Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, awali ya yote nitumie nafasi hii kukushukuru kwa kunipa fursa, lakini tumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutujalia kuwa na a health discussion inayoendelea ndani ya Bunge lako tukufu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba, mimi ni Mbunge wa awamu ya pili, katika Ripoti za CAG ambazo nimewahi kuona zikijadiliwa openly, transparently na healthy, hii ni moja wapo ya ripoti ambayo nimeiona katika kipindi changu cha pili cha Ubunge. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, nataka tu nimhakikishie Mheshimiwa Bonny Kwamba, Mawaziri hatuko katika sehemu ya kulinda ubadhirifu wala hatuungi mkono uhalifu wowote unaofanyika. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la jumla, CAG ni jicho na ni jicho la Bunge lako kwa maana ya oversight function. Vile vile, ni jicho kwa sisi tuliopewa responsibility ya kuweza kusimamia na kuhakikisha tunachukua hatua za kulinda rasilimali za nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pale CAG anapokabidhi ripoti kwa Rais na inapokuja Bungeni na tunapotakiwa kwenda mbele ya Kamati, Serikali tunachukua hatua. Kwa mfano, CAG katika ripoti hii ya mwaka 2021/2022, amezungumzia suala la Mfuko wa Pembejeo kwamba, kuna non-performing loans za zaidi ya shilingi bilioni 121 ambazo hazijakusanywa.

Mheshimiwa Spika, vile vile, CAG ametoa recommendation na Kamati yako ya PIC imetoa recommendation. Moja ya recommendation iliyotoa ni kwamba baadhi ya madeni tuyafute. Hata hivyo, sisi kama Serikali tunachukua hatua gani ili kuweza kusimamia rasilimali za umma?

(i) Kama Serikali tumefanya mabadiliko ya taasisi yetu ya Mfuko wa Pembejeo. Tumewaondoa viongozi waliokuwa wanasimamia taasisi zile na tumechukua professionals ambao wengine ni credible. Sasa hivi DG wa Mfuko wa Pembejeo ni Formal Chief Executive Officer wa ECO BANK. Tumemwomba Rais, tumemtoa private sector na tumemleta tumkabidhi ule Mfuko ili aweze kuu-transform. Mfuko ule ni muhimu kwa uchumi wetu na sekta yetu. (Makofi)

(ii) Mfuko wa pembejeo, wote, viongozi na wasiokuwa viongozi wali-take advantage na CAG amesema na ametoa maelekezo. Sisi katika hatua ya kufuta madeni, hatuendi kufuta madeni kwanza, tunataka ku-recover fedha. Toka mwezi Machi alipo-submit report, tumeshakusanya zaidi ya 1.4 billion. Pia, baadhi ya Wabunge, watumishi wa umma pamoja na viongozi wastaafu wanaodaiwa tumeshawaletea notice. Sasa tunakwenda kuwasajili kwenye credit reference bureau ili wakose uhalali wa kukopeshwa kwenye sekta yoyote ile ya nje katika uchumi mpaka waje walipe hela za umma walizokopa katika Mfuko wa Pembejeo. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Waziri, wapo Wabunge wanaodaiwa?

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, yes wapo. Vile vile, wapo hapa kwenye orodha ninayo. Pia ukiniruhusu naweza nikawataja. (Makofi/Kicheko)

SPIKA: Hapana, nimetaka tu hilo Wabunge wafahamu. Maana watu tunaposema CAG amekwenda huko kukagua akakuta madeni makubwa halafu na sisi tunadaiwa humo, tuwe wa mfano, maana sasa tusije tukawa tunawazungumzia wengine huko na sisi wenyewe hatufanyi. (Makofi)

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika…
SPIKA: Mheshimiwa Bashe, muda wako unalindwa. Endelea na mchango wako, nilitaka tu kujua hilo.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, tunakuletea rasmi (formally) ili wakati wa gratuity tuweze ku-recover zile hela. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo la pili ambalo Kamati ya PAC na bahati nzuri Makamu Mwenyekiti wa Kamati ni aliyekuwa Boss wangu, ametupatia ushauri kwenye Kampuni ya TFC…

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Taarifa inatoka wapi? Okay, Mheshimiwa Bashe, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Hamis Taletale.

TAARIFA

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, naomba Kaka yangu Bashe, hiyo list uliyoishika ungeitaja kidogo, tungejua umuhimu wa CAG.

