Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuchangia katika Wizara hii ya Madini mambo yafuatayo:-
Katika Mkoa wa Njombe Vijiji vingi havina umeme, mfano, katika Halmashauri ya Njombe Mjini, Kata tatu tu ambazo ziko mjini, wakati Kata kumi ni za vijijini hata kama vijiji hivi vina hadhi ya mji. Hivyo, naiomba Serikali ione ni namna gani inasaidia hizo kata kumi ambazo hazina mradi wa REA kwa sababu zina hadhi ya mji wakati kata hizo ziko vijijini, mradi wa REA ni wa vijijini tu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa ukataji wa miti huharibu mazingira, ili kuzuia ukataji wa miti bei ya gesi ipungue ili watu wengi watumie gesi kuliko kutumia kuni na mkaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia kwa kuwa kuna vyanzo vingi vya kupata nishati, basi Serikali ifanye utafiti maeneo mbalimbali kwa kuzingatia rasilimali zilizopo kwenye maeneo hayo kwa ajili ya kutengenezea nishati. Mfano, maeneo yenye mifugo mingi basi Serikali ione namna ya kupeleka program ya kutengeneza umeme au nishati ya gesi kutokana na kinyesi cha wanyama. Hali kadhalika maeneo yenye maji mengi au takataka nyingi kama maeneo ya mijini basi takataka hizo zitumike kutengenezea gesi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Mkoa wa Njombe hasa Njombe mjini, inazalisha takataka nyingi basi takataka hizo zitumike kwa ajili ya kutengenezea gesi.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Ludewa ina madini mengi ikiwemo chuma, makaa ya mawe na mengine. Naomba Serikali ihakikishe inasimamia uchimbaji wa madini ambayo yatatuongezea kipato. Wawekezaji wanaofika kwenye migodi hiyo ya Liganga na Mchuchuma wahakikishe wanapeleka huduma za jamii katika maeneo hayo ya Mchuchuma na Liganga pamoja na Wilaya yote ya Ludewa. Huduma hizo kama Umeme, Maji, huduma za afya na barabara za lami.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuwasilisha.