Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali katika Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kwa sababu ni mara yangu ya kwanza, kuchangia, nimshukuru sana Mwenyezi Mungu, ambaye ametupigania mpaka leo tupo hapa. Jambo la pili niwashukuru sana wananchi wa Tarime ambao kwa miaka mingi na miaka yote wameonesha imani kwangu walinichagua, kuwa Diwani wa Kata ya Tarime Mjini nikiwa Mwanafuzi wa Chuo Kikuu, lakini vilevile pamoja na mapambano makali yaliyokuwepo kwenye uchaguzi huu mpaka mauaji yaliyofanyika tarehe kumi mwezi wa Tisa, wananchi walisimama imara na wamenileta hapa na nataka niwahakikishie nitawawakilisha na nitasimamia kero zao kwa nguvu zangu zote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, jana usiku nilijitahidi sana kusoma na ku-google nchi mbalimbali kuhusiana na Uongozi, nikajaribu kuangalia mambo yaliyofanyika siku za hivi karibuni hapa Bungeni, ya Polisi kuingia ndani ya Bunge wakiwa wamevaa Head gear, bunduki, sijui mipini kujaribu kupiga Wabunge waliokuwa hawana silaha. Nikagundua kwamba hata Idd Amini, hata Adolf Hitler, hakuwahi kuingiza Polisi kwenye Bunge kujaribu kupiga watu wanaopinga. Kwa hiyo, hapo mtajaza wenyewe kwamba mna uongozi wa aina gani. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatuwezi kuongoza nchi hii kwa takwimu za uongo. Hapa Dkt. Mpango naomba unisikilize vizuri, nimesoma vitabu vya Mpango hivi, takwimu zilizoko hapa, ni takwimu feki, na kwa takwimu hizi hamuwezi kufanya kitu chochote hata muwe na nia njema. Kwa nini nasema hivyo, kwa mfano, maji vijijini kitabu hiki kinaonesha cha Mpango kwamba kuna maji Vijijini kwa asilimia 68.
MHE. JOHN W. HECHE: Nimejaribu kuangalia kwenye Jimbo langu peke yake…
MWENYEKITI: Taarifa Mheshimiwa Naibu Waziri!....
MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba ulinde muda wangu, naamua kuwapuuza wote niendelee tu. Nilikuwa nazungumzia kuhusu takwimu. Takwimu za maji kwa mfano vijijini wamesema maji yapo kwa aslilimia 68, lakini nimeangalia Jimbo langu ni Jimbo la Vijijini tuna Kata 26, katika Kata 26 hizo asilimia 68 ya 26 ni Kata 17 ina maana kwa mujibu wenu kwenye Kata 17 kuna maji hivi sasa tunavyozungumza, kitu ambacho ni uwongo na hakipo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Mijini mmesema kuna maji asilimia 95, hii ni aibu ina maana kila watu 10 watu tisa wanapata maji, au kila watu 100, watu 95 wanapata maji, lakini pale Dar es Salaam ni kielelezo, kipindupindu kinawaumbua kila siku, kwamba hakuna maji na takwimu mnazoleta humu ni za uongo. Kwa hiyo, kama mnataka kulitoa Taifa hili hapa ni lazima tuwe na takwimu ambazo zinaeleza ukweli, na takwimu ambazo zitawasaidia kujenga kwenda mbele, lakini mkija na takwimu za uongo hapa mnajidanganya wenyewe na wananchi wanawaona.
MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara, zetu ni mbovu
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa!
MWENYEKITI: Taarifa...
