Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Dr. Joseph Kizito Mhagama

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Madaba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. KIZITO M. JOSEPH: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia muda niliopewa niende moja kwa moja, kwanza kutoa salamu za shukurani kwa Waziri, Mheshimiwa Profesa Sospeter Muhongo, ambaye majira ya jioni kuelekea saa moja, mvua zinanyesha, amechoka, amefanya kazi kutwa nzima Ludewa, anarudi anakwenda Songea Mjini, alikubali kuendesha mkutano Madaba. Wananchi wa Jimbo la Madaba hawataisahau ile taswira.
Mheshimiwa Naibu Spika, siku ile Mheshimiwa Profesa Sospeter Muhongo, alitoa majibu ya moja kwa moja ya tatizo kubwa la umeme la wananchi wa Madaba. Wananchi wa Madaba wanamshukuru na wapo pamoja naye katika safari hii ya kutekeleza majukumu aliyopewa na Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kuna changamoto katika utekelezaji wa maagizo ya Mheshimiwa Waziri, lakini changamoto hizi zinahusisha zaidi muundo wa utaratibu huo wa utekelezaji. Kwa utaratibu ambao Mheshimiwa Muhongo ameuweka, ni kwamba Madaba ifikapo Desemba tutapata umeme, lakini katika kipindi hiki cha miaka miwili Madaba Mjini patakuwa hub ya umeme unaotoka Makambako kuelekea Songea, lakini pia hub ya umeme unaotoka Mchuchuma na Liganga kulelekea maeneo mengine ya Taifa letu. Maana yake nini? Maana yake Madaba inakwenda kupitia transformation kubwa sana ya uchumi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto inayotupata kwa sasa ni kwamba Serikali bado ina ugumu kidogo wa kuchangia gharama kuweza ku-meet gharama za wafadhili kwenye hilo jukumu na kikwazo kinaonekana kipo Hazina. Naomba watu wa Hazina wasikalie pesa kama zipo. Kama pesa zipo na zimepangwa kwa matumizi hayo, basi zitolewe zikafanye hizo kazi ili hizi Wizara husika ziweze kujibu matatizo ya wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita kwenye hili tu kwa sababu linanigusa na wananchi wa Madaba lina wagusa sana. Ndani ya Jimbo langu la Madaba ni kijiji kimoja tu cha Lilondo kina umeme na umeme huu ni wa wananchi. Nachukua nafasi hii kumshukuru sana Mheshimiwa Jenista Mhagama na Mheshimiwa Mwijage, ambao kwa namna moja au nyingine wamesaidia sana kupatikana ule umeme. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo yote ya Jimbo la Madaba, Vituo vyote vya Afya, saa hizi mimi Mbunge kwa kutegemea posho ninazopata hapa Bungeni, naweka solar. Hata ukiiangalia gari ninayoitembelea ni ya kawaida sana ili niweze kubana matumizi ya kupata solar kwa ajili ya Vituo vyote vya Afya. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana na wananchi wa Jimbo la Madaba wanaomba sana kwa Mheshimiwa Waziri Profesa Sospeter Muhongo, kwamba yale ambayo ameyapanga wanamwomba Mwenyezi Mungu amjalie nguvu ili ifikapo Desemba na kuendelea changamoto hii iwe imekwisha. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tunayo miradi ya kielelezo ya kiuchumi. Ndugu yangu…
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante na naunga mkono hoja.