Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Kwanza kwa sababu ya muda nichukue muda huu kupongeza Kamati ya Ardhi, Maliasili, Mazingira na Utalii kwa kazi nzuri ambayo wameifanya hapa, nipongeze pia Serikali Wizara ya Ardhi na Maliasili kwa kazi wanazojaribu kufanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaongelea kidogo kuhusu migogoro. Tumeona data hapa kwamba vijiji viko 12,318 hivi, halafu vijiji vilivyopimwa na kuwa na matumizi bora ya ardhi ni 3,681, halafu ambazo bado ni karibu 8,638 hivi, sasa hii inatisha kidogo, kwamba migogoro ambayo imekuwepo kwa muda mrefu baina ya vijiji na hifadhi, Wilaya - Wilaya, Kijiji kwa Kijiji, lakini kubwa zaidi migogoro inaondoa raha sana kutoka kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vyema Wizara na specifically Tume hii Taifa matumizi bora ya ardhi kama walivyosema Kamati wapewe pesa nyingi sana ili tukiondokana na migogoro haya mengine yote tunayapanga itawezekana, bila kupima vijiji kwanza, mipaka ikafahamika na matumizi ya ardhi yakawekwa vizuri migogoro inaweza ikaendelea kwa miaka na miaka. Kwa hiyo ni vema pesa zikatengwa za kutosha kwa ajili ya Tume hii ya Taifa ya Mipango na Matumizi bora. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukifanya hivyo itaondoa migogoro na migogoro nadhani ndiyo easiest kuliko kutafuta pesa za barabara. Hilo ni rahisi kuliko yote, tuliambiwa hapa kwamba Kijiji sijui milioni 15, kama ndiyo Tume inasema hivyo, sasa tutashindwaje kutafuta bilioni 300 kweli ili tumalizane na migogoro ili haya mengine yote tunayoyapanga iwezekane, hilo la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulibadilisha sheria hapa ya kuondoa mamlaka kwa Mabaraza yale ya Kata, sasa tunataka ije kwenye Mabaraza ya Wilaya na nadhani thinking ni kwa sababu sheria hawa wanafahamu zaidi. Tunatarajia Wizara ya Ardhi sasa muanze kuajiri hawa ili sasa migogoro isirundikane bure. Kwa mfano, Kiteto Mheshimiwa Naibu Waziri wa Ardhi nakumbuka na nawapongeza sana kwa kuja Kiteto na timu yenu mnahangaika sana, mnakwenda kila mahala na Waziri wako, ndio maana Waziri wako karibu nywele kichwa chote kinakuwa nyeupe na wewe kila siku mnapishana, lakini Jimbo la Kiteto ambalo kila siku nazungumza hapa migogoro ni mingi mikubwa kuliko Mkoa halafu bado mnatuletea Mwenyekiti anayetembelea sijui anatoka wapi? Mheshimiwa Waziri mtuletee Mwenyekiti wa Balaza la Ardhi Kiteto awe pale full time ili migogoro ishughulikiwe na kwingine kote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo jingine Wizara ya Ardhi kuna clip ya Mheshimiwa Rais Mstaafu ilikuwa inatembea hapa siku za hivi karibuni kusema hii Wizara yenu bwana kuna watu wagumu kwelikweli, sasa sijui ni changamoto na hiyo imegeuka kuwa nayo ni changamoto ama ni confusion iliyopo kwamba wale Maafisa Ardhi waliopo Wilayani hawajulikani kama wako Halmashauri ama wako kwenu ni kama wana-hang tu hivi, ni vyema mkaweka hili sawa ili na wale waanze kufanya kazi huko Wilayani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nirudi Maliasili na Utalii, kwanza nimpongeze Waziri na Naibu Waziri kwa kuja na huu mpango wa kukutana na Wabunge Mikoa, nadhani itawajengea fursa ya kufahamu changamoto nyingi kutoka kwa watu wanowakilisha wananchi hapa ambao ndiyo wanatupa kura hapa. Sasa mkichanganya na ripoti zile za wataalam wenu na nyinyi mkapata na picha huku nadhani mtatengeneza majawabu ambayo ni mazuri kwa watu na uhifadhi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo nitajikita kwenye WMA zaidi na WMA nchini kuna WMA karibu 38 hivi, lakini 22 ndio ziko active kidogo na Kiteto tuna WMA, Mahakama ya WMA lakini kuna Waheshimiwa Wabunge wengi sana hapa wana WMA, Mwenyekiti wa Bunge Mheshimiwa Baran Sillo ana WMA ya Bunge Mheshimiwa Mpakate ana WMA, Mheshimiwa Kuchauka, kuna Wabunge zaidi kama 30 hivi, Dkt. Steven Kiruswa kule Longido.