MHE. JOHN W. HECHE: Nawashauri Mawaziri tulieni msikilize, kwa mujibu wa sera ya maji ya Taifa hili, maji ambayo mnahesabu kwamba watu wanapata wapate ndani ya mita 400 kutoka wanapokaa, sasa kwenye hivi vijiji mimi ninavyosema watu wanafuata maji mpaka kilometa moja, mbili, sasa unatoa taarifa gani hapa. Tulia usikilize tukueleze wananchi watapima kule anasema nani uongo kama maji yapo au kama hayapo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara, barabara zetu ni mbovu, kwa mfano barabara za Tarime. Kutoka Tarime kwenda Serengeti ambako kuna Mbuga kubwa ya wanyama. Inapita Nyamongo kwenye eneo la Mgodi wa Nyamongo, barabara ni mbovu, na mimi ninamwomba sana Waziri achukue hii hoja ya barabara hii iwemo kwenye Mipango ya Serikali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu nishati; leo mnakuja hapa kuzungumza kuendeleza Taifa, wakati watu wanapikia kuni. Dar es Salaam peke yake, ambayo mkaa unakwenda pale magunia tani na tani, mngeweza kama kweli mnataka kuendeleza Taifa hili, kuliko kurukaruka hapa, mngechukua Dar es Salaam ile peke yake, mkazuia utumiaji wa mkaa na magogo na kila kitu mkapeleka gesi pale kwa bei rahisi watu wote watumie gesi pale Dar es Salaam, Arusha na Mwanza, tayari mngekuwa mmesaidia misitu ya Taifa hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mnakuja humu mnaimba tu misitu tuta-conserve misitu, mazuia watu. Kama kule Jimboni kwangu naona eti Afisa Misitu anazuia watu wasitumie mkaa, nimemwambia wananchi watakuchapa wewe! Wapelekee kwanza gesi ndiyo uwazuie kutumia mkaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Makusanyo ya Serikali; nataka mtuambie hapa, hicho mnachojisifia kwamba mmekusanya mwezi wa 12 ni arrears au ni vyanzo vipya mmeleta na mmekusanya. Kwa sababu msije mkajisifu hapa tumekusanya tirioni 1.4 kumbe ni arrears za huko nyuma ambazo ni za watu ambao ni majipu na majipu wengine wako humu mnawajua wanatakiwa walipe na ni madeni. Sasa huko mbele mmetengeneza vyanzo gani, mmvionesha wapi kwenye Mpango huu, vyanzo vipya. Leo mnataka mchukue pesa kwenye Halmashauri na hili msithubutu Mheshimiwa Waziri, Halmashauri watu wakusanye pesa wao wenyewe, wakupelekee Benki Kuu, halafu wewe ndiyo urudishe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hapa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime, tunaidai Serikali pesa za ardhi ambazo ni asilimia 30 miaka karibia sita zaidi ya milioni 500, tunapeleka pesa zetu wakati wa kurudi hazirudi. Leo ndiyo wamerudisha milioni 27, leo tena tuchukue pesa zetu za mapato ya ndani tuwapelekee na nyie mnajua, kama mnataka kuendeleza uchumi wa watu kule vijijini mabenki yaliyoko kule Wilayani ndiyo yanakopesha watu wanaofanya biashara ndogondogo na benki hizi zinategemea pesa kutoka kwenye Halmashauri, leo mnataka mchukue pesa zitoke Halmashauri mabenki yakose pesa, yashindwe kukopesha watu wetu kule chini, biashara zife kule chini, halafu mnasema mnataka kuendeleza Watanzania au mnataka kuwa-suffocate.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mmekuja hapa mnasema viwanda, kila mtu anasimama hapa viwanda. Viwanda gani, viwanda vinategemea foreign direct investment, Wazungu hawa mnaoenda kukinga mabakuli wamesema wako concerned na mambo yaliyofanyika Zanzibar, hakuna amani, Zanzibar kule kuna Nkurunziza. (Makofi)
Mmechukua hamtaki kutoa nchi kwa mtu aliyeshinda, kwa maana hiyo Wazungu wanakwenda kuzuia hiyo misaada sijui mtapata wapi pesa za kuanzisha hivyo viwanda.
MWENYEKITI: Mheshimiwa muda wako umemalizika naomba ukae.