Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nashukuru sana kwa kupata nafasi hii niweze kuchangia katika Wizara hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo langu liko mpakani kabisa mwa Zambia na Tanzania. Ni Jimbo ambalo ni lango kuu la nchi za Kusini na kati mwa Afrika. Jimbo la Tunduma linakuwa na wageni wengi sana ambao wanatoka nchi mbalimbali; South Africa, Botswana, Zimbabwe, Congo, Malawi na Zambia. Cha kushangaza katika Serikali yetu hii huwezi kuamini, Mji wa Tunduma hauna umeme wa kutosha kabisa. Wageni wengi katika Mji wa Tunduma sasa hivi wanakwenda kulala Zambia kwa sababu ya kuhofia usalama wao kutokana na giza kubwa linalokuwepo katika Mji wa Tunduma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nimshauri tu Mheshimiwa Waziri wakati anakuja hapa atuambie, ni lini Tunduma tutapata umeme wa kutosha ambao utasaidia kuwavutia wawekezaji na watu wanaotumia Bandari ya Dar es Salaam ili waweze kutumia gesti zilizoko Tunduma na kuweza kukaa katika nyumba ambazo tumezijenga katika Mji wetu wa Tunduma kuliko kuwa na giza katika mpaka wetu?
Mheshimiwa Naibu Spika, ni aibu kubwa sana kwa nchi kama Tanzania ambayo sasa mpaka wa Tunduma ni mkubwa unaoingiza fedha nyingi. Miezi sita tu ulikuwa umeingiza karibuni shilingi bilioni 22 kwenye mpaka wetu wa Tunduma. Huwezi kuamini, hata maji Tunduma pale, imefika mahali mashine zetu za kuvutia maji kila siku zinakufa kwa sababu ya umeme kuwa mdogo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunataka Mheshimiwa Waziri atuambie leo, kwamba ni lini atahakikisha umeme wa pale utakuwa vizuri? Kama wameshindwa kuleta umeme Tunduma, tuna transforma pale upande wa Zambia, miaka ya nyuma tulikuwa tunatumia umeme wa Zambia. Tunaomba watuunganishe na umeme wa Zambia ili wananchi wetu wa Mji wa Tunduma waweze kuwa na umeme masaa 24. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kuna mitaa mingi sana kwenye Mji wangu wa Tunduma haina umeme. Mitaa hiyo ni Namole, Msambatuu, Chiwezi na Mtaa wa Niumba, hawana umeme kabisa. Tunavyozungumzia mitaa, ina maana ni maeneo ambayo yako mjini, lakini huwezi kuamini, hakuna umeme kabisa. Wananchi wanalima vizuri, wanazalisha, lakini wanashindwa kupata huduma muhimu za umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri, atuambie, ni lini atahakikisha kwamba wananchi hawa, maeneo ambayo nimeyataja wanahakikisha kwamba wanapata umeme kwa kipindi hiki ambacho tunacho.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia imekuwa ni tatizo kubwa sana katika nchi yetu, kwamba katika Wilaya zetu ambamo wamepelekwa Mameneja wa Wilaya, wamekuwa wanalalamikiwa sana na wananchi katika maeneo yale, kuna mambo ya msingi sana ambayo ilitakiwa Wizara ifanye, lakini imefika mahali wanashindwa kufanya kwa sababu fedha ambazo zinakuwa zimepangwa kwenye bajeti kwa ajili ya kuweka umeme, unakuta fedha zile hazifiki.
Mheshimiwa Naibu Spika, tunaomba sana, tunapotengeneza bajeti hapa Bungeni na tunapitisha, tunaomba hizi fedha ziende katika maeneo hayo ili zikawatumikie wananchi, waweze kupata huduma ya umeme. Kitendo cha kutengeneza bajeti hapa halafu baadaye bajeti zile zinashindwa kuwafikia wananchi kama tulivyokuwa tumepanga, ni kurudisha maendeleo nyuma. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tukubaliane kabisa, hakuna nchi yoyote inaweza kupiga hatua kama nguvu ya umeme katika nchi hii itakuwa chini kiasi hiki. Wananchi wengi sana wamejiajiri, hasa vijana, wamejiajiri, wanachomelea, wana viwanda vidogo vidogo, lakini vile viwanda sasa hivi vimeanza kufa na wameshindwa kufanya kazi hizo kwa sababu ya kukosa umeme katika nchi hii. Tunaomba nchi hii iachane na mazoea ya kutoa ahadi ambazo hazitekelezeki; wawe na muda mzuri wa kutekeleza na kufanya mambo ambayo yanaweza yakawasaidia wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi Tunduma nimeshamwambia Waziri wa Uchukuzi, Waziri wa Maji na sasa namwambia Waziri Profesa Muhongo, wahakikishe kwamba wanaleta umeme na huduma zote za kijamii kwenye Mji wa Tunduma kwa Wizara zote, zinapatikana pale kwa sababu sisi ndio tunaolinda Bandari ya Dar es Salaam. Bandari ya Dar es Salaam asilimia 60 ya mzigo unapitia kwenye mpaka wa Tunduma. Kwa hiyo, tuna….
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. Ahsante sana.