Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

Hon. Dr. Philip Isdor Mpango

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano kwa Mwaka wa Fedha wa 2016/2017.

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri na Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kazi nzuri wanayoifanya kuongoza Wizara hii nyeti sana na vilevile kwa hotuba yao nzuri sana ambayo kwa kweli ni ya kina. Na niseme moja kwa moja kwamba naunga mkono hoja iliyotolewa na nawaomba Waheshimiwa Wabunge wakubali kuidhinisha bajeti hii kama ilivyowasilishwa, maana hii ndio msingi wa uchumi wa viwanda ambao tunajaribu kujenga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, dunia nzima kinachotofautisha nchi maskini na nchi ambazo zimeendelea ni ubora wa miundombinu yake. Sasa tatizo ni kwamba, ujenzi wa miundombinu bora tunaihitaji wote, lakini ina gharama kubwa sana na hivyo ni lazima tuijenge kwa awamu, lakini twende kimkakati tukianza na maeneo ambayo yatatusukuma kwa haraka kama Taifa. Kwa hiyo, sequencing ni lazima na hakuna nchi yoyote ulimwenguni ambayo ina uwezo wa kujenga miundombinu yote wanayoihitaji kwa wakati mmoja. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nizichangie hoja chache ambazo zilizungumzwa humu ndani na moja wapo imejirudia ni ile inayohusu uhamisho wa fedha. Nisisitize tu kwamba, uhamisho wa fedha ambao unafanywa na Serikali baina ya mafungu na ndani ya mafungu unaongozwa na sharia; kuna vitu viwili vikubwa ambavyo vinazingatiwa katika kufanya uhamisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ni kutekeleza maamuzi ambayo yana maslahi kwa Taifa na sheria inasema hivyo, lakini la pili, unaweza ukafanya uhamisho; Waziri wa Fedha anaruhusiwa kufanya uhamisho pale ambapo kuna mahitaji ya dharura. Ukisoma Sheria ya Matumizi (Appropriation Act), inasema vizuri katika kifungu kile cha 6(1), inaeleza ni mazingira gani ambayo Waziri wa Fedha anaruhusiwa kufanya uhamisho, sijui kama ni lazima nisome, lakini Waheshimiwa Wabunge nawasihi tena kwenda kuziangalia zile sheria vizuri. Hatuwezi kufanya uhamisho kinyume cha sheria, ziko bayana, lakini vilevile Sheria ya Bajeti, Kanuni ya 28(1), inasema wazi kwamba reallocations zote kati ya mafungu ni lazima zipate idhini ya Waziri wa Fedha kwa hiyo, huwezi tu ukafanya hivi hivi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini sio hivyo tu, kifungu cha 41 kinasema vilevile kwamba kinaweka masharti ya kufanya uhamisho kati ya mafungu na kinasema; all reallocations between votes shall not exceed 5% of total government budget na haya yote tumekuwa tunayazingatia. Sasa nilikwisha liarifu Bunge lako tukufu kwamba katika mwaka huu wa fedha tulionao, Fungu 98 - Ujenzi; Bunge hili liliidhinisha shilingi bilioni 798.26 kwa ajili ya fedha za maendeleo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hadi kufikia mwezi Machi tulishatoa shilingi bilioni 931 kwa ajli ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Na nilishaeleza hili kwamba ukichukua tarakimu hizi ni kweli kabisa tumeshatoa fungu zaidi ya fedha zilizoidhinishwa na Bunge kwenye hicho kifungu, lakini narudia kwa kuzingatia maelekezo ya sheria. Fedha zilizotolewa na Serikali zilitoka Fungu 21 ambalo ni Mradi Namba 6294 ambapo Bunge, kwenye kifungu kile lilikuwa limeidhinisha shilingi bilioni 628.5 kwa ajili ya kulipia madeni mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tulihamisha fedha kutoka fungu hili kwenda fungu 98 kulipia madeni ya miundombinu kwa hiyo, nilishalieleza na fedha zilizozidi ni shilingi bilioni 133.04 ambazo ni sawa na asilimia 0.6 tu ya bajeti yote ya Serikali ya shilingi trilioni 22.5. Kwa hiyo, narudia tena katika kufanya uhamisho wa fedha tunazingatia kikamilifu Sheria ya Bajeti, hakuna mahali ambapo tunakiuka utaratibu huu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa kulisemea kulikuwa na ushauri wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kwamba tutenge fedha zaidi kwa ajili ya mindombinu na angalau ifike asilimia 20 ya bajeti yote ya Serikali. Ninawaelewa vizuri kabisa, kama nilivyotangulia kusema miundombinu ndio kikwazo kikubwa ambacho kinachelewesha maendeleo ya nchi yetu, kwa hiyo, ni ombi halali kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka ujao wa fedha 2016/2017 tumetenga zaidi ya shilingi trilioni saba kwa jaili ya miundombinu kwa maana ya uchukuzi, barabara, maji, mawasiliano, nishati na umwagiliaji. Na hii peke yake ni asilimia 24 ya bajeti yote ya Serikali, kwa hiyo, tunapiga hatua kuelekea kwenye ushauri huu ambao tuliupokea kutoka kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nisemee moja lingine ambalo linahusu Himaya ya Forodha, kwa pamoja ni Single Customs Territory, hili nilikwishalielezea, lakini linajirudia tena. Kwa hiyo, niseme mfumo huu unawezesha ushuru wa forodha wa mizigo inayoingia kwenye nchi kama ya kwetu ulipiwe moja kwa moja katika nchi ambayo mizigo ile inafikia badala ya kwenda kulipiwa kwenye destination country. Sasa huu ni mfumo mpya ambao unatumika kwa Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwa Congo pia tumekubaliana kwamba tutumie mfumo huu. Sasa wale ambao walizoea utaratibu wa zamani na wakawa wanakwepa kodi chini ya utaratibu wa zamani wanaukimbia huu ili wasilipe kodi ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nilishalitaarifu Bunge lako kwamba pamoja na kuona hitilafu hiyo, nilikwishatoa maagizo kwa TRA na Mamlaka ya Bandari kulichunguza jambo hili kuona jinsi ambavyo kweli, linaathiri kiasi cha mizigo inayopita katika Bandari yetu ya Dar es Salaam. Na nilisema hivyo kwa sababu ukiangalia trend katika bandari nyingine ulimwenguni kwa miezi ya karibuni na hususani kuanzia mwezi Januari, tunaona pia bandari nyingine ambazo haziko katika mfumo huu nazo mizigo yake imeathirika. Na nilieleza kwamba hisia mojawapo inaweza kuwa ni madhara ya kuporomoka kwa uchumi wa China ambao ume-affect biashara katika nchi ambazo inafanya nazo biashara, lakini hili linahitaji kufanyiwa uchambuzi wa kina ili kujua ukweli ni nini na kuweza kuchukua hatua ipasavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niseme pia kuhusu mgongano ambao unasema kuna mgongano wa tozo ya hifadhi za mizigo. Moja inalipwa kama customs… (Makofi)
MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa Waziri.