Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Othman Omar Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Gando

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. OTHMAN OMAR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakwenda moja kwa moja kuhusu mafuta na gesi. Hapa naanza na TPDC, Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania. Kwa makala chungu nzima nilizosoma nimegundua kwamba TPDC siyo shirika la Muungano, lakini shirika hili lilipewa kazi ya kushughulikia sekta ya mafuta Tanzania nzima. TPDC katika miaka ya karibuni lilikuwa likitoa vibali na kuingia mikataba na mashirika tofauti ya Kimataifa, moja kati ya mashirika hayo lilikuwa Shirika la Shell la Uholanzi. Shirika la Shell lilifanya utafiti wa mafuta katika vitalu vilivyoko Zanzibar, ikiwepo kitalu namba Tisa, namba 10, namba 11 na namba 12, vitalu hivi vyote vinaonekana katika maeneo ya Zanzibar. Namuuliza Waziri mwenye dhamana, TPDC ilikuwa na uhalali kiasi gani kuingia katika maeneo ya Zanzibar na kutafuta mafuta bila ya idhini ya watu wa Zanzibar! (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kitendo cha TPDC kuingia katika maeneo ya Zanzibar na kutafuta mafuta ni sawasawa na kuwadharau watu wa Zanzibar. Tunaomba tu wenzetu waache kijicho juu ya Zanzibar kwa sababu Wazanzibari kuna rasilimali nyingi sana Tanzania Bara wao hawana habari nazo, wametosheka na umaskini wao. Tanzania Bara kuna madini ya aina chungu nzima, Tanzania Bara kuna gesi, lakini hujamsikia Mzanzibari hata mmoja kudadisi masuala ya madini, masuala ya gesi yaliyoko bara. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na Sheria ya Mafuta iliyoundwa mwaka jana (The Petroleum Act 2015), Sheria Na. 2 ambayo imezipa nafasi pande hizi mbili kushughulikia mafuta kila mmoja upande wake, lakini kutokana na hali ya Zanzibar ilivyo, Serikali dhalimu iliyopo, sisi hatuna imani kwamba wanaweza wakawatendea haki Wazanzibari wakaweza kudhibiti mafuta yale bila ya kuyatorosha kuyapeleka Tanzania Bara. Kwa sababu Serikali iliyopo kule ni dhalimu, ni Serikali imewekwa na Tanzania Bara na wanaketi kama ni mawakala wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sisi siyo Serikali ya Wazanzibari, kwa hiyo hawana uwezo, jambo lolote lile mtakalowaambia, wakiambiwa wa-pump mafuta walete Tanzania Bara wataleta, hawana uwezo wa kuyazuia mafuta. Kwa maana hiyo, hatutegemei kwamba kwa wakati huu inaweza ikaja kampuni kuchimba mafuta kule kwa muda huu. Mafuta yale yaliyoko Zanzibar, na yapo, yatakaa vilevile mpaka pale ambapo watu wa Zanzibar watakuwa na Serikali yao wenyewe waliyoichagua. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nichangie katika maeneo ya madini. Wachangiaji wengi sana hapa wamezungumzia kuhusu madini. Moja katika madini ambayo yameonekana Tanzania hii ni madini ya uranium. Pamoja na umuhimu wa madini haya ambao ni pamoja na kuzalisha umeme, kama wanavyofanya wenzetu Afrika Kusini kule, pamoja na kutengeneza silaha za nyuklia, madini haya yanatoa mionzi hatari ambayo ni hatari kwa maisha ya watu. Kuna maeneo mengi ambayo madini haya yameonekana, kama maeneo ya Bahi yaliyopo Dodoma hapa.