Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Raphael Michael Japhary

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. RAPHAEL J. MICHAEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea hapo alipoishia mchangiaji aliyepita ambaye amenipa muda wake wa dakika tano, naomba niongelee mambo machache sana ya Jimbo langu la Moshi Mjini katika suala la nishati. Napenda kuongelea kwenye upande wa nishati mbadala kama ilivyoandikwa kwenye hotuba ya Mheshimiwa Waziri katika page ya 60 na Serikali imeonyesha kwamba, imepitia maeneo ambayo wanadhani kwamba, wanaweza wakawekeza kwenye umeme wa upepo na umeme wa jua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nadhani ni mpango mzuri, lakini sijui kwa nini umechelewa kiasi hiki kwa Taifa letu la Tanzania. Pamoja na yote hayo, nataka nisisitize kidogo kwenye suala la matumizi ya takataka zetu, miji yetu mingi inazalisha takataka nyingi, lakini Serikali haijawa tayari kuwa na matumizi bora ya takataka hizi na matokeo yake tumekuwa tukizalisha maradhi ya kila siku na kuharibu mazingira kila wakati, wakati tunaweza tuka-control hiyo situation.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nachukulia mfano Manispaa ya Moshi; Manispaa ya Moshi tuna mradi wa kutumia jalala letu ambalo ni semi-land fill ambalo lina uwezo wa kuzalisha methane gas ambayo inaweza ikatumika kupunguza sana matatizo ya nishati ya umeme katika mji wetu wa Moshi. Bahati nzuri tumeshafanya feasibility study na bahati nzuri tumeshapata ushirikiano wa wenzetu wa mji dada wa Tubingen, Ujerumani kwa hiyo, tuko katika hatua nzuri ya kutekeleza mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunachohitaji ni msukumo wa Serikali katika hili kwa sababu, haionekani kama vile Serikali imeweka mkazo katika eneo hili. Kwa hiyo, tunahitaji msukumo wa Serikali katika hili, ili wale watu wa Ujerumani watusaidie kufikia malengo yetu kwa sababu tayari tumeshatumia fedha za own source katika kutekeleza mradi huu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, tunahitaji committment ya Serikali kwamba, wenzetu wa Ujerumani wametuambia kama tuki-raise cost ya mradi, wao wako tayari ku-raise 80% na sisi tu-raise 20%. Uwezo wa halmashauri kufanya kazi hii ni mdogo, lakini tunaamini kama Wizara itaji-commit itatusaidia sisi kupata 20% ili huo mradi utekelezwe mapema zaidi. Namwomba Mheshimiwa Waziri, aifanye Moshi pilot area ya mradi wa methane gas ambayo itasaidia sana kuzalisha umeme ili maeneo mengine yaige katika nchi hii ya Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna suala lenye shida katika Manispaa yangu ya Moshi katika Jengo la Stand kuhusu suala la umeme. Wananchi wanaomiliki vibanda katika Jengo la Stand yetu Kuu, jengo ambalo ni mali ya Manispaa, wametaka kuwekewa LUKU, lakini TANESCO wamekataa kuwafungia LUKU wakisema kwamba, mpaka wapate kibali cha Waziri. Sasa wale wananchi hawako tayari kuletewa bili na landlord ambaye ni manispaa. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri atoe kibali, ili wananchi wale wa Manispaa ya Moshi wafungiwe zile LUKU ili waweze kuendesha shughuli zao kirahisi kuliko kupata usumbufu usio wa lazima.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la tatu ni suala la biogas. Ukiangalia page ya 28 ya hotuba hii, biogas imeonekana kuelekezwa zaidi maeneo ya vijijini kupitia mradi wa REA na miradi mingine. Hata hiyo 3.2 billion iliyotengwa inaonesha ni kwa maeneo ya vijijini, lakini maeneo ya mjini watu wanafanya zero grazing, kwa hiyo, wanapata resources ambazo zinafaa kwa biogas na hitaji muhimu sana la wananchi, ili kupunguza matumizi ya kuni na ya mkaa ambayo siku zote tumekuwa tukikimbizana na tunagombana na wananchi kwa sababu, wanatumia mkaa na kuni na wengine mpaka tunawafunga.
Mheshimiwa Mwenyekiti,kwa hiyo, naomba maeneo ya mjini ikiwemo Manispaa ya Moshi mradi huu uwe considered kufika katika eneo hili ili wananchi wangu wa Manispaa ya Moshi nao wafaidike na mradi huu wa Serikali. Naamini tukilitekeleza hili tutaweza kukabiliana na hali halisi ya uchafuzi wa mazingira. Bado naamini, Serikali yetu haijawekeza vizuri katika solid waste management ambayo ni teknolojia itakayosaidia sana maendeleo ya nishati katika dunia tunayoishi leo. Ukienda Nchi za Ulaya…
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa kwa mchango wako.