Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, ninamshukuru Mungu kwa kuwezesha kujadili mada za kuiletea nchi yetu ya Tanzania maendeleo.
Pili, ninampongeza sana Mheshimiwa Waziri Profesa Makame Mbarawa, Naibu Waziri, Injinia Edwin Ngonyani na Injinia Joseph Nyamhanga, Katibu Mkuu Ujenzi, Dkt. Leonard Chamuriho, Katibu Mkuu Uchukuzi, Profesa Faustine Kamuzora, Katibu Mkuu Mawasiliano, Injinia Dkt. Maria Sasabo, Naibu Katibu Mkuu Mawasiliano na watendaji wote wa Wizara husika na bodi zao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja yangu ni kuhusu mawasilianio ya simu. Utakubaliana na mimi kwamba simu za mkononi zimeshamiri kila kona ya nchi hii, lakini kila leo gharama za simu zinapanda.
Swali, hivi Mtanzania wa kawaida anafaidikaje na wawekezaji hao wa mitandao mbalimbali wakiwemo Airtel, Vodacom, Tigo, Zantel, Halotel na wengine?
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana atoe mwongozo kwa makampuni hayo yatoe elimu ya ujasiriamali kwa wanawake kama mgao wa CSR. Niko tayari kuungana nao kule Kilimanjaro ili elimu hiyo iwafikie wengi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga hoja mkono.