Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hoja ya Kuazimia Kuwahamisha Maafisa Ushirika katika Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Maafisa Ugani chini ya Wizara ya Kilimo

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hoja ya Kuazimia Kuwahamisha Maafisa Ushirika katika Tume ya Maendeleo ya Ushirika na Maafisa Ugani chini ya Wizara ya Kilimo

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, cha kwanza nianze kukushukuru kwa kunipa nafasi na nianze kwa kusema mambo mawili makubwa. Changamoto ambazo mtoa hoja amezitaja ni changamoto ambazo zipo lakini changamoto hizi msingi wake ni changamoto zinazotokana na administration ni suala la utawala. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, dhana ya D by D Wizara ya Kilimo haina mkulima Wizarani. Mkulima yuko wilayani na kule wilayani aliko anatakiwa asimamiwe na Afisa Ugani aliyeko wilayani. Kama Wizara na Bunge lako tukufu lilitielekeza hapa kwamba tulete mabadiliko ya sheria ya ushirika ambayo tunaifanyia kazi ili tuweze kutatua changamoto zilizopo kwa sababu hoja siyo kwamba nani amsimamie nani? Hoja iliyoko ni kwamba afisa kilimo aliyeko katika ngazi ya halmashauri atimize wajibu wake na kufanya kazi inayostahili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sisi sasa hivi kama Wizara tukishirikiana na wenzetu wa TAMISEMI tunapitia Sheria ya Tume ya Ushirika ambayo itayapitia mapungufu yote ya kiutawala yaliyoko na ya usimamizi katika sekta ya ushirika. Vilevile, tunapitia upya Sheria ya Tume ya Umwagiliaji ambayo inatupa mamlaka ya kwenda kuanzisha ofisi za umwagiliaji katika ngazi ya wilaya na kuweza kuwasimamia maafisa kilimo walioko katika ngazi ya wilaya na vijiji bila kuathiri D by D. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nawaomba Waheshimiwa Wabunge watupe nafasi wasubiiri tulete mabadiliko ya sheria hizo halafu tutatoa ushauri kutokana na jambo…(Makofi)
MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

SPIKA: Nani anataka kutoa taarifa? Sawa Mheshimiwa Zuberi Kuchauka.

TAARIFA

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, nataka nimpe taarifa mzungumzaji amechangia vizuri. Shida iliyopo ukienda kwenye kata zetu kama mtendaji kata hayupo hachukuliwi mwalimu mkuu akawe mtendaji wa kata wala hachukuliwi mganga mkuu akawe mtendaji wa kata anachukuliwa afisa kilimo ndiyo anaenda kukaimu mtendaji kata kwa maana wanaonekana kwamba maafisa kilimo wa kata hawana shughuli. Halafu hoja nyingine inakuja wanasema hawa maafisa kilimo…

SPIKA: Mheshimiwa taarifa huwa ni moja tu Mheshimiwa. Mheshimiwa Bashe unaipokea taarifa hiyo?

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, taarifa yake ni suala la utawala tu ni suala la usiamamizi, ni suala la maafisa kilimo kutokusimamiwa na kutokufanya kazi na ni suala la maafisa kilimo kutokuwezeshwa. Kwa hiyo, ninachotaka ni-appeal kwa mtoa hoja na ni-appeal kwa Waheshimiwa Wabunge kama Waziri wa Kilimo ninaesimamia sera na masuala ya uratibu wa shughuli za kilimo ninatambua changamoto zilizoko katika ngazi ya halmashauri, ninatambua matamanio ya Waheshimiwa Wabunge na ninatambua matamanio ya wakulima.

Mheshimiwa Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge mtuache tumalizie kazi tunayoifanya ndani ya Serikali ili kutatua changamoto zilizoko zinazowakabili maafisa ugani na zinazokabili suala la ushirika ambazo… (Makofi)

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, taarifa.

WAZIRI WA KILIMO: na maafisa ushirika ambazo zitatuliwa… nimalizie, ambazo zitatuliwa tutakapoleta mabadiliko ya sheria ya Tume ya Ushirika…

SPIKA: Haya ahsante sana kuna taarifa…

WAZIRI WA KILIMO: lakini tutakapoleta mabadiliko ya sheria ya Tume ya Umwagiliaji bila kuathiri…

SPIKA: Kuna taarifa Mheshimiwa Bashe, Mheshimiwa Ole-Sendeka

TAARIFA

MHE. CHRISTOPHER O. OLE-SENDEKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa niungane na mawazo mazuri sana ya Mheshimiwa Bashe. Naunga mkono hoja ya kutungwa kwa sheria inayowadhibiti hawa maafisa wa ushirika. Mheshimiwa Bashe ni shahidi alipokuja Njombe alikuta ufisadi wa vyama vya ushirika na tukalazimika kuwakamata wale waliohusika ambvapo baadae tulikusanya shilingi bilioni 5.5 kutoka kwa mafisadi wa vyama vya ushirika na SACCOS. Sheria ilikuwa vibaya tulipokuwa tunaomba ushauri wanasheria. Kwa hiyo, sheria ibadilishwe bila kuathiri D by D.

SPIKA: Haya huyu nadhani yeye hajatoa taarifa ameunga mkono unachosema na kengele imeshagongwa, sekunde 30 malizia.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nataka nimalizie kwa kumuomba mtoa hoja kama Serikali tunafahamu tatizo linalokabili Sekta ya Ushirika na tunafahamu tatizo linalokabili Sekta ya Ugani. Watupe nafasi tumalizie michakato hii ya kisheria ambayo itaenda kutatua masuala ya utawala na ugatuaji lakini vilevile itatatua tatizo la upelekaji wa rasilimali na usimamizi wa maafisa ugani. (Makofi)