Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Kuazimia Kuwahamisha Maafisa Ushirika katika Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Maafisa Ugani chini ya Wizara ya Kilimo

Hon. Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hoja ya Kuazimia Kuwahamisha Maafisa Ushirika katika Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Maafisa Ugani chini ya Wizara ya Kilimo

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza nianze kusema kwamba siungi mkono hoja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba niwakumbushe Waheshimiwa Wabunge wenzangu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ibara ya 145 na ibara ya 146 kwa ruhusa yako sijui nirejee ama muda hautoshi? Muda hautoshi, lakini Serikali za Mitaa imeandikwa kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hatuwezi kurekebisha kwa mtindo huo. Kama kuna udhaifu wa Sheria Na. 6 ya Vyama vya Ushirika ya Mwaka 2013, sehemu ya kuyafanyia marekebisho ni kuileta hiyo Sheria irekebishwe lakini siyo kwa kunyofoa vipande kwa vipande. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, maelezo ya mtoa hoja yamejieleza vizuri sana kwamba Mrajisi Msaidizi wa Ushirika wa Mkoa kwa sasa ni sehemu ya TAMISEMI, halikadhalika Maafisa Ushirika waliopo kwenye halmashauri zetu ni TAMISEMI. Tatizo liko wapi? Usimamizi unawezekana, warajisi wasaidizi wa mkoa ni sehemu ya TAMISEMI, wawasimamie vizuri hao Maafisa Ushirika kutoka kwenye halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiniuliza, iko changamoto kubwa ambapo upungufu uko kwenye hiyo Sheria Na. 6 iliyoanzisha vyama vya ushirika ya 2013 iletwe Bungeni, tuifanyie marekebisho ili warajisi waweze kufanya kazi yao vizuri na Maafisa Ushirika na Maafisa Ugani kwenye ngazi za vijiji na kata waweze kufanya kazi zao. Hatuwezi kuacha wazururaji wasimamiwe na Tume ya Ushirika kutoka Makao Makuu, kwenye Tawala za Mikoa hakuna, kwenye Halmashauri Mkurugenzi hawajui, Madiwani hatuwajui, watakuwa wanafanya kazi za nani? Ugatuaji (D by D) lazima iendelee. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nakushukuru. (Makofi)

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.