Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia Wizara hii kwa maeneo yanayohusu Jimbo langu la Bunda Vijijini. Jimbo la Bunda lina Vijiji 39. Matatizo ya umeme ni kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, REA I vijiji vilivyopata umeme ni Kyandege, Migeta, Mariwanda, Salama „A‟ na Hunyuri Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo umeme wa REA Phase I uliwekwa katika maeneo ya center (Barabara kuu). Aidha, maeneo yote ya Taasisi; Mashuleni, Hospitali, Ofisi) hakuna umeme. Aidha, katika Vijiji vya Mariwanda, Hunyari, umeme uliwekwa katika volt ndogo (muhimu). TANESCO Bunda wanajua.
REA II: Vijiji vilivyopata umeme ni Kiloreli, Kambubu, Nyamuswa, Marambeka, Salama Kati, Kurusanga, Mikomariro na Mibingo.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo vijiji vya REA II nilivyovitaja kuanzia cha 1 – 6 umeme umewaka katika maeneo ya center tu. Taasisi zote za Umma hakuna umeme. Wizara imetoa agizo kupitia Mheshimiwa Muhongo (Waziri) kuwa Taasisi zote za Umma zipate umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, REA III; vijiji ambavyo vinahitaji umeme ni Manchimaro, Tingirima, Nyangiranga, Rakana, Tiringati, Bigegu, Nyaburundu, Mahanga, Mmagunga, Nyariswori, Sarakwa, Majengo, Nyangere, Nyabuzame, Mmuruwaro, Nyang‟ombe, Nyanungu, Rubimaha na Bukoba,
Mheshimiwa Naibu Spika, ni matumaini yangu kuwa maeneo yote hayo yatapewa umeme wa REA Phase III kama ilivyoahidiwa na Mheshimiwa Rais wakati wa kampeni.
N.B. Vijiji vya Bukoba na Samata vimewekewa transformer, tunahitaji umeme uwake. Mungu ibariki Wizara, Mungu ibariki Tanzania.