Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi niungane na wenzangu na kwanza nichukue fursa hii nimshukuru Mungu kwa kuwa ametujalia tuko hapa, lakini pia nichukue fursa hii nami kwanza niunge hoja mkono kwa Taarifa za Kamati ambazo zimewasilishwa hapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nichukue fursa hii niwapongeze sana Waheshimiwa Wabunge kwa michango yao mizuri waliyoichangia, lakini nichukue fursa hii nimshukuru sana Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye maeneo mbalimbali, lakini hasa kwenye jambo la kuuendeleza muungano wetu, lakini katika jambo la kuendeleza kutunza, kuhifadhi mazingira yetu na kupambana dhidi ya athari kubwa ya mabadiliko ya tabianchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumezungumzwa mambo mengi, lakini miongoni mwa mambo yaliyozungumzwa ni jambo la hoja ya muungano ambalo kwa upande wa hoja hii Waheshimiwa Wajumbe wamepongeza sana kwa hatua kubwa iliyofikiwa, lakini vilevile kumegusiwa jambo la mazingira hasa kwenye jambo la biashara ya hewa ya ukaa. Nataka niwaambie Waheshimiwa pongezi ambazo wamezitoa, hasa kwenye tasnia ama kwenye eneo hili la muungano ni kwa sababu, kwanza ya juhudi kubwa ambayo Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan anaifanya katika kuendeleza kutuunganisha Watanzania na kuhakikisha kwamba, tunaendelea kuwa kitu kimoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja za muungano zilikuwa nyingi ama changamoto zilikuwa nyingi, lakini ndani ya kipindi chake Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan zaidi ya hoja 14 amezitatua na leo muungano wetu uko salama na unakwenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kubwa zaidi katika kuendeleza timu ambayo imeundwa. Timu hii ama Kamati hii ya majadiliano ya hoja za muungano imekuwa inafanya kazi kubwa na ndio maana umefika wakati sasa imetolewa maelekezo kamati hii iwe inakutana ndani ya kipindi cha miezi mitatu; kila miezi mitatu ikutane ili lengo na madhumuni tusiendeleze kulea changamoto za muungano kwa muda mrefu, maana yake zikitokea, tukae tutatue muungano usonge mbele. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zaidi ni busara za viongozi wetu Dkt. Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mama Dkt. Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Pili wa Rais, lakini Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano nao wanafanya kazi kubwa katika kuuboresha na kuutunza Muungano huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pamezungumzwa jambo hapa la biashara ya hewa ukaa, nataka niwaambie Waheshimiwa Wabunge, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira tupo tayari na tumeendelea kuchukua hatua mbalimbali. Moja, tumeshaanzisha tumefungua kituo maalum, kituo ambacho kinatoa taarifa zote sokoine pale, kituo ambacho kinatoa taarifa zote, lakini kituo ambacho kinaendeleza kufanya utafiti. Kituo ambacho kinaendelea kusaidia wawekezaji na watu wengine ambao wako interested katika kutaka kujua juu ya suala zima la biashara hii ya hewa ya ukaa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeendelea kutoa elimu, tumeanza kwa Halmashauri, tumekwenda kwa Wakuu wa Mikoa, tumekwenda kwa Wakuu wa Wilaya, tumewapa Wabunge, wawakilishi na sasa tunataka tushuke kwa wananchi mmoja-mmoja, ili waielewe biashara hii ili lengo na madhumuni wananchi waweze kufanya biashara hii, lakini wao wapate kipato na maendeleo kupitia huduma za jamii yapatikane. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine tunaendelea kuendelea kuwashauri wananchi kuwaambia kwamba, sisi kwanza tuko tayari kushirikiana nao. Muwekezaji yeyote ambaye yuko interested na biashara hii na yuko tayari kufuata sheria na taratibu zilizowekwa kwa sababu, tulishaandaa muongozo na muongozo umeshatoka wa biashara ya hewa ya ukaa maana kule nyuma tulikuwa tunakwenda, lakini tukasema tuandae muongozo maalum ambao utawapa wananchi dira na muelekeo katika kuendeleza biashara hiyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, muongozo upo, wawekezaji waje, ili lengo na madhumuni wananchi wapate, lakini na huduma za jamii ziendelee, na tayari iko Mikoa ambayo tumeshaanza kutoa hizo huduma, hospitali zipo, elimu zipo, maji safi yapo na huduma nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, mimi niendelee tu kuunga mkono hoja hii, ahsante sana. (Makofi