Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Amb. Adadi Mohamed Rajabu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muheza

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. BALOZI ADADI M. RAJAB: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuunga mkono hoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Waziri kwa juhudi zake za kuhakikisha zabuni ya bomba la mafuta kutoka Ziwa Albert- Uganda hadi Bandari ya Tanga inafanikiwa. Namwomba aangalie uwezekano wa kusaidia vyombo mbalimbali bandari Tanga kwa sababu ni chakavu ili tupate vyombo vya kisasa zaidi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nampongeza Waziri kwa mradi wa REA. Mradi huu ni moja ya sababu zilizotufanya tuingie Bungeni. Binafsi nina eneo la Jimbo kubwa kuliko Majimbo yote hapa Bungeni. Nina kata 37 na vijiji 135. Vijiji ambavyo nimefanikiwa kupata umeme ni asilimia ndogo sana ambayo haizidi asilimia 50. Namwomba sana Mheshimiwa Waziri REA III nipate mgao mkubwa. Nimetuma orodha ya vijiji 100 kwa kuanzia. Aidha, naomba anitatulie tatizo la transformer Mjini Muheza, kila siku umeme unakatika sababu ni uchakavu na ni dogo, limeelemewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, mkandarasi Sengerema apunguziwe kazi. Kasi anayokwenda nayo kwenye mradi wa REA hairidhishi, anafanya taratibu sana. Aidha, utaratibu wa kuwekewa umeme usiruke kijiji kupunguza malalamiko ya vijiji vinavyorukwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la madini, ni kwa nini Serikali isianze mipango maalum ya kujenga kiwanda kikubwa cha kuanza kusafisha madini yetu hapahapa nchini. Mipango hii imekwishaanza nchi nyingine kama Zimbabwe, Botswana na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ni lazima iangalie uwezekano wa kuweka maeneo maalum ya madini ambapo wawekezaji wakija wanaweza kuonyeshwa moja kwa moja badala ya wawekezaji kuzungushwa. Aidha, wale walioshika maeneo bila ya kuyaendeleza wanyang‟anywe.