Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba niongeze kidogo kwenye mchango wangu niliowasilisha jana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuombe Waziri wa Ujenzi aipe barabara ya Ruaha Mbuyuni - Mlolo (Chabi) - Ibanda - Mlunga - Ileling‟ombe mpaka Mpwapwa ya kilometa 74 ambapo inaunganisha Wilaya mbili za Kilosa na Mpwapwa. Hii inamaanisha kuwa inaunganisha mikoa ya Iringa, Morogoro na Dodoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Mfuko wa Barabara wa Mkoa wa Morogoro walifanya tathmini na kuipitisha barabara hii kuwa chini ya TANROADS na pia waliwaalika wataalam kutoka Wizara ya Ujenzi ambao nao waliipitisha na kusema inafaa kufanyiwa kazi haraka sana kadri inavyowezekana. Namuomba sana Mheshimiwa Waziri akija ku-wind up aje atupe majibu, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii ili kuunganisha wananchi hawa wa mikoa ya Dodoma na Morogoro na Iringa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.