Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Selemani Said Bungara

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SELEMANI S. BUNGARA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri wa Nishati na Madini awali ya yote, napenda kukupongeza kwa kuchaguliwa tena kuwa Waziri wa Nishati na Madini, Wizara nyeti na muhimu katika Tanzania yetu. Mwenyezi Mungu akuzidishie busara na hekima.
Pia napenda kukupongeza kwa katika hotuba yako ukurasa wa 36 mpaka 37 kwa kuturejeshea mradi wa ujenzi wa kiwanda cha mbolea, mradi utakaogharimu Dola za Kimarekani bilioni 1.98 sawa na shilingi za Kitanzania bilioni 411.24. Natoa shukrani kwa Serikali kwa kutupatia mradi huu mkubwa kwa maendeleo ya Kilwa na Tanzania kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na yote hayo, Jimbo la Kilwa Kusini, pamoja na gesi inatoka katika Jimbo la Kilwa Kusini lakini katika mradi wa umeme vijiji REA, kwenye Jimbo la Kilwa Kusini ni Kijiji kimoja tu cha Matanda ndicho kimepata umeme katika mradi wa REA. Mheshimiwa Waziri naomba vijiji vifuatavyo vipate umeme wa REA: Pande, Mtilimita, Namwando, Nakimwera, Nangao Malalani (Kata ya Pande), Rushungi, Kisongo, Ruyaya, Lilimalya Kaskazini na Kusini, Namakongoro (Kata ya Linimalyao), Makangaga, Nakia, Nanjilinji „A‟ na „B‟ (Kata ya Nanjilinji), Likawange, Mirawi, Nainokwe (Kata ya Likawaga) Kilole, Ruatwe, Kisangi, Kimbarambara (Kata ya Kikole).
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa Wilaya ya Kilwa Jimbo la Kilwa Kusini ndilo Jimbo litowalo gesi asili kwa heshima na taadhima lipewe kipaumbele katika mradi wa umeme vijijini. Natanguliza shukrani. Ahsante.