Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo langu lina ofisi ndogo ya TANESCO ambayo inahudumia kutoka Itigi hadi Mitundu, kilometa 70; na REA II umeme unakwenda hadi Mwamagembe, kilometa 63 toka Mitundu. Ofisi hii pia inahudumia toka Mkiwa hadi Itigi kilometa 30. Kwa maana hiyo ukianzia kilometa 30 ongeza 70 ongeza 63; na ukiongeza REA III mtandao unaongezeka. Jimbo langu kwa sasa lina Halmashauri ya Wilaya ya Itigi kwa maana karibuni kutakuwa na Wilaya ya Itigi, hivyo noamba ofisi yenye hadhi ya Wilaya ili kuendana na mtandao mzuri wa Wizara hii ambayo nami naipongeza. Ahsante.