Mheshimiwa Mwenyekiti, WMAs zilianzishwa na Sera ya Wanyamapori ya mwaka 1998 na nia ilikuwa ni kwamba pamoja na kwamba tuna maeneo ya hifadhi (core protected areas); maeneo mengine ya kufanya uhifadhi bila kubugudhana na watu ni kushawishi watu washiriki kwenye suala la uhifadhi. Kwa hiyo, wananchi wanatenga ardhi zao, halafu wanapewa mamlaka ya kuingia mikataba na wawekezaji. Kwa hiyo, nimependa sana Kamati walivyoweka hapa kwamba WMA siyo Hifadhi za Taifa wala siyo extension ya National Parks, siyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama walivyosema Kamati, WMA siyo Hifadhi ya Taifa wala siyo mwendelezo wa Hifadhi za Taifa, hizi ni ardhi za vijiji, ambacho wanachofanya ni wanafanya mnachofanya ninyi, kuhifadhi. Sasa nadhani ingekuwa ni jambo jema kama Hifadhi za Taifa za hizi za kijamii zikafanya kazi pamoja na mkashindana kibiashara bila kusumbuana, kwa sababu lengo ni lile lile. Data hapa zinatuambia pamoja na mbuga zote ishirini na ngapi sijui, asilimia 65 mpaka 70 ya wanyamapori wako nje ya hizi tunazoziita core protected areas na logic ni simple tu, mnyama wala hajui kwamba eti ndio na cross Serengeti sasa kwa hiyo anaanza ku-vibrate kwamba navuka mpaka wa Serengeti, no these are free agents, wanakwenda kila mahali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo unless tu-improve mahusiano zaidi na watu ndio itafanya uhifadhi uwe complete. Itakuwa ni kujidanganya sana kama mnafikiri mtafanya uhifadhi bila ku-involve watu, hiyo haitowezekana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Waziri task kubwa ni kuangalia mahusiano, mahusiano ya wananchi na hifadhi na wanyamapori. Siku mkitengeneza balance nzuri sana uhifadhi utakuwa umekamilika vizuri sana na utakuwa na manufaa makubwa zaidi kwa nchi na kwa wananchi wenyewe. Tutaongea mengi zaidi tukikutana kwenye Kamati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kilichonifurahisha sana leo ni Maazimio ya Bunge kuhusu pesa za WMA; WMA wamepewa Madaraka, wanasaini mikataba na wawekezaji, mwekezaji kalipa hela halafu hela haziji. Hawa wanashindwa kulipa mishahara, wanashindwa kufanya kazi za uhifadhi, wanashindwa ku-control majangili kwa sababu pesa zimekwama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii kwa kweli Kamati kwa kweli shikamoo Kamati, kama ndio Mwenyekiti ndio anapokea kwa niaba yenu. Mmefanya jambo ambalo limetusumbua kwa muda mrefu kidogo. Azimio lenyewe; Serikali ihakikishe inarejesha kiasi chote cha fedha kinachostahili kwenda WMA na naambiwa na watu wa WMA wanadai kama four point something billion sasa. Kwa hiyo, mlete hiyo haraka kama lilivyosema azimio hapa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lingine zuri sana mtengeneze mpango wa kuhakikisha kwa sababu tumeshakubaliana kikanuni, kila mtu anapata nini hapa, WMA percent ngapi, Serikali, wilaya na wawekezaji na wao wako tayari, kwani akiandika cheque tatu kila mtu akapata kwa wakati kuna shida gani? Kwa hiyo, kama azimio hili lilivyoweka vizuri tunataka hela za WMA ziende directly, hizi za kwenu zinazokwenda Hazina kwanza ziende huku, hiyo vita ni yenu wenyewe kwa wenyewe lakini hizi za wananchi angalau ziende straight ili mambo ya uhifadhi na pia isilete migogoro kati ya WMAs na wawekezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu leo you can imagine an investor ana-sign mkataba na WMA hela haziji, halafu anaye-hold hela siyo sehemu ya mkataba, anaye-hold hela ana-frustrate ile agreement kwa sababu ya ku-hold hela. Kwa hiyo, sheria kama ilivyokuwa inasema hizi hela ziende, kwa kweli hapa Kamati mmetufanya sisi ambao tunatoka maeneo haya, tumefurahi sana na WMA nchi nzima leo nadhani zinafuatilia sana hili na wamefarijika sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la mwisho, narudi kwenye mahusiano, mimi nawaambia wananchi wangu wa Kiteto, hizi fidia hizi tunazozungumza hapa, kanuni hizi ambazo mmesema kifuta jasho, sijui ni kifuta nini, halafu haziji na zinachelewa. Mimi Kiteto pekee yake wananchi wameleta forms zaidi ya 223 lakini kesi za mifugo 21, majeruhi wanne, vifo vinavyotokana na wanyamapori.

Mheshimiwa Mwenyekiti, is very unfair, leo tembo anavuruga shamba lote na wananchi wale hawalali kila siku wako mashambani. Halafu tembo au wanyamapori anakuja anavuruga, halafu mnaniambia shilingi 500,000 na shamba lote eka mia, mia mbili lote limevurugwa.

Kwa hiyo, kati ya vitu ambavyo kwa kweli ningetamani hii kanuni mmelete haraka sana ili turekebishe ili wananchi hawa wasivunjike moyo ambao hawalali usiku na mchana wakijaribu kulima ili wanufaishe nchi na Taifa kwa ujumla. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nafurahi na nashukuru sana, ahsanteni sana. (Makofi)