Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nami kwa moyo mkunjufu kabisa japokuwa najua hawanioni, niwashukuru wananchi wa Jimbo la Kawe, kwa kunipa heshima kubwa, najua kuna watu walifikiria lile Jimbo nimeazimwa miaka mitano, sasa hii nguvu ya kuingia mara ya pili kwa tofauti ya kura 17,000 nadhani imetuma somo huko, mjue kwamba watoto wa kitaa wamenisoma vizuri na uzuri upande wa huko wengi ni wananchi wangu, kwa hiyo mtanivumilia kwa kipindi hiki cha miaka mitano. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane kabisa na Mheshimiwa Peter Serukamba alivyozungumza asubuhi, baada ya Kamati ya Bajeti kuundwa, Chenge one na Chenge two, ilitoa mapendekezo ya kina baada ya Kamati kujadili, baada ya Bunge kujadili, na Kamati kwenda ku-compile, ilitoa mapendekezo ya kina ya vyanzo mbadala vya kodi vya Serikali. Leo tunakuja hapa, yaani ni kama vile akitoka Rais huyu, akiingia Rais mwingine, ni kama vile imetoka mbingu, imekuja dunia, hakuna connectivity.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua kuna Wabunge ma-junior hapa, tuko asilimia thelathini (30%) tumerudi ma-senior, lakini nawaambieni hii miaka mitano lugha ninayoizungumza leo mtakuja kuizungumza 2019. Serikali ya Chama cha Mapinduzi, mmechoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana Zanzibar wamewakataa mnataka kulazimisha, ndiyo maana Tanganyika waliwakataa Tume ya Taifa ya Uchaguzi ikawabeba beba tu kindakindaki na ninyi mnajua. Nashukuru Mpango ametusaidia, katueleza yaani jinsi Serikali ya Chama cha Mapinduzi ilivyo-fail kwenye huu, alivyo review miaka mitano, anatuambia.
Mheshimwa Mwenyekiti, Reli mlipanga kukarabati, Reli ya Kati, kilometa 2,700, mmeweza 150 hivi hamuoni aibu? Halafu mtu anakuja hapa anasifia tu vyanzo tulishawapa Kambi ya Upinzani iliwapa miaka mitano iliyopita, kila mwaka tunawapa. Kamati ya Bajeti iliwapa mnakuja mnaumiza vichwa vya watu hapa for nothing.
Mheshimiwa Mwenyekiti, haya mabehewa ya Mwakyembe, 274 tunaambiwa na yenyewe feki, yaani hayo yenyewe ndiyo yamenunuliwa basi na yenyewe Mheshimiwa Sitta katuambia siyo sisi, akaunda Kamati yake pale Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara Mzee Magufuli mwenyewe…
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Kuhusu utaratibu...
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mwakyembe ahsante kwa taarifa, tunaomba Mheshimiwa Halima Mdee uendelee.
MHE. HALIMA J. MDEE: Walikwambia wewe ni jipu? Sikiliza, mimi nimesema hivi, kwa mujibu wa Mheshimiwa Samuel Sitta alivyoenda Wizara ya Uchukuzi aliyasema hayo maneno. Sasa hayo mambo mengine wakamalizane wao wenyewe. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara, alikuwa Mheshimiwa Magufuli. Walijipanga kujenga na kukarabati 5,204, wameweza kukarabari 2,700, na ni kati ya Mawaziri ambao walikuwa wanakuja na vitabu vikubwa sana na mikwara mingi, lakini kumbe hata nusu ya lengo haijatimia, Chama cha Mapinduzi.
NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu utaratibu...
MWENYEKITI: Ahsante, naomba Halima uendelee.
MHE. HALIMA J. MDEE: Halafu hii biashara ya kufanya Rais hashikiki, wala hakamatiki wakati sisi jukumu letu ni kuisimamia Serikali ikome. Mimi hapa nimerejea…
MWENYEKITI: Naomba utumie lugha ya staha Bungeni kwa mujibu wa taratibu.
MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesema hivi hii biashara ya kufanya Rais ni mtu ambaye hashikiki, hagusiki, hatajwi, hazungumzwi iishe kwa sababu jukumu la Bunge ni kuisimamia Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, rejea niliyoitoa hapa ni mafanikio ya …
MWENYEKITI: Mheshimiwa Halima naomba ukae, Mheshimiwa Waziri azungumze...
MWENYEKITI: Mheshimiwa Mdee naomba uheshimu Kanuni na katika mazungumzo.
MHE HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mpango wa Miaka Mitano iliyopita, wakati Mheshimiwa Magufuli ambae sasa ni Rais, alipokuwa Waziri wa Miundombinu hatimae Ujenzi na kila kitu, barabara zilizotakiwa kukarabatiwa na kujengwa ni kilomita 5,204 lakini sasa hivi tunaambiwa zilizokarabatiwa ni 2,775 kilometa. Kidumu Chama cha Mapinduzi! (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu kuna watu hapa wanazungumza utafikiria hii Serikali ni mpya, kumbe ninyi tokea mwaka 1961 mmepata dhamana kuanzia TANU mpaka CCM, watu tunaumiza brain tunatoa mawazo hamfanyi kitu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Kilimo: Tukija kwenye sekta ya kilimo kimekua kwa asilimia 3.4 tuliokuja Bungeni miaka 10 iliyopita, kilimo kilikuwa kimekua kipindi kile kwa asilimia minne, tena malengo ya Serikali ilikua ni asilimia 10. Serikali ilivyoona inabanwa ikashusha mpaka asilimia sita. Leo tunaambiwa kilimo kimekua kwa asilimia 3.4 maana yake kwanza mmeshuka chini. Ile asilimia sita imekuja hapa chini mmeshindwa kui-balance, halafu mnasema eti mapinduzi ya kilimo! Hapa kazi tu! Yaani, kilimo cha umwagiliaji, wakati mkoloni anaondoka, tuna hekta za umwagiliaji 400,000, ninyi hapa mmetushusha mpaka 345,000 halafu mmnatuambia mmeongeza asilimia 46, wakati mnajua miaka mitano iliyopita tulikuwa tuna hekta 350,000. Yaani mnacheza na mahesabu, figure iliyokuwepo mnaongeza 5000 halafu mnajumlisha mnasema ni mafanikio. It is a shame! (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka sijui 64 baada ya uhuru, asilimia 10 ya wananchi wana hati za kawaida na hati za kimila, hivi migogoro ya ardhi itaacha kuwepo? Miaka 64 sijui 54 baada ya uhuru, asilimia 20 ya ardhi yetu ndiyo ipo kwenye mipango, hivi mgogoro wa wakulima na wafugaji itaacha kuwepo? halafu inakuja Serikali hapa inaleta mpango, ime-adress vipi hivi vitu ambavyo ni critical, hakuna! Eti! mnaenda mnabomoabomoa Dar es Salaam, hivi tungekuwa na utaratibu wa kuwapa Watanzania maskini viwanja kwa gharama nafuu, kuna mtu anataka kwenda kujenga mtoni? Kuna mtu anataka kujenga mabondeni? Viwanja vya Serikali huna milioni sita, huna milioni saba hununui kiwanja, tena milioni 10, milioni 20 hununui kiwanja!
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni hivi, vipaumbele, miaka mitano iliyopita tulikuwa tuna miundombinu, tulikuwa tuna kilimo, tulikuwa tuna viwanda, tulikuwa tuna human development, tulikuwa tuna tourism, miaka mitano baadae majamaa yamegeuka, viwanda, kufungamanisha maendeleo ya watu, miradi mikubwa ya kielelezo, ujenzi wa maeneo wezeshi, yaani kilimo wameweka pembeni, kinaajiri asilimia 70 ya Watanzania, inachangia asilimia 30 ya pato la taifa, asilimia 40 ya fedha za nje umeweka pembeni, halafu unatuambia eti hivi vitu tulivyoviacha viporo vitajumuishwa, vinajumuishwaje kama havipo kwenye kipaumbele? Tutatengaje bajeti kama haipo kwenye kipaumbele?
MHE HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, niungane na Kamati ambayo imesema hivi ni muhimu kama kweli tunataka kuwasaidia Watanzania. Kama tunataka kuwasaidia Watanzania lazima tuingize kilimo kama kipaumbele cha msingi. Kamati ya Bajeti imesema na tukiingiza kilimo tutenge bajeti, mwaka jana tulikuwa tunasema hapa kwamba haiwezekani kitabu cha maendeleo cha Wizara ya Kilimo, fedha za maendeleo kwenye vocha ya kilimo imetengewa bilioni 40 wakati Jakaya Mrisho Kikwete ametengewa bilioni 50 kusafiri nje. Kwa hiyo, kama we mean business tuwekeze kwenye kilimo, tutapunguza Watanzania hao maskini kuwa wategemezi kwa Serikali.
MHE, HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo lazima miundombinu irejeshwe sababu kama tunataka viwanda, hivi viwanda bila uzalishaji kuna viwanda au kuna matope? Kwa hiyo lazima….
(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)