Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Dr. Josephat Mathias Gwajima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kawe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

MHE. ASKOFU JOSEPHAT M. GWAJIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru wa kunipa nafasi ya kuchangia, kwa sababu muda wetu ni mdogo naomba nikimbie haraka haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nianze na jambo ambalo linanigusa sana, kuna taarifa za utekaji zimeanza tena katika nchi hii ya Tanzania. Nakumbuka wiki mbili zilizopita mtoto wa Muhammad wa Zanzibar Kebo ambaye ni mtoto wa Mzee Muhammad al Jabir alitekwa kule Dar es Salaam na maiti yake ikaja kuokotwa baadaye imekatwa vipande vipande na macho yametobolewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu vizuri kwamba Mwenezi wetu wa Chama cha Mapinduzi, Ndugu Paul Makonda anazuguka nchi nzima kwenye ziara ya kujenga Chama cha Mapinduzi. Nimefuatilia kila mahali anapofika wananchi wanampa taarifa za kupotea kwa watu, watu kutokuonekana, watu kutekwa na watu kutokupatikana, Kiongozi huyu anapokea sana malalamiko ya watu hao. Nataka kuuliza Serikali Mheshimiwa Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan amefanya kazi nzuri sana. Namuomba Waziri atolee ufafanuzi jamo hili ili kuondoa sintofahamu ya kuichafua Serikali yetu njema ya Mama Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili kwa sababu ya kukimbiakimbia nazungumza kwa habari ya kupanuka kwa mito na kuleta hasara kwa wananchi. Kupanuka kwa mito kunaleta matatizo kadha wa kadha. Tatizo la kwanza, kupanuka kwa mito kunafanya maji yatoke kwenye mto yaanze kuingia kwenye nyumba za watu. Kupanuka kwa mto kunasababisha barabara zinakatika. Kupanuka kwa mto kunasababisha maji yatoke kwenye mto yaingie kwenye nyumba za watu yalete mafuriko. Kupanuka kwa mto kunasababisha maji yatoke kwenye mto mama yatengeneze mito mingine midogo midogo. Kupanuka kwa mto kunaleta ardhi kumomonyoka na adhi ya Tanzania na ya Dar es Salaam kuendelea kupunga kila siku na kupanuka kwa mto kunaharibu barabara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Jimbo la Kawe nina mitaa 54, karibu kila mtaa una mto uliotokana na kupanuka kwa mto mwingine. Narudia tena, karibu kila mtaa una mto mama na huo mto mama umezaa mito mingine. Kusema kweli hata sielewi watu wa mazingira wako wapi, kwa sababu wangekuwepo ningekuwa nimewaona kwenye hii mito. Hapa mimi sielewi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikupe mfano, Mtaa wa Nyakasangwe una Mto Nyakasangwe na una Mto Nakalekwa. Mto Nyakasangwe nilijaribu kwenda ili niwasaidie wananchi tujaribu kujenga kingo kwa nguvu za Mbunge na wananchi, ulikuwa na upana wa mita 40, baada ya wiki tatu nimekwenda nimekuta una upana wa mita 103. Mto Mpiji kwenye Mtaa wa Kihonzime nilikwenda ulikuwa na upana wa mita 60 nimekwenda mara ya pili una upana wa zaidi ya mita 150, zaidi ya mita 100 zinaongezeka. Hili ni suala la dharura, kama kweli mazingira mpo na mko Serious, hili ni suala la dharura.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mtaa wa Kilimahewa una Mto Wabarikiwe na una Mto Buzwiriri, Mtaa wa Tegeta una Mto Tegeta na mito mingi ambayo siwezi kuitaja. Mto Nyakasangwe, Mto Mpiji, Mto Kidoboya, Mto Nakalekwa, Mto Mbezi, Mto Ndumbwi na Mto Dogodogo Centre. Kila Serikali ya mtaa ina mto na huo mto mama unazaa mito mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, najiuliza sana if we cannot pay attention to these emergences, kama hatuwezi kutoa muda kwa ajili ya hizi dharura za wananchi, watu wamekufa kwenye Jimbo la Kawe kwa ajili ya mito, nami nilitegemea sana kwa mtu mwenye akili na anajua kuzitumia, naruadia tena kwa mtu mwenye akili na anajua kuzitumia. Ukisikia unaambiwa na Mbunge mwenzako kwamba mto uliokuwa na upana wa mita 60 ndani ya wiki tatu zimeongezeka mita nyingine 100, that is a disaster!

Mheshimiwa Mwenyekiti, unazungumza lakini mtu hashtuki, unazungumza unategemea mtu atashtuka, hashtuki. Nyakasangwe kama mto ndani ya wiki tatu mita nyingine zimeongezeka 60 na mito mingine ambayo siwezi kuitaja. Mito hii ni kila mtaa kwenye mitaa 54. Sasa nasikia viongozi wengi wanasema wananchi wamefuata mito, siyo kweli! Kama mto umepanuka mita 100 ina maana umeingia kwenye eneo la wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wanakufa na wananchi wanapoteza maisha kwa sababu ya hii mito. Naomba sana Wizara hii husika m-take responsibility ya kutembelea maeneo haya na kuyaona maeneo haya na kuwafariji wananchi waliopatwa ghasia hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu yangu Kasekenya Naibu Waziri wa Ujenzi alikuja kutembelea barabara zilizoharibika kwa sababu ya mafuriko. Utakuwa shahidi hakuna daraja hata moja ambalo limebomolewa na mafuriko, halipo! Kuanzia daraja la Kunduchi Mtongani halijabomolewa na mafuriko, kilichotokea maji yamekuwa mengi, mto umepanuka unaliacha daraja. Kwa hiyo, daraja linabaki salama barabara inakatwa pande zote kila mahali. Daraja la Mbweni JKT mto umepanuka daraja halijakatwa lakini maji yanapita kushoto na kulia yanakata barabara. Daraja la Mbopo hivyo hivyo, daraja liko imara mto umepanuka kushoto na kulia maji yanakata barabara. Daraja la Tegeta hivyo hivyo mto umepanuka kulia na kushoto unakata barabara. Tulichokuja kufanya tumekuja kurudishia tu mahala ambapo barabara imebomoka bila kutafuta ufumbuzi wa tatizo. Maana yake mvua ikiendelea kunyesha mito ileile tena itakata pale pale tutatumia fedha ile ile. We must not deal with the result of the problem; we must go to the source of the problem. Kama tunataka kuleta ufumbuzi tuache kushughulika na matokeo ya tatizo tushughulike na source ya tatizo lenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niishie hapo lakini niseme ni muhimu sana linapotajwa jambo linalohusu watu kuwa hai au watu kuwa wamekufa, jambo la watu kuwa wamepoteza maisha watoto hawaendi shule kwa sababu ya mito na mvua inaendelea. Nakuomba sana Mheshimiwa Waziri pay attention to this, njoo uje uone hiyo hali, kama mto mmoja ndani ya wiki tatu utanapanuka kwa mita 100 nakuomba sana pay attention to this. Nampongeza sana Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwa kazi thabiti anayofanya ya kuijenga Tanzania na kuwajenga Watanzania, nakushukuru sana. (Makofi)