SPIKA: Hebu hiyo orodha niletewe hapa mbele. (Kicheko/Makofi)

Waheshimiwa Wabunge, nataka niletewe hiyo taarifa kwa sababu na ninyi humu ndani mkichangia kuna watu mnawataja. Kwa hiyo, ngoja niletewe hiyo taarifa nione ukubwa wa hilo tatizo. Ahsante sana. Mheshimiwa Waziri endelea na mchango wako.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, Taarifa ninayokukabidhi ni baadhi ya Waheshimiwa Wabunge waliokopa wao binafsi. Vile vile, baadhi ya Wabunge waliowadhamini wananchi wao kama guarantor. Pia vilevile baadhi ya viongozi wastaafu. Kwa hiyo hii hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatizo linalokabili Mfuko wa Pembejeo katika nchi yetu kwenye hili suala la kukopesha, linaikabili vile vile Tanzania Investment Bank na linaikabili Benki yetu ya Kilimo. Tumeomba katika eneo la Benki ya Kilimo nao tukuletee list ili uweze kutusaidia na TIB iweze kutusaidia kupitia ofisi yako. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, eneo la pili ambalo nataka nichangie ni eneo la maoni ya Kamati kuhusu TFC. Nataka niwahakikishie Kamati, tumechukua recommendation za CAG kuhakikisha kwamba, Kampuni yetu ya Mbolea inanunua moja kwa moja kutoka kwenye source na inafanya trading. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kulikuwa na hoja kwamba Serikali isifanye biashara, nataka niwaombe Waheshimiwa Wabunge, duniani kote Serikali inafanya biashara. Tunachotakiwa kujiuliza ni kwamba, taasisi za Serikali zinazofanya biashara, zinafanya biashara efficiently and effectively? Kama hazifanyi ni kwa nini hazifanyi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa mfano TFC, tuliiua wenyewe TFC, tukaua viwanda vya kuchakata mbolea, tukavibinafsisha kwa bei holela, lakini leo tumeona umuhimu na sasa Serikali imeipatia TFC zaidi ya bilioni 110. Leo tunavyoongea, TFC inapakua zaidi ya tani 50,000 katika Bandari ya Dar es Salaam ili kuingiza katika soko la mbolea ndani ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tumefanya mabadiliko kutokana na recommendation za Mkaguzi (CAG) kwamba, tufanye mabadiliko ya menejimenti. Tumefanya mabadiliko ya menejimenti, imeundwa Bodi, tumeweka CEO mpya, tumeweka Commercial Director mpya, tumepeleka Director of Finance mpya mwenye uwezo. Mabadiliko ya Sheria ya Procurement Act ambayo yamekuwa yakiifunga miguu TFC ku-compete sokoni, tumechukua hatua hizo ili TFC iwe competitive na hivi sasa tume… (Makofi)

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Haya, ahsante sana. Mheshimiwa Bashe, kuna taarifa kutoka kwa Mheshimiwa Kandege.

TAARIFA

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Taarifa ambayo nataka nimpe Mheshimiwa Waziri, pamoja na mchango wake mzuri juu ya sisi kuua taasisi za Serikali. Kwa mfano TFC ni kwamba, waliagiza mbolea lakini yakaja maelekezo wauze below price. Kwa hiyo, kwa vyovyote vile hasara ilianza kupatikana tangu siku ya kwanza. Ahsante.

SPIKA: Mheshimiwa Bashe, unaipokea taarifa hiyo?

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naipokea na nakiri kwamba, TFC na mashirika mengi ya nchi yetu yaliuawa because of political intervention na maamuzi ambayo ni ya kisera na policy ambazo hazikuwa home-grown policies, kwamba, government should not trade. Hii ndiyo ilipelekea kuua na kwa kuwa tumejifunza, naamini hatutokwenda tena siku nyingine kuichokonoa TFC katika nchi yetu. Sasa, TFC tumeipatia fedha inajenga blending facility Kwala. Tumeinunulia eneo na inajenga blending facility ili kuwa competitive.

Mheshimiwa Spika, la tatu, ambalo nilitaka nimalizie, mawili tu ya mwisho ili nimalizie…

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Maganga.

TAARIFA

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Spika, mchangiaji, Mheshimiwa Waziri anachangia vizuri sana na namheshimu. Hata hivyo, kwenye taarifa iliyoko hapa mezani, tunajadili ripoti ya CAG. Kuna watu wametajwa majina na wewe umesema kuna majina ya Wabunge pamoja na Mawaziri ambao ni wahusika. Sasa, naomba Waziri afunguke kabisa aache kufumba macho tusije tukaua Chama. Ahsante sana. (Makofi)

SPIKA: Mheshimiwa Waziri, dakika moja malizia mchango wako.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba nimalizie. Pia, kama dakika moja haitatosha nitakuomba unipe hata mbili. Nataka nimalize mambo mawili ya mwisho.

