Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi. Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kumshukuru Mwenyezi Mungu na kuwashukuru wanawake wa Mkoa wa Rukwa kwa kuniwezesha kuwawakilisha Bungeni, Mwenyezi Mungu awabariki. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa John Pombe Magufuli kwa ushindi mkubwa alioupata na kuanza kazi mara moja ya utekelezaji wa ilani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze pia Waziri wa Fedha kwa kuwasilisha Mpango wa Maendeleo wa Taifa utakaokuwa dira ya utekelezaji. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze sasa kuchangia na kuishauri Serikali sikivu ya Chama cha Mapinduzi kwamba, mpango huu ungetoa kipaumbele cha kwanza cha maji safi na salama hivyo kutokana na shida kubwa wanayoipata wanawake wa Mkoa wa Rukwa kufuatia maji kwa mwendo mrefu wakati huo shughuli za kilimo zinawasubiri, kulea watoto kunawasubiria, hata akinababa wanawasubiri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, wanawake wa Mkoa wa Rukwa wanapata shida sana ya maji, imepelekea kwamba na wananachi wengine wameamua kuchimba visima vya kienyeji ambavyo vimepelekea kuleta matatizo ya watoto kutumbukia kwenye visima hivyo na vijana wengine wawili kufariki kwa sababu ya kutumbukia kwenye hivyo visima.
Mheshimiwa Injinia Stella Manyanya yupo hapa ni shahidi, naishukuru kwanza Serikali ya Chama cha Mapinduzi ilileta mradi wa bilioni 30, lakini huo mradi hakuna maji mpaka sasa hivi. Naomba niishauri Serikali ya Chama cha Mapinduzi huo mradi uishe mara moja ili tatizo la maji liweze kuisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niingie kwenye suala la kilimo, ili kwenda kuwa Tanzania ya viwanda lazima wakulima waangalie sana katika kuwapatia zana za kilimo na pembejeo. Suala la pembejeo ni muhimu sana kwa sababu wakulima wanapata pembejeo na mbolea kwa kuchelewa. Ili tuweze kwenda na wakati kwa Tanzania ya Viwanda lazima wakulima wapate pembejeo kwa wakati na mbolea. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye suala la uwezeshaji, kama ilani ya Chama cha Mapinduzi inavyoeleza kwamba itawawezesha wanawake na vijana kwa kutoa milioni hamsini kwa kila kijiji, Mpango huu ni mzuri naomba sasa Serikali itekeleze.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha. (Makofi)