Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Joseph Leonard Haule

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mikumi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. JOSEPH L. HAULE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Moja kwa moja nianze mchango wangu nikiuelekeza kwenye kilio cha muda mrefu cha wananchi wa Kata ya Malolo ambao wapo kwenye Jimbo la Mikumi wakilalamikia fidia yao ya uharibifu mkubwa sana wa mazao na mashamba yao uliosababishwa na kupasuka kwa bomba kubwa la mafuta ya TAZAMA Pipeline.
Mheshimiwa Naibu Spika, tangu mwaka 2011 bomba la TAZAMA lilipasuka na kusababisha hasara kubwa sana siyo tu kwa mazao bali zaidi kwenye afya za wananchi wa Kata hiyo ya Malolo hasa kwenye Vijiji vya Mgogozi, Chabi, Malolo „A‟, Malolo „B‟ na maeneo mengine yaliyozungukwa na bomba hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali na wataalam walikuja kufanya tathmini ya uharibifu uliotokea na walikubaliana na wananchi wa Kata ya Malolo kuwa watalipwa fidia ya sh. 320,000,000/= kwa madhara hayo. Tofauti na walivyokubaliana, wananchi wakaambiwa na Halmashauri ya Kilosa kuwa watalipwa sh. 50,000,000/=. Sasa wananchi wa Malolo wanataka kujua ni lini watalipwa sh. 320,000,000/= zao?
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Kata ya Malolo kwa masikitiko makubwa sana wanaiomba Serikali ya Chama cha Mapinduzi iwape majibu, ni lini itawafuta machozi yao kwa kuwalipa haki yao hii muhimu ya fidia hii ambayo hawajalipwa tangu mwaka 2011?
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, napenda sana kuchangia kuhusu mradi huu wa REA. Inasikitisha sana kuona Jimbo la Mikumi halijaguswa kabisa kwenye mradi wa REA I na REA II na sasa tunaingia kwenye REA III tukiwa na sintofahamu kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Mikumi limebatizwa jina na sasa kuitwa Jimbo la giza kwa sababu ya vijiji vingi sana vya Jimboni Mikumi kukosa umeme. Nilishaandika na kuipeleka barua kwa Mkurugenzi wa REA na kumwelezea hali halisi ya Jimbo langu la Mikumi lakini pia baada ya kuuliza swali la nyongeza kwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini ambaye naye alinijibu kwamba atahakikisha mradi wa REA III vijiji vyangu vya Jimbo la Mikumi vyote vitaingizwa kwenye mradi huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, napenda Mheshimiwa Waziri akija kwenye majumuisho yake atuambie ni lini vijiji vifuatavyo vya kwenye Jimbo langu la Mikumi vitapata umeme?
(1) Kata ya Maloo – Vijiji vya Mgogozi, Malolo A & B, Chabi, Itipi;
(2) Kata ya Vidunda – Vijiji vya Vidunda, Udungu na Chonwe, Itembe;
(3) Kata ya Uleling‟ombe – Vijiji vya Uleling‟ombe, Mlunga, Lengewaha;
(4) Vijiji vya Mhenda – Vijiji vya Mhenda, Kitundueta, Ilakala, Maili 30;
5. Kata ya Masanze – Vijiji vya Munisagara, Chabima, Dodoma Isanga;
6. Kata ya Tindiga – Vijiji vya Malui, Tindiga, Kwalukwambe, Malangali;
7. Kata ya Ulaya – Vijiji vya Nyameni, Mbuyuni, Kibaoni, Ng‟ole, Nyalanda;
8. Kata ya Kilangali – Vijiji vya Mbamba, Kiduhi;
9. Kata ya Mikumi – Vijiji vya Ihombwe, Tambuka Reli, Msimba;
10. Kata ya Zombo – Vijiji vya Kigunga, Madudunizi, Nyali, Zombo; na
11. Kata ya Ruhembe – Kijiji cha Kielezo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.