Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Njalu Daudi Silanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Itilima

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. NJALU D. SILANGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naipongeza Wizara ya Nishati na Madini kwa kazi nzuri wanayoifanya wakiongozwa na Mheshimiwa Profesa Muhongo, Naibu wake, Mheshimiwa Dkt. Medard Kalemani pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini na watalaam wake wote.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Wizara ya Nishati na Madini, katika Jimbo langu la Itilima, Makao Makuu ya Wiliya, REA phase two, haikuweza kuweka umeme katika maeneo ya nyumba za viongozi wa Wilaya ikiwemo nyumba ya Mkurugenzi na nyumba ambayo Viongozi wa Kitaifa hufikia pamoja na kituo cha mafuta kilichojengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naombe Wizara ya Nishati na Madini ione umuhimu kwenye REA phase three iweze kuzambaza umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika maeneo ya Makao Makuu ya Tarafa ipo miradi ya maji ya Serikali iliyowekezwa inahitaji umeme. Mfano Tarafa ya Kinamweli Kijiji cha Nzezei tunao mradi wa maji ambao uko tayari, unafanya kazi kwa kutumia jenereta ambayo inaleta gharama kubwa kwa wananchi pamoja na kituo cha afya cha Zagayu ambacho kinatoa huduma ya afya katika Vijiji 18 pamoja na Wilaya jirani ya Maswa.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Kanadi katika Kijiji cha Migato ni center kubwa ambayo inaweza kuongeza mapato makubwa kwenye nchi yetu pamoja na ajira kwa vijana; inahitaji umeme. Kuna baadhi ya Vijiji ambavyo havina umeme katika Jimbo langu la Itilima kama ifuatavyo:-
Tarafa ya Kinang‟weli, Kijiji cha Nhobola, Sunzara, Kidula, Ngwamnemha, Sawida, Isegwe, Mahembe, Kinang‟weli, Isegwa, Lulung‟ombe, Kabale, Sasago, Mlimani, Kashishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Itilima, Gambasuga, Dasina, Musoma, Ng‟wabagwa, Ng‟wangwita, Ikangalipu, Tagaswa, Nseme, Magazo, Nkololo, Mwalushu, Ng‟wamanhu, Ng‟wagwita, Dasina B, Banamhala, Bugani, Isakang‟wale.
Mheshimiwa Naibu Spika, Tarafa ya Kanadi ambavyo havina umeme ni kama ifuatavyo; Chimwamiti, Shishasi, Ng‟wakatale, Mtobo, Mwabalah, Pijulu, Nkuyu, Ngailo, Migoto, Simiyu, Lali, Madilana, Mhunze, Ngwabulugu, Ngailo, Lali, Nyatugu, Senani Ng‟waogama, Ng‟wangutugu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba hoja yetu niliyosema, Mheshimiwa Waziri aweze kutupatia hitaji hilo muhimu kwenye eneo langu la Jimbo la Itilima.
Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja kwa asilimia mia moja.