Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Aaah tumekuwa watatu sasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuipongeza Wizara ya Nishari na Madini kwamba sisi wengi Wabunge tuliorudi safari hii ni heshima yako Mheshimiwa Profesa. Nasema hivyo kwa sababu sehemu zote ulizoweka umeme ndiyo watu wamepata neno la kuongea na leo hii Wabunge tumeingia hapa. Tunamshukuru sana yeye pamoja na taasisi zako zote na tunaomba waendelee na moyo huo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nianze kwa neno dogo. Katika utaratibu wa umeme kuna sehemu vimejitokeza vitu ambavyo vinatakiwa vifanyiwe kazi haraka sana na Serikali ya Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Katika mita zetu za LUKU Watanzania wengi wamekuwa wanakatwa ikifika mwisho wa mwezi. Kama ni kukatwa pesa ni afadhali mtu awe anataarifiwa kwamba katika kuwekewa LUKU yako LUKU hiyo imekutwa na matatizo, huko nyuma ulikuwa una deni na kama ni deni tujue kwamba, ilikuwa ni kiasi gani.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Lakini kumekuwa na taratibu ndani ya TANESCO mtu anatarajia katika simu yake ana shilingi 20,000; anaweka LUKU lakini ikifika pale anaambiwa pesa yako haitoshi, wakati hana pesa nyingine na anahitaji msaada wa umeme. Unaweka shilingi 30,000 unaambiwa pesa yako haitoshi. Sasa kama haitoshi kwanini vitu hivi mtu asikuambie mapema kwamba, unawekewa LUKU lakini siku za nyuma ulikuwa una deni kiasi fulani unatakiwa ulipe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mnawangoja walala hoi inafika siku ya mwisho wa mwezi mtu analipia LUKU yake kwa misingi kwamba nyumba yake ipate umeme, unakatwa pesa yako. Mheshimiwa Waziri naomba sana kama utaratibu huu huufahamu tunataka tukuambie kuna tatizo hili kwa Watanzania wa chini ambao hawajui kwamba maisha yao ya baadaye yanakuaje wanakatwa pesa zao hovyo hovyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, watu wanaowekewa REA waliambiwa kwamba wanawekewa umeme kwa shilingi 27,000. Na Watanzania wengi walipata nguvu kubwa sana kwamba sasa tunawekewa umeme kwa shilingi 27,000. Lakini kunatokea mabadilika, mtu anakwenda kutafuta pesa hata kwa kukopa kwa mtu, anaweka line katika nyumba yake, siku anayotarajia anaambiwa kwamba leo REA imekiuka sio hii tena shilingi 27,000 inapanda bei kiasi ambacho Mtanzania wa chini anashindwa wakati nyumba yake tayari imekuwa na LUKU tayari ameshaifanyia kila kitu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuomba Mheshimiwa Waziri, kama umeme wa REA ameufanyia jitihada kubwa sana kwa Watanzania, wameupata, lakini sasa inafika mahali wanabadilishiwa viwango vya kuweka umeme, hatuwatendei haki kwa sababu umeme huu umeletwa na Watanzania na hii pesa ya Watanzania na ni kodi ya Watanzania. Kama kweli tunataka kuwasaidia Watanzania basi wawekewe kiwango kile kile kiwasaidie Watanzania wa chini na wao wawe na umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunakuja umeme. TANESCO wanafanya kazi nzuri sana usiyemkuta mtu anayemshukuru mtu wa TANESCO au watu wote wa TANESCO basi mwangalie huyu mtu ana mapungufu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ila nataka niwashauri kitu kimoja Serikali yangu ya Chama cha Mapinduzi. Umeme tunao utumia sasa hivi ni wa gharama kubwa sana kwa sababu unatumia mafuta na vitu vingine, na wengine mnakodi mitambo. Lakini kuna vituo vya nguvu vya umeme ambavyo vinatumia maji. Vituo hivi ndivyo vinavyofanya leo Uganda wanakuwa na umeme ambao haukatiki mara kwa mara, na umeme huo wa Uganda umefika mpaka Tanzania kwa kutumia maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini eneo la Hale, Kihansi, Bwawa la Nyumba ya Mungu na Bwawa la Mtera tusiyaendeleze kwa kuweka mitambo ya kisasa badala ya kutegemea hawa watu wanaotoka nje ya nchi kuja kutuibia Watanzania? Wanatuongezea bills zisizokuwa na maana, matokeo yake wanataka watupeleke mahakamani? Hawa watu walikuja kwetu kuchuma au walikuja kuwasaidia Watanzania? