Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Anthony Calist Komu

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Moshi Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. ANTHONY C. KOMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa naongea kwa mara ya kwanza katika Bunge hili, nichukue fursa hii kumshukuru Mungu na mimi kuwepo hapa. Zaidi niwashukuru wananchi wa Moshi Vijijini kwa maamuzi waliyofanya ambayo yameweza kunifanya nikawa mwakilishi wao, Mungu aendelee kuwaimarisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kabla sijaenda kwenye mchango niweke record sawasawa. Wakati ule tukiwa tunafanya semina hapa, Mwanasheria Mkuu wa Serikali alisema wakati akijaribu kutuaminisha kwamba yeye ni Mwanasheria wa kila kitu. Mwanasheria Mkuu wa Mihimili yote, alisema yuko mtu mmoja alilishtaki Bunge katika Mahakama ya haki ya Afrika Mashariki na yeye akaenda kulitetea Bunge kule kama Mwanasheria Mkuu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ndiye niliyeishtaki lakini sikulishtaki Bunge. Niliishtaki Serikali ya Jamhuri ya Tanzania na nilimshtaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Kesi yangu ni reference Na. 7 ambayo ni Anthony Calist Komu versus Attorney General of United Republic of Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kesi hiyo nilishinda, Mwanasheria Mkuu amekata rufaa na nina uhakika nitamshinda tena ili wanilipe vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niende kwenye kazi hii ambayo iko mbele yetu. Kama mwenzangu aliyenitangulia alivyosema, kama unataka kukamua ng‟ombe ni lazima umlishe vizuri, vinginevyo utakamua damu. Ukienda kwenye haya Mapendekezo ya Mpango, idadi ya watu na pato la kila mtu. Mapendekezo haya yanasema, nchi hii itakwenda kwenye kipato cha kati, na itakwenda kwenye kipato cha kati kwa sababu hapa wamefanya makadirio. Wanasema kipato cha Mtanzania kinakua na sasa hivi kimefikia dola za Kimarekani 1,043, maana yake Shilingi 1,724,716 kwa mwaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukifanya hesabu utaona kwamba kila Mtanzania anapaswa awe anapata kipato cha Shilingi 1,043,000 na pesa kidogo. Sasa nauliza, hivi kweli ni Watanzania wangapi wana kipato hicho siku ya leo? Kima cha chini cha mshahara kwenye viwanda vyetu, viwanda vya Wahindi, Wachina ni Sh. 100,000 na hilo huwezi kulichukua kama ni pato ambalo mtu anakwenda nalo nyumbani kwa sababu bado hujatoa gharama za kumuwezesha yeye kwenda kutekeleza wajibu huo unaompa kwa Sh. 100,000. Maana yake ni lazima alipe nauli, ale mchana halafu ndipo sasa apate kitu fulani. Ma-house girls mmewahi kusema chapa Bungeni kwamba wanapaswa kulipwa Shilingi 80,000 kwa mwezi. Ma-bar maid ambao ni wengi sana katika nchi hii. Sasa hizi takwimu zinatu-mislead na hapa ndiko tunakokwenda kukamua ng‟ombe ambaye hatumlishi vizuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ukienda kwenye viwanda vingi, ukienda kwenye mashamba, sisi tuna mashamba yale ambayo yalikuwa nationalized kule Moshi vijijini, watu hawaajiriwi, watu wanakuwa vibarua kwa miaka mitatu, minne, mitano. Akifika ule muda wa kuambiwa aajiriwe anapewa likizo isiyokuwa na malipo au anakuwa terminated halafu anaomba tena akianza anaanza upya tena. Sasa kwa utaratibu huo ni lazima tuangalie sana mipango yetu na hizi takwimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, madeni. Niko hapo hapo kwa Mtanzania. Tukitaka kwenye uchumi huu wa kipato cha kati ni lazima tuwe na sekta binafsi ambayo ina nguvu. Leo haya madeni yanayozungumzwa na bahati mbaya yanayowahusu watu wa ndani, sekta binafsi ambayo ilikuwa inaongozwa na Mheshimiwa sana Rais Magufuli, Rais wetu wa Awamu ya Tano; Wakandarasi wanadai madeni makubwa sana. Sasa, ukiangalia katika Mpango huu wote hakuna mahali ambapo inaonesha kwamba Serikali imejipanga kulipa haya madeni hasa ya watu wa ndani (Wazawa). Sasa hii sekta binafsi ambayo ndiyo yenye mchango mkubwa sana katika huu Mpango, kwa sababu ukisoma huu Mpango utaona kwamba mapato ambayo ni ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeona katika ule mwelekeo uliyoletwa hapa au hata ukifanya mapitio ya Mpango wa Kwanza wa Miaka Mitano, utaona kwamba ni wastani wa trilioni 8.9 ndizo ambazo zinapaswa kutumika kila mwaka. Lakini katika hizo trilioni 8.9, 2.9 ndizo ambazo ni mapato yetu ambayo naweza kusema Serikali ina uwezo nayo. Trilioni sita zinapaswa kutoka kwenye Sekta binafsi na washirika wa maendeleo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hakuna mkakati wa makusudi, wa kuhakikisha sekta binafsi inalindwa, inalipwa ili kutoa huduma na inalipwa kwa wakati, hatuoni kama tunaanza kuzika huu mpango kabla haujaanza. Kwa hiyo, naishauri sana Serikali iliangalie hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ukienda kwenye Sekta ya Elimu utaona kwamba kuna mambo mazuri yanayozungumzwa, tuna madarasa fulani tunajenga, tuna hiki tunajenga, lakini siamini kama kuna review ya yale ambayo yalikwishafanyika, kwa sababu kungekuwepo na review, toka nimekuwa Mbunge nimetembea karibu Kata zote za Jimbo langu, hakuna Kata hata moja ambayo nimekwenda nikaacha kukuta kuna madarasa ambayo hayafai, yameshakuwa condemned, hakuna vyoo, unakuta shule ina watoto 370 haina choo. Shule ina watoto 188 haina choo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iwe inafanya na kile kitengo cha ukaguzi kwenye mashule wapo tu, hawana fedha, hawafanyi ukaguzi. Kwa hiyo hakuna ripoti za hali halisi ilivyo kwenye field. Hivyo hivyo kwenye sekta ya maji, hapa wanasema maji ni asilimia kadhaa, lakini ukienda kwenye reality, unakuta kwamba hakuna hayo wanayoyazungumza. Kule kwangu wanasema Kata ya Uru Kusini ina maji, Kata ya Uru Kaskazini ina maji.(Makofi)