Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuwapongeza viongozi wote wa Wizara ya Nishati na Madini kwa:-
(i) Kupunguza urasimu wa wateja na kutembelea wahitaji wa umeme;
(ii) Kusambaza nguzo kwa sehemu kubwa; na
(iii) Kutenga 94% bajeti ya maendeleo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutoa hoja juu ya mradi wa Kinyerezi II. Mradi huu unagusa mitaa 40 lakini hadi sasa ni mitaa nane tu imefanyiwa tathmini na mitatu tu ndiyo wamepewa cheque ambazo hadi sasa hakuna pesa kwa wananchi. Fidia kwa wananchi hawa imechukua zaidi ya miaka mitano (5) sasa na hivyo hata malipo yake hayatakuwa halisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mitaa inapewa pesa za kulinda mabomba ya gesi. Naomba pesa za ulinzi ziangaliwe upya ili kuboresha malipo haya kwa mazingira ya sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, umeme wa Kinyerezi II unapitia Kata za Kivule, Kipunguni, Gongo la Mboto, Majohe na Kinyerezi. Hata hivyo, Jimbo la Ukonga lina ukosefu wa umeme katika Kata za Pugu, Buyuni, Chanika, Msongola na Zingiziwa. Naomba Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini pamoja na kupeleka umeme mijini na vijijini, ni muhimu kipaumbele kiwe kwenye maeneo ya shule, vituo vya polisi, zahanati na visima vya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Ukonga lina changamoto ya kuhudumiwa na sehemu mbili yaani Kituo cha Gongo la Mboto na Kisarawe. Suala hili linasumbua wananchi, naomba uwekwe utaratibu wa kupunguza hiyo kero.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana aangalie kwenye migodi hasa huduma za jamii kwa wanaozunguka mgodi na mrahaba wa 0.3% namna unavyokokotolewa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.