Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia REA inafanya kazi ya kusambaza umeme vijijini, pamoja na kufanya kazi hiyo katika Mkoa wa Iringa, Wilaya ya Iringa Vijijini kuna substation iliyopo katika Kijiji cha Tagamenda ambapo umeme umeanza kusambazwa kwenda mikoa mbalimbali ikiwemo Shinyanga na mingine
Mheshimiwa Naibu Spika, kitu cha kushangaza, wanakijiji wanaofanya kazi ya kulinda umeme huo, hawajapata umeme hata huo wa REA. Swali kwa Wizara, hivi hawaoni kuwa hawawatendei haki wananchi wa Vijiji vya Tagamenda, Wangama, Ikuvilo na vingine ambao huishi karibu na kituo hicho substation kuunganisha umeme huo au hata wakapata umeme wa REA na wasiwe walinzi tu wa kituo na nyaya hizo?
Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Waziri, anapohitimisha naomba kupata majibu ili tuweze kuondokana na adha hii kwa wananchi wetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.