Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, umeme wa REA katika Jimbo langu lenye vijiji 87 na mitaa tisa mradi wa REA II umehusisha vijiji vitatu tu. Hii inakuwa ngumu kujibu maswali ya wananchi. Nashauri kuwa phase III ihusishe vijiji vyote kama Mheshimiwa Waziri alivyoahidi wakati nimempelekea hoja hii kwa mapendekezo ya vijiji vitakavyohusika kwenye REA phase III vijiji au mitaa ifuatayo haijawekwa.
Mitaa ya Nanyamba Mjini, Natoto, Chitondela, Chikwaya, Mibabo, Vijiji Miule, Mtimbwilimbwi, Shaba, Mbambakofi, Hinju Mtiniko, Maili, Maranje, Ngorongoro, Misufini, Kiromba, Kiyanga, Mayembe Juu, Mayembe Chini na Mchanje.
Mradi wa REA Mtwara Manispaa eneo la Ufukoni, Mbaye na Mji mwema ambao phase II ulitakiwa kukamilika mwezi Juni unasuasua, hivyo usimamiwe ili ukamilike kwa wakati.