Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, namshukuru Mungu kwa neema za kutujalia sote uhai. Kipekee nampongeza Mheshimiwa Profesa Sospeter Mwijarubi Muhongo, Waziri wa Nishati na Madini na Mheshimiwa Dkt. Merdad Matogolo Kalemani, Naibu Waziri wa Nishati na Madini pamoja na Watendaji wote wa Wizara.
Mheshimiwa Naibu Spika, kero yangu kubwa ni kuhusu gharama kubwa ya biogas kwa kuwa maeneo ya vijijini ni wafugaji hususan wanawake wa Kilimanjaro. Naomba iwepo namna ya kupunguza gharama ya kujenga na kuunganisha nishati na madini ya biogas majumbani.
Mheshimiwa Naibu Spika, michango mikubwa watumiaji wanayotozwa kwa ajili ya EWURA hainiingii akilini na wala haipendezi kwa watumiaji wa maji na umeme wanavyotozwa na EWURA katika ankara tofauti, bahati mbaya EWURA yenyewe hairejeshi chochote kwa wananchi kama CSR, natumaini kuona wakitoa mchango wa kuwaelimisha wanawake kwenye ujasiriamali na kadhalika.
Mheshimiwa Naibu Spika, watumiaji wengi wa umeme vijijini ni kwa ajili ya taa na baadhi luninga na kuchaji simu. Namwomba Mheshimiwa Waziri awaagize Mameneja wa Mikoa wateremshe tozo za vijijini ili familia nyingi zinufaike.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu tozo la umeme kwenye shule na vyuo; kumekuwepo na malalamiko makubwa sana kwa wamiliki wa wa maeneo tajwa. Namwomba Mheshimiwa Waziri aangalie namna ya kurekebisha tatizo hili, mfano, Kibosho School of Nursing, Chuo hiki kiko Moshi Vijijini katika Mkoa wa Kilimanjaro.
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo. naunga mkono hoja.