Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

Hon. Maulid Saleh Ali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Welezo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

MHE. MAULID SALEH ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kunijalia uhai na afya njema ya kuweza kuchangia bajeti hii ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu kwa kuendeleza vyema vyombo vyetu hivi vya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. (Makofi)

Vilevile nimshukuru Mheshimiwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Stergomena Lawrence Tax, kwa kazi nzuri anayofanya akishirikiana na Katibu Mkuu Dkt. Faraji Mnyepe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika lakini vilevile nimpongeze sana Mkuu wa Majeshi - Jenerali John Mkunda na nimpongeze msaidizi wake, Mnadhimu Mkuu wa Jeshi - Luteni Jenerali Othman. Vilevile niwapongeze Makamanda, Wakuu wa Kamandi wote, maafisa wakubwa na maafisa wadogo wote. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kuchangia na nitachangia mambo mawili; jambo la kwanza, kuhusu upatikanaji wa fedha za maendeleo katika jeshi letu hili.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni ukweli usiopingika jeshi letu linafanya kazi kubwa na nzuri sana ya kulinda mipaka yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhakikisha nchi yetu inakuwa salama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika fedha za maendeleo ya jeshi letu hili lililopo chini ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, kiukweli fedha walizopokea ni kidogo sana...

NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Mbunge masuala ya pesa zote mwisho wa bajeti ya Serikali ni mwezi wa sita na hoja zote za mapato na maingizo ya pesa kwenye Wizara zipo kwenye Kamati ya Bajeti, naomba uchangie maeneo mengine, masuala yote ya pesa zitalipwa na zipo kwenye Kamati ya Bajeti. (Makofi)

MHE. MAULID SALEH ALI: Mheshimiwa Naibu Spika, saw ana nikushukuru.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niombe Serikali ipeleke fedha kwa wakati ili watekeleze majukumu yao kwa muda waliyojiwekea. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini lingine kuna madeni, niiombe Serikali iweke mpango mkakati wa kuyafuatilia madeni haya ili iweze kuyalipa kwa Wizara hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine nilipongeze Shirika la Mzinga kwa uvumbuzi wa bomu hili baridi la kufukuza tembo. Tembo hawa wamekuwa wakiathiri sana uchumi wa maendeleo katika nchi yetu, lakini niipongeze tena Serikali hususani shirika hili kwa ubunifu wao na umahiri wao wa kuweza kuleta teknolojia hii ambayo nchi yetu itanufaika kwa maendeleo zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri Serikali hasa Wizara ya Fedha kuwa na mpango mzuri wa kupeleka fedha kwa wakati ili mashirika yetu haya yaweze kufanya kazi kwa ufanisi zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ninawashukuru sana watendaji wote wa Wizara hii ya Ulinzi na Jeshi la Ulinzi la Kujenga Taifa na nimpongeze sana Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa umahiri wake na umakini wake wa kuweza kuwa nchi yetu ipo salama zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)