Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Naibu Spika, mpango wa usambazaji umeme vijiji unaotekelezwa na REA katika Awamu ya Pili uligusa vijiji vichache sana katika Wilaya ya Karatu. Serikali inatamka kuwa Awamu ya Tatu itaelekezwa katika vijiji vyote vilivyobakia nchini.
Mheshimiwa Naibu Spika, hizi ni habari njema kwa ananchi wote. Nimwombe Mheshimiwa Waziri agawe orodha ya vijiji kwa kila Wilaya ili sisi Wabunge tuweze kufuatilia utekelezaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Karatu inavyo visima virefu 13 vya maji ambavyo vinaendeshwa kwa mashine za Diesel.
Mheshimiwa Naibu Spika, uendeshaji wa visima kutumia Diesel Engine ni gharama kubwa unafanya wanachi kushindwa kuendesha miradi hii. Nimwombe Mheshimiwa Waziri wa Wizara hii apeleke umeme katika miradi hii ya visima vilivyoko Vijiji vya Basodamsh (2), Emaranek (3), Kiviwasu (2), Rhotia Kainan (1), Endabash (1), Gilambo (1), Gendaa (1), Getamoa (1), Kambi Faru (1).
Mheshimiwa Naibu Spika, tukifikisha umeme katika visima hivi pia kwa vijiji ambavyo visima vipo vitanufaika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sekta ya Madini. Serikali imeteua mawakala kukusanya kodi au tozo ya madini ya ujenzi Example mchanga, kokoto, mawe, moram na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo hili limeleta vurugu na mkanganyiko mkubwa. Kwa muda wote wa nyuma madini hayo yamekuwa chini ya Halmashauri za Vijiji kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya. Mfano, huko nyuma tozo zilizokuwepo ni; kijiji sh. 5,000/=, Halmashauri sh. 5,000/= na wapakiaji Sh. 10,000/=.
Mheshimiwa Naibu Spika, wakala huyo aliyeletwa sasa naye anachukua sh. 5, 000/= na Serikali Kuu sh. 3, 000/=. Jambo hili limeongeza gharama ya kupata mchanga. Lori tani saba kutoka Sh. 20, 000/= hadi Sh. 28, 000/=, huyu Wakala anapata sh. 5, 000/= kwa kila tani saba kwa sababu gani? Hivi Halmashauri zetu haziwezi kukusanya mapato?.
Mheshimiwa Naibu Spika, huyu bwana hachangii matengenezo ya barabara, jambo hili halikubaliki kabisa na litaleta mgogoro mkubwa. Tunaomba Waziri amuondoe wakala huyu na ushuru huo ukusanywe na Halmashauri ya Wilaya.