: Ahsante kwa mchango mzuri. (Makofi)

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, tum-audit huyu time keeper. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja na ahsanteni sana. (Makofi)