Mheshimiwa Spika, jana kwenye contribution ya Waheshimiwa Wabunge, kuna jambo lilisemwa hapa. kwamba, Ripoti ya Financial Intelligence Unit imeonesha upotevu wa over two hundred trillion shillings. Nimeamua kwenda kuichukua ile ripoti na kuisoma, kuangalia, nilishtuka sana.

Mheshimiwa Spika, mchangiaji alisema, nanukuu: “fedha hizi zinahamishwa kupita mipakani.” Technically ukijiuliza kwa kufumba macho, unaamini kuwa kuna malori yanakatiza pale border na hela.

Mheshimiwa Spika, nimekwenda kuchukua ile taarifa. Sisi ni Wabunge tuna communicate na wananchi nje, ni hivi, Financial Intelligence Unit Report ambayo summary yake hii hapa, imesema hivi: “Taarifa za miamala ya fedha taslimu (cash transactions) ni 7,313, value ya hizo cash transactions siyo value ya hela tu, transactions thamani yake ukijumlisha ni 56 trillion shillings.”

Mheshimiwa Spika, nini maana yake? Any financial analyst anatakiwa afanye analysis. Nini maana yake? Maana yake ni hivi, our economy is dominated with cash transaction. Nimeuza mahindi NFRA nalipwa cash, nabeba nakwenda foleni benki na-deposit. Financial Intelligence Unit wana-capture zile data. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Financial Intelligence Unit wamesema, taarifa za miamala ya fedha kwa njia za kielektroniki 8,784, thamani yake ni trilioni 200. Maana yake, huko mtaani tunapeana cash, tunalipana kwa M-pesa, tunarushiana. Leo kwa taarifa za Benki Kuu, ratio ya formal na informal ni 60:40. Tafsiri yake bado kuna cash nyingi huko mikononi mwa wananchi ambazo haziko katika mfumo rasmi. Kwa hiyo, tunapoziona cash zinatoka kwenye informal kuingia kwenye mfumo wa kibenki ni hatua nzuri kwa uchumi wowote unaokua. (Makofi)

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, Taarifa.

SPIKA: Waheshimiwa Wabunge, kwanza taarifa zimekwishafika tatu. Pili, huu muda anaotumia Mheshimiwa Waziri ni wa kumalizia sentensi ili nimwambie muda umekwenda, kwa sababu sasa hivi ni saa nane Waheshimiwa.

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Spika, anapotosha, anachokizungumza anapotosha siyo purpose ya FIU.

SPIKA: Omba utaratibu, kama anapotosha omba utaratibu.

Mheshimiwa Bashe.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, la mwisho, kwenye hii hoja, ninachotaka niseme kwenye hii hoja ni hivi, tusichukue taarifa kwenye document na kufanya literal translation halafu na kuzipeleka mtaani, zina-confuse public.

Mheshimiwa Spika, la pili, leo hapa na wewe naomba nikunukuu, umehoji kitu ambacho tunatakiwa tukijadili as a country. Our governance system, umehoji hivi, baada ya Mheshimiwa Jerry Silaa kutoa taarifa kuhusu nafasi ya Mbunge katika halmashauri kwamba, Mbunge ni Mjumbe wa Kamati ya Fedha. Wewe ukasema, kama Mbunge ni sehemu ya Kamati ya Fedha katika Halmashauri inayotuhumiwa, huwezi kujadili kesi inayokuhusu.

Mheshimiwa Spika, nini maana yake? Maana yake umefika wakati wa kufanya critical analysis ya role ya Mbunge kwenye halmashauri na namna gani anamsimamia Accounting Officer. Waziri anapokwenda kwenye PAC, ambapo PAC inamwita Katibu Mkuu, Waziri hayupo. Nafika hapa ndani ya Bunge nahojiwa kwa kile ambacho wali-differ kati ya PAC na Waziri kwenye kikao ambacho mimi sijashiriki kama Waziri. (Makofi)
SPIKA: Haya, sawa.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, namalizia…

SPIKA: Mheshimiwa Waziri, hoja yako imeeleweka. Umekwishatoa pendekezo kwamba umefika muda wa kufanya hilo jambo, hatuwezi kuchukua muda zaidi ya hapo. Ahsante sana.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)