Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GERSON H. LWENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja hii ili Wizara hii itekeleze miradi iliyopanga pamoja na kujibu hoja zangu ambazo naziwasilisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Profesa Muhongo na timu yake yote ya Wizara kwa utendaji uliotukuka kwenye utekelezaji wa REA Phase II. Wilaya ya Wanging‟ombe kuna vijiji vinahitaji transformer tu na LV line ya kilomita moja mpaka mbili ili wananchi wapate huduma ya umeme. Niliwahi kumwandikia Waziri lakini hadi leo hakuna utekelezaji.
Mheshimiwa Naibu Spika, Vijiji hivyo ni Lusisi, Ihanja, Idindilimunyo, Luduga sekondari, Igelehedza, Mpuhilu, Igelango na Ipunda. Majibu niliyopewa toka REA ni kuwa quantities za mkataba wa REA phase II zimekwisha. Sasa swali langu, je, mradi mlioanzisha REA kutoa umeme kupeleka Kijiji cha Itengelo ambacho hakikuwepo kwenye mpango wa REA II zimetoka wapi na kwa nini REA wanaanzisha miradi bila kuhusisha uongozi wa Serikali ya Wilaya pamoja na Bunge?
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba sana Mheshimiwa Waziri atekeleze ombi hili la wananchi wa Wilaya ya Wanging‟ombe.
Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili ambalo nashauri ni kwamba, TANESCO wasipokee mradi huu mpaka wajiridhishe pasipo shaka kuwa umekamilika kufuatana na mkataba. Yapo maeneo mengi kama Imalinyi, Kanani, Ludinga nguzo zimewekwa lakini hakuna waya. Pia yapo maeneo zilifungwa transformer za size 50 ambazo zimekuwa zikiungua mara kabla ya kutumika. Zaidi ya transformer 40 kwa Mkoa wa Njombe zimebadilishwa baada ya kuungua. Specifications ziangaliwe upya kama ndizo sahihi kwani zimekuwa zinaungua hasa wakati wa mvua na radi. Sasa hivi ni kiangazi tatizo hili halipo, lakini mvua zitakaporudi linaweza kujirudia.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Wanging‟ombe ina vijiji 106. Katika mpango wa REA phase II na phase I ni vijiji 42 tu ndivyo vina umeme. Naomba mpango wa REA phase III Serikali ipeleke umeme kwenye vijiji vilivyobaki ambavyo ni takribani vijiji 64.