Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023 na Taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kuchangia kwenye Kamati hizi mbili. Nawapongeza Wenyeviti wote waliowasilisha mezani hoja hizi mbili na ninaunga mkono hoja pamoja na mapendekezo yote ya Kamati.

Mheshimiwa Spika, ninamshukuru Mheshimiwa Rais na ninaipongeza Serikali yake kwa kupeleka fedha nyingi sana kwenye majimbo na kwenye halmashauri mbalimbali; na ukisikia hoja zetu zote hapa ni kwamba fedha zimekwenda nyingi sana lakini tatizo linalozungumzwa hapa na ukiangalia maoni ya CAG kunakuwa na usimamizi hafifu wa fedha zilizopelekwa na Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, hapa tatizo kubwa halipo tena kwenye Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan lakini tatizo lipo kwenye wale waliopewa mamlaka ya usimamizi. Sasa CAG tayari amekwishatuambia na Kamati zetu hizi mbili zimekwishaleta mapendekezo Bungeni.

Mheshimiwa Spika, kwa kifupi sana kinachokosekana ni uadilifu, uaminifu pamoja na uzalendo wa watu wetu ambao wamepewa dhamana ya kuisaidia Serikali katika kuwatumikia wananchi. Jambo hili ni kubwa sana, kama tunataka kwenda sawa sawa ni lazima tujikite kwenye maadili ya watu wetu waliopewa dhamana. Lazima tupime uaminifu na uadilifu wa watu wetu hawa waliopewa dhamana ya kuzitumia hizo fedha kwa ajili ya miradi ya wananchi.

Mheshimiwa Spika, nitajikita katika hoja moja tu ya CAG ambayo na Kamati yetu tumeweza kuitolea mapendekezo, inayohusu usimamizi hafifu. Usimamizi huu hafifu ndio unapelekea miradi kuwa na variation kubwa, usimamizi hafifu unasababisha majengo yetu yajengwe chini ya viwango, lakini pia usimamizi hafifu unasababisha hasara kubwa sana kwenye nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, halmashauri zilizokuja kuhojiwa, asilimia 100 wameshindwa kufuata miongozo wanayoletewa na Wizara ya TAMISEMI. Mmoja anaweza kufuata mwongozo asilimia 40, mwingine aka-fail kwenye mwongozo wa force account na mwingine anaweza aka-fail kwenye sehemu nyingine kama vile ile asilimia 10 ya wanawake, asilimia 4:4:2. Kwa hiyo, Wakurugenzi na Halmashauri nyingi zime-fail kuweza kufuata miongozo na ndiyo maana tatizo linakuwa ni kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kiukweli hali siyo nzuri sana, ukiangalia miradi yetu ambayo tunaletewa ambayo CAG kaipitia, kila halmashauri inakuja na ongezeko kubwa la zaidi ya kile kilichopangwa na TAMISEMI. Mimi siamini kwamba Wizara ikaleta ile schedule of materials halafu ikatoa nafasi kwa halmashauri na wataalam wa pale kutengeneza BOQ, halafu kukawa na variation kubwa kiasi hicho na variation zenyewe hazina justification. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukiwauliza wahasibu na wakandarasi ambao wametengeneza hizo BOQ kiukweli utaionea huruma Serikali, anakwambia anahitaji shilingi milioni 200 ili aweze kukamilisha mradi ambao umepewa shilingi milioni 470. Ukimwambia tufafanulie hii shilingi milioni 200 inaongezeka wapi anaweze akaishia shilingi milioni 20 au 30. Hizi nyingine zote hana pa kuzipeleka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa maana hiyo tujikite kwenye maoni ya kwamba sasa TAMISEMI waweze kuwashughulikia watendaji wote ambao wamepewa dhamana halafu wanashindwa kutekeleza miongozo ambayo wamepelekewa. Kama ile mifumo ya ufuatiliaji wa miradi itakaa sawasawa, maana yake haya yote yanatokea ilhali pale halmashauri kuna viongozi, wilayani pale kuna viongozi na mkoa una viongozi lakini hali inakuwa kama hivi. Tunao Wakuu wa Wilaya, Mikoa, Ma-DAS na Ma-RAS; kama wote wakitekeleza wajibu wao vizuri kisawasawa tunaweza tukalinusuru Taifa letu na tukaweza kufanya miradi hii ikawa inaenda vizuri kabisa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mimi wala sina shaka na force account, shida hapa ni uadilifu. Nilikuwa najaribu kuangalia miradi ambayo imetengenezwa na force account, lakini pia nikapitia baadhi ya miradi ambayo imetekelezwa na wakandarasi, badi hali ni ile ile, tatizo ni uadilifu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, iko miradi iliyotekelezwa na wakandarasi mwezi ulipita, leo ukienda kuitembelea ile miradi yote imesombwa na maji. Tofauti na kazi zilizofanywa na wazee wetu miaka ya 1970 na 1980; unaweza ukakuta miaka ile miradi yao mpaka leo ina-survive, lakini miradi ya wataalam wetu wa sasa inachukua muda mfupi. Kwa hiyo, tunafikia kupoteza fedha nyingi kwa sababu ya kukosa uadilifu. (Makofi)

Mheshimwa Spika, mimi pamoja na kuunga mkono hoja iliyoko mezani, bado nasisitiza kwamba hao hao waliopo kwa uchache wake, hatuwezi kusubiri Serikali ikaajiri asilimia 100 ndipo miradi ikatekelezwa. Kwa hao hao ambao tunao wakati Serikali inaendelea kushughulika na kutafuta uwezo wa kuajiri basi waliopo waendelee kusisitizwa katika uadilifu wa kusimamia fedha za Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba