Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

Hon. Amina Ali Mzee

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2023

MHE. AMINA ALI MZEE: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi kunipa nafasi hii, nami nishukuru kwa nafasi ya kuchangia ya Wizara ya Ujenzi. Nianze kumpongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuweza kuendelea kutoa fedha nyingi ndani ya Sekta hii ya Ujenzi. Tunaona mtandao mkubwa wa barabara ndani ya nchi hii; Mheshimiwa Rais anatoa fedha nyingi ili mtandao uendelee kuenea na kuendeleza demokrasia ya nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niipongeze Wizara kwa kuendelea kuwapa wakandarasi vijana na wanawake ambao wanamaliza chuoni pale high court kuwajengea uwezo wa miaka mitatu ili waweze kujiajiri katika kazi mbalimbali za barabara ambazo zinaendelea ndani ya nchi hii, niipongeze sana Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nianze mchango wangu kwa kuchangia kuhusu kuwawezesha Shirika la TBA. Serikali ilitazame kwa jicho la huruma Shirika hili la TBA. Shirika letu la TBA linajitahidi sana kuhakikisha kwamba linajenga nyumba kwa ajili ya wananchi na watumishi wanaoishi ndani ya Dodoma hii na maeneo mengine ya Taifa hili. Serikali itazame basi haja, kama Kamati ilivyoshauri, kuomba shilingi bilioni 50 ili shirika hili nao wapatiwe ili waweze kujiendesha kibiashara na waweze kuzalisha faida. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, taasisi nyingi za Serikali zinadaiwa na Shirika hili la TBA, taasisi hizi zinalikwamisha shirika letu kujiendesha kwa faida na kibiashara. Wapo baadhi ya Waheshimiwa Wabunge na wananchi ambao pia wanadaiwa na shirika hili. Nitoe wito kwa wananchi na taasisi za Serikali, zilipe madeni ambayo wanadaiwa na TBA. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niendelee na mchango wangu kwa taasisi ya TEMESA. Tunaelewa kuwa taasisi nyingi za Serikali pamoja na Wizara wanapeