Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa na Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha uliuoishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishi tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezajiwa wa Mitaji ya Umma kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa na Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha uliuoishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishi tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezajiwa wa Mitaji ya Umma kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru kwa kunipa nafasi hii, nitumie nafasi hii kumshukuru sana Mwenyezi Mungu Mwingi wa Rehema kwa kutujalia uhai. Nipongeze Kamati zote zilizowasilisha taarifa kwa niaba yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakuwa na mchango kwenye maeneo matatu. Kwenye Taarifa ya Kamati ya LAAC ukurasa wa 10 wanatoa mapendekezo baada ya kufanya tathmini na kuona kwamba kuna shida kwanye makusanyo kwenye halmashauri zetu. Kwa maana hiyo, Kamati ya LAAC inapendekeza ubunifu wa vyanzo vipya vya mapato.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni jambo jema, na kwa uzoefu wa miaka kadhaa tukipokea taarifa za CAG kumeonekana udhaifu kwenye makusanyo ya Halmashauri zetu, lakini vilevile kuna umuhimu wa kuanzisha vyanzo vipya vya mapato. Lakini mimi nilikuwa na mtazamo tofauti. Tuna vyanzo vingi vya mapato na katika vyanzo tulivyonavyo, baadhi vinakuwa ni kero kwa wananchi. Hii ni kwa sababu, moja, kunakuwa hakuna ufanisi kwenye vyanzo tulivyonavyo katika makusanyo yake. Matokeo yake ni kwamba kila mwaka taarifa inayoletwa inaonekana kwamba hatufikii malengo; lakini si kwamba vyanzo havipo. Vyanzo vipo lakini tuna udhaifu kwenye makusanyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo kinachopaswa si kuendelea kubuni vyanzo vipya kila kukicha bali mimi ninachokifikiri, katika vyanzo tulivyonavyo tuweke mifumo thabiti ya kuhakikisha kwamba ukusanyaji wa mapato kwenye vyanzo tulivyonavyo unakuwa ni wenye ufanisi; lilevile tunaziba mianya ya upotevu wa fedha kwenye vyanzo tulivyonavyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mianya mingi sana inayopelekea upotevu wa mapato kwenye halmashauri zetu kupitia vyanzo vya mapato tulivyonavyo. Kwa hiyo, badala ya kuendelea kubuni vyanzo vipya vya mapato ambavyo vingi vinaweza vikawa ni kero kwenye jamii, zaidi tuwekeze kwenye kuongeza ufanisi kwenye makusanyo kwenye vyanzo tulivyonavyo na kuziba mianya ya upotevu wa fedha kwenye vyanzo hivi na hatimaye tutafikia malengo kuliko kuendelea kubuni kila kukicha vyanzo vipya ambavyo vingine vinakuwa ni shida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye ripoti ya CAG kama ambavyo imewasilishwa na Kamati, kupitia mashine za ukusanyaji (POS). Kulikuwa na upotevu wa takriban shilingi bilioni 11.07. Fedha hizi ni kwa sababu tu, ya kutokudhibiti mianya hii ya upotevu wa mapato. Kwa hiyo, niendelee kusisitiza, kwa kutumia Kamati zetu; lakini kwa kuwa Serikali mpo, tujenge mfumo ambao utaondoa udhaifu huu ili vyanzo hivi tulivyonavyo viwe ni vyenye tija lakini vilevile ufanisi katika ukusanyaji wa mapato kwenye vyanzo hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la pili ambalo nilitaka kuchangia ni kuhusu ubadhilifu kupitia manunuzi kwenye halmashauri zetu. Nimpongeze Mheshimiwa Rais anafanya kazi kubwa sana. Hakuna kipindi ambacho tumepokea fedha nyingi kwenye majimbo yetu kama kipindi hiki. Mheshimiwa Rais amefanya kazi kubwa sana kuhakikisha kwamba fedha zinapatikana, miradi ya maendeleo inapatikana kwenye majimbo yetu. Jukumu tunalokuwa nalo na ambalo tumeonesha udhaifu mkubwa ni kwenye kuthibiti fedha kwenye maeneo yetu kama ambavyo wachangiaji wengi wamesema, juu ya ubadhilifu unaofanywa na watendaji kwenye halmashauri zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa natafakari baada ya kupitia taarifa hii, kwamba kwa mfano tumepoteza kwa sample ya halmashauri kadhaa zilizohojiwa na Kamati; kwamba bilioni 3.29 zimelipwa kwenye halmashauri zetu kwa ajili ya manunuzi ya vifaa ambavyo havijaweza kupokelewa; unaweza kuona. Kwa mujibu wa sheria, ukiangalia Sheria ya Manunuzi, Kanuni namba 242 na 248 inaonesha wazi taratibu gani zinapaswa zifuatwe wakati wa manunuzi. Kama inatokea fedha zinalipwa, bidhaa hazijaletwa matokeo yake halmashauri itapokea bidhaa ambazo zina mapungufu au zisizokidhi viwango.

Mheshimiwa Mwneyekiti, na kama imechukuliwa kwa sampeling pekee, je, kwa halmashauri zote tumepoteza fedha kiasi gani? Kwa hiyo, tuna jukumu kama Bunge kuishinikiza Serikali iweze kusimamia eneo hili. Kwa sababu kanuni zipo, kusingekuwa na kanuni tungekuwa hakuna mahala ambapo tunaweza tukasema kwamba inawezekana kuna udhaifu, lakini udhaifu uliokuwepo sasa ni kwenye usimamiziwa kanuni hizi. Kwa hiyo niombe Serikali iliangalie jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la mwisho ambalo nilifikiri nilichangie ni juu ya miradi inayotekelezwa kwa force accont. Kwenye Taarifa ya Kamati imeonesha udhaifu kwenye miradi inayotekelezwa kwa mfumo wa force account. Kifungu namba 64 cha Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2011 na Kanuni zake, inaoneshani miradi gani na kwa mfumo upi miradi miradi inaweza kutekelezwa kwa force accout.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mmoja kati ya watu wanaoamini katika mfumo wa Force account katika utekelezaji wa miradi yetu. Tatizo tunalokuwa nalo ni kwenye usimamizi. Hii ningependekeza, ukiangalia uzoefu wa miradi yetu tunayoitekeleza kwa mfumo wa force account, shida kubwa sana inatokea kwenye usimamizi na kufuata taratibu zinazoweza kusimamia utekelezaji bora wa miradi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeshauri, kama ambavyo baadhi ya nchi nyingine zimefanya. Nilikuwa ninapitia kijarida hapa cha nchi ya Zambia ambacho ninafikiri na sisi kama taifa tungeona umuhimu kwamba, tuwe na sera ya monitoring and evaluation ya kitaifa ambayo inaweza kufanya kazi kwa kusimamia miradi yetu ya maendeleo kwenye ngazi zote. Kwenye eneo la kitaifa, mikoa, wilaya, Wizara na kadhalika. Tukiwa na national policy ya monitoring and evaluation ninaamini miradi yetu mingi kwa kutumia mfumo huo wa force account inaweza kuwa na tija na fedha tunazozitumia kwa ajili ya kutekeleza miradi hii ikawa na tija kwa taifa letu na wananchi waka-benefit kutokana na fedha hizi ambazo zinapelekwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi kwenye maendeleo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru sana kwa nafasi. Ahsanteni sana. Ninaunga mkono hoja. (Makofi)