Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Dr. Abdallah Saleh Possi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU (WATU WENYE ULEMAVU): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kusema machache kuhusu bajeti ya Wizara inayohusika na Mawasiliano na Uchukuzi. Kuna mambo mawili hatuwezi tukakwepa na wala hatuwezi tukaingiza siasa inapokuja katika masuala ya mawasiliano ambayo ni sheria na teknolojia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninavyozungumzia sheria nina maanisha Sheria za Kimataifa na Kitaifa na nianze kwa kusema kwamba Tanzania mwaka 1983 ilikuwa mwanachama wa WIPO (World Intellectual Property Organization) na kwa maana hiyo, ndio maana tuna sheria ambazo zinalinda haki za watu waliotoa ubunifu wa aina mbalimbali katika teknolojia, kwa lugha rahisi ni patents.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kwa sababu tunakubali kwamba Tanzania haiwezi ikajifungia na tupo katika kisiwa kinachoitwa globalization, kwa hiyo, ni wajibu wa Tanzania kulinda patents za wabunifu mbalimbali wa Hitanzania na wa Kimataifa. Na ndio maana suala la kukataza matumizi ya simu fake sio utashi tu wa TCRA au sio siasa tu, ni wajibu wa kisheria za kwetu za ndani, lakini pia na za kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu sisi sote, Wabunge tuna nia moja ya kuhakikisha kwamba tuna act kama viongozi kuhakikisha kwamba Taifa linakwenda katika mstari ulionyooka, basi ni rai yangu kwa Wabunge wote kuunga mkono suala hili. Na katika kusema hivyo niweke wazi kwamba maendeleo ya teknolojia sasa yamewafanya pia baadhi ya wajanja kuwa haraka zaidi kutumia teknolojia hiyo hiyo kuingiza simu fake, ndio maana kwa wale wanaofuatilia wanakumbuka mwaka 2014 Ujerumani zilikamatwa Samsung Galaxy, Uingereza pia hivyo hivyo, tena kule ulikamatwa mpaka mnara fake uliokuwa unaingilia mawasiliano ya watu. Mwaka jana tu pale China kabla ya IPhone, nafikiri, kutoa toleo lao jipya, China zilitoka mpya na watu wakaamini kwamba zile ndio zilikuwa ni sahihi, maana yake ni nini?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa haya yote tusiwe na ile dhana ya kudhani kwamba TCRA wanaweza wakaweka watu bandarini na airport kuzuia simu fake. Njia pekee ya kuzizuia ni njia ya matumizi ya teknolojia kama hivi wanavyotaka kufanya kwamba, kuzima simu fake, kuzidhibiti zisiweze kutumika. Na hii naamini inafanyika kwa manufaa ya wananchi wote kwa sababu, wananchi sasa watakuwa wana pata kitu halisi kulingana na fedha yao kwa sababu nina amini ni wizi kumuuzia mtu kitu cha shilingi 700,000 wakati ukweli ni kwamba ni cha shilingi 200,000 kwa sababu kilitengenezwa kwa low quality au kinaweza kikawa kwa quality isiwe low sana, lakini ukweli ni kwamba kime-infringe patent ya watu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hivyo naunga mkono hoja ya Waziri. Ahsante sana.