Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia jioni hii ya leo. Naamini kabisa kwamba, katika historia ya bajeti ya Nishati na Madini na hususan katika Mafungu ya Maendeleo Wizara hii imevunja rekodi kwa safari hii. Wamepewa fedha za kutosha, japo kuandikwa katika vitabu ni suala moja, sasa tungojee wakati wa kugawa mafungu haya kwa Wizara hii husika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa bahati nzuri Mheshimiwa Waziri ni kipindi kifupi kilichopita alitembelea Mkoa wetu wa Kagera na sehemu mojawapo alitembelea Manispaa ya Bukoba Town, mojawapo ya kazi ambayo tuliifanya baada ya kuongea naye ni suala la kufikiria kuweza kutupa umeme katika vijiji mji vya Mji wa Bukoba ambavyo kimsingi haviko katika programu ya REA. Naamini Mheshimiwa Waziri anatambua kabisa nyaraka husika zimeshafika kwenye ofisi yake kama alivyohitaji, tunaomba vijiji vya Nyanga, Kitendagulo, Ijuganyondo, Buhembe, Kibeta, Kagondo pamoja na visiwa ambavyo kule Bukoba tunaviita Pemba na Unguja ndogo, bila shaka tunaamini Waziri atatimiza ile azma na matumaini aliyowaachia wananchi wa Bukoba Town kwamba vijiji mji hivi atavitafutia fursa ya kuviingiza katika mpango wa REA. Vijiji hivi pamoja na kuwa katika eneo la mji ni vijiji ambavyo kwa kweli maisha yao ya kila siku ni sawasawa na maeneo mengine ya vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa pili ni suala la mpango mzima wa nishati na vyanzo vyake. Ukisoma kitabu cha bajeti ya Wizara hii kuna vikolokolo vingi ambavyo vimeandaliwa kwa ajili ya kuwa vyanzo vya umeme. Kwa mtizamo wangu, kama walivyokuwa wametangulia kuzungumza wenzangu, Tanzania ina bahati ya kuwa na vyanzo vingi vya nishati, nashauri ni vema tukafikia mahali kama Taifa tukaamua ni chanzo gani tuingize nguvu zetu zote ili tuweze ku-utilize nguvu hiyo kuweza kupata umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tunaamua kuingia kwenye upande wa umeme unaotokana na makaa ya mawe, basi tuelekeze nguvu na investiment kubwa ielekezwe huko, lakini hii ya kutawanya tawanya nguvu kwenda kwenye vyanzo vingi pamoja na kwamba tunavyo, tunatawanya man power, tunatawanya a concentration ya human resource tuliyonayo katika Wizara hii japo ni chache, kwa hiyo, unakuta Makamishna wanabaki kuzunguka sehemu nyingi na matokeo yake tija inakuwa ni ndogo. Kwa kweli, tufike mahali ambako concentration tunaweza tukaiweka ikawa kubwa kwenye mradi mmoja mkubwa ninajua tunavyo vyanzo ambavyo vinaweza vikatoa umeme wa kutosha kama ni gesi, kama ni makaa ya mawe, kama ni vyanzo vya maji, mimi naamini tuchague badala ya kutawanyatawanya resources na matokeo yake tunabaki tunahangaika na hatupati umeme wa uhakika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa tatu ni ushauri kwa ndugu zangu wa TANESCO. Kama tumefika mahali ambapo makampuni mengi yana-out source services, nafikiri TANESCO nao kidogo wangechukua ushauri huu kwamba sidhani kama ni mahesabu ya kiuchumi, kama inapigwa simu kutoka Katoro kilomita 60 kutoka Bukoba Town labda kuna hitilafu ndogo imetokea kwenye nguzo kwenye transfoma, hata kwenye nyumba ya mtu, unakuta kikosi cha TANESCO kwa sababu hakijui nini tatizo limetokea wanahama mji mzima na mafundi wake wote wanajazana kwenye gari wanakwenda kilometa 60, kumbe unakuta ni fuse ni kitu kidogo tu kimeharibika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kati ya sekta ambayo tuna watu wamebobea na hawana kazi wana makampuni ambayo yanaweza kujikita katika suala la kuingia katika sekta ya kutoa huduma ya kurekebisha hata shughuli ndogo ndogo basi TANESCO iweze kuwa na authorized agents ambao wanaweza kufanya shughuli ndogo