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kama kuna uwezekano, haya meneo ambayo tuliyaanzisha sisi; Watanzania walikuwa wanategea sana umeme wa nguvu za maji leo Zimbabwe na Zambia wanategemea nguvu ya maji tu. Na hii nguvu ya maji inasaidia haina gharama kubwa kama hizo wanazotupa hawa wenzetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba sana Mheshimiwa Waziri, yeye ni msikivu sana, tena ni Profesa mwenzangu naomba aliangalie suala hili ambalo mimi bila yeye nisingerudi pale jimbo la Korogwe Vijijini. Alifanya kazi ya ziada kulisambazia umeme, lakini pamoja na umeme ule ambao ameusambaza namshukuru na uendelee na jitihada zake. Lakini swali ambalo ninajiuliza, kuna baadhi ya maeneo ambayo hayana umeme.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jimbo la Korogwe katika Mkoa wa Tanga, Jimbo la Korogwe Vijijini ndiko kwenye nguvu za umeme aina mbili, iko Hale, iko Chemka. Lakini nguzo nyingi za umeme zimepita kwenye nyumba za watu zimekwenda kwenye mashamba ya mkonge ambayo leo hii hayaendelezwi.
Sasa badala ya kuchukua nguzo nyingi kupeleka kwenye maeneo, na kuna vijiji ambavyo vimepitiwa na maeneo yale, kwa nini wasipeleke nguzo moja badala ya kupeleka nguzo 50?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini tusitumie vielelezo hivi? Kwa mfano nina kata pale toka Uhuru umeme wanausikia kwenye redio, kata ya Kizara, kata Vugiri katika vijiji vya Mlalo, kata ya Mpale katika kijiji cha Mpale na Mali hakuna kitu cha aina yoyote. Kata ya Mkalamo, Mswaha hakuna umeme, sasa na ndio umeme umetokea huko kwangu. Mheshimiwa Waziri, naomba ulivyonisaidia wakati nikiumwa, nikiwa India ukanipelekea na watu wako wa REA wamefanya kazi nzuri sana hebu nimalizie hili na mimi nijijue kwamba mwaka 2020 basi tunakuwa watu wa kupeta tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la madini. Madini ni kitu muhimu sana kwa Tanzania. Mimi kwenye jimbo langu kuna sehemu kubwa tu za kutoa madini, lakini watu wa madini hawapati faida yoyote ya madini yale. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, miaka ya nyuma Serikali iliahidi kwamba itakwenda kule kuwapelekea wachimbaji wadogo wadogo, watakwenda kuwafungulia SACCOS zao za kupata pesa kwa ajili ya wao kuendeleza miradi yao ya madini, lakini cha kushangaza mpaka leo hii katika Jimbo langu kule Kalalani hakuna hata mtu mmoja ambaye amesaidiwa. Sasa hawa wachimbaji wadogo wadogo kwanini hatuwathamini wakati wao ndio wanaoonesha njia kwamba, hapa ndiko kwenye madini na ndipo wanapoonesha njia na Serikali inakuja kuchimba inapata faida kubwa, wawekezaji wanakuja; lakini sio kwa Serikali peke yake bila kushirikiana na hawa wachimbaji wadogo wadogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri ni msikivu na Wizara yake ni sikivu. Mimi nimeiita kwenye Kamati yangu, tumeona matatizo yake na mmejaribu kuyarekebisha. Katibu wako Mkuu, anafanya kazi vizuri, Katibu Mkuu wa REA anafanya kazi vizuri. Naomba sana hii shughuli hebu imalizie kwa sababu wengine hatuwezi kusimama hapa kila siku kupinga wakati Serikali imefanya. Si mimi tu hata upinzani kuna majimbo mengi yamepewa umeme na kama yamepewa umeme ni kwa ajili yako na ndio maana wengine hapa leo hata kusema yale maneno makubwa makubwa hatuwezi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja asilimia mia, Mungu akubariki sana.