Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, miundombinu imara ni msingi muhimu wa maendeleo ya sekta nyingine zote. Naamini unapokuwepo mgawanyo sawa wa rasilimali za nchi, unapunguza ombwe la watu wengine kuilaumu Serikali. Napongeza ujenzi wa barabara ya Tabora - Koga - Mpanda kwa kiwango cha lami ambao utaanza hivi punde. Rai yangu ni mchakato huu wa ujenzi usichukue muda mrefu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ujenzi wa uwanja wa ndege Mpanda uendelee kuimarishwa kwani huduma ya ndege ni muhimu sana. Niiombe Wizara kutupatia huduma ya mafuta ya ndege, sambamba na route za ndege.
Mheshimiwa Mwenyekiti, reli ya kati na matawi yake, ikiwemo Kaliua - Mpanda - Karema ni la msingi. Barabara ya Mpanda - Ugala - Kaliua ni muhimu mno, ukizingatia uwepo wa barabara moja bila kuwa na escaping route ni jambo la hatari, hasa pale barabara zinapojifunga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha na kuunga mkono hoja.