ndogo sawa na makampuni yanavyofanya, kwa mfano, Vodacom kwa M-Pesa, unaweza ukatawanya kwa maajenti wakafanya kazi nzuri tu, tajiri anakaa Afrika ya Kusini au huko Ulaya anakula hela tu, ana-outsource hizi services kwa watu wengine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu wa nne na ninaamini utakuwa wa mwisho ni kwamba kama nilivyosema Wizara hii imetengewa fedha za kutosha, lakini inanitia wasiwasi binafsi kwamba unapotoa shilingi 1,56,350,669,000 lakini ukatenga OC kwa maana ya ku-supervise hizi pesa shilingi 66,220,848,000 kwamba hii asilimia sita iende ku-supervise asilimia 98 ya bajeti hapa ni mgogoro. Ni sawa na kutaka kupika kilo 1000 za mchele kwa gunia moja la mkaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa tunatoa fursa ya kuendelea kutendeka mambo tuliyoyakuta Njombe, nina-declare kwamba mimi ni Mjumbe wa Kamati hii bahati nzuri, kwamba mkandarasi yuko kule kwenye Mradi wa REA, anafanya vitu vya ajabu, anafunga matransfoma ambayo ni mabovu yanalipuka kila siku, anafunga transfoma na anawaambia wanakijiji kwamba hawaruhusiwi kufunga mashine ya unga zaidi ya moja, tunamuuliza supervisor wa TANESCO na bosi wake wa Mkoa anaanza kutueleza alikuwa hajaenda wala hajui kinachoendelea, alikwenda siku Kamati imekwenda, ndiyo na yeye mara ya kwanza anakwenda kule kukagua mradi. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo maskini yule bwana hawezi kuzungumza ukweli, lakini kwa mafungu ya OC kama hayapo na hii nazungumzia kwa miradi hata mingine ambayo inatengewa mafungu makubwa ya maendeleo, kama fedha za supervision kwa misingi ya OC kwamba anahitaji mafuta, anahitaji gari, gari inaharibika, inahitaji vipuri hawa wakandarasi wataogelea katika kutufanyia mambo ya ajabu kwa fedha hizi chungu mzima mlizozitenga kwa ajili ya maendeleo, hata kama makandarasi watafanya kazi, hawa supervisors wetu kuna uwezekano wa kuwa vibarua wa makandarasi. Wakati wa kwenda kuwasupervised mkandarasi anaweza akamwambia supervisor wake ambaye anatokana na TANESCO hata Wizara anampitia na anamlipia nauli kwenda kum-supervise ili asaini certificate. Hii biashara ina convince rushwa, mazingira haya yana convince hawa watu ku-collaborate hata kufanya hujuma ya aina yoyote. Kwa hiyo, suala la OC ni vizuri pamoja na kwamba najua kuna watu wameshapewa yellow card wakithubutu kuomba OC watapigwa red card. Naomba suala la OC lipatiwe tafsiri sahihi. Tunakubali kwamba kuna wakati linakuwa misused na ubadhilifu unapitia hapo, lakini katika maana halisi wa ku-supervise projects na kusimamia ipasavyo OC ina umaana wake, tusije tukajikuta tumetenga fungu kubwa lisilokuwa na usimamizi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho nilipata bahati ya kwenda Merereni na sikuishia juu tu peke yake, lakini niliingia chini kabisa kwenye mgodi zaidi ya mita 700 na kitu kushuhudia ili nisisimuliwe.
Waheshimiwa Wabunge, kama ni kuibiwa pale Tanzanite sisi tumefungua milango tuibiwe. Mambo yanayofanyika pale, huyu anayejiita mwekezaji ambaye naamini hakuna kitu ambacho ameshawekeza tangu akabidhiwe huo mgodi ni kwamba tutaendelea kuibiwa na kuibiwa na kuibiwa, na hata hawa wawekezaji wazalendo waliowekwa pale inaonekana wale watu ni watu wa deal tu. Wale ni third part wanategeategea kuchukua mzigo. Mbaya zaidi kama nilivyowaeleza suala la kutokuwa na fedha ya ku- supervise, niliwakuta kule chini wale vijana wa TMAA wanaopaswa kufanya kazi ya auditing ya madini yanayochimbwa kule, naamini ni njaa ya kutopelekewa hela ya kuishi, wale unawaona moja kwa moja wana njaa na wamechoka kuliko kawaida. Sasa unaanza kujiuliza…..
MWENYEKITI: Ahsante sana Mheshimiwa