Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

Hon. Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, naomba kuunga mkono hoja ya Wizara ya Kilimo, kwanza kwa kumpongeza Waziri Mheshimiwa Bashe na Naibu Waziri pamoja na timu nzima kwa kazi nzuri na ubunifu katika kufanya majukumu yao.

Mheshimiwa Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi nzuri ya kuharakisha maendeleo katika sekta zote, sisi Wanamtwara tuna mambo mengi sana ametufanyia, tunamshukuru sana kipekee kwa Sekta ya Kilimo naomba kutaja machache: -

(a) Upanuzi wa Bandari ya Mtwara ili kuwezesha korosho kusafirishwa;

(b) Upatikanaji wa pembejeo za kilimo kwa wakulima wote na hasa viatilifu vya korosho (sulphur); na

(c) Kupanda kwa bei ya mazao hasa ufuta na mbaazi. Kwa msimu uliopita mbaazi imeuzwa 4,000 kwa kilo jambo ambalo halijawahi kutokea tangu tupate uhuru, wananchi wa Mtwara walifurahi na kuishukuru sana Serikali ya Awamu ya Sita.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia changamoto zifuatazo:-

(1) Upatikanaji wa viatilifu usimamiwe na Bodi ya Korosho;

(2) Wizara itafute masoko nje ya nchi hasa Vietnam kwa ajili ya korosho badala ya wanunuzi kutumia mawakala;

(3) Wizara isimamie kwa karibu sana mfumo mpya wa ununuzi wa korosho ambao Tume imependekeza yaani TMX badala ya boksi;

(4) Tozo nyingi za korosho zinapunguza bei kwa mkulima hivyo zipunguzwe hasa tozo ya TARI shilingi 25 na Bodi shilingi 25 zote kwa sasa zifutwe;

(5) Export levy 100% ipelekwe Wizara ya Kilimo kwa ajili ya kuendeleza zao la korosho; na

(6) Mradi wa kongani ya korosho Maranje iendelee.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja, naomba mapendekezo ya Tume Maalum yafanyiwe kazi yote ili kuboresha uzalishaji wa zao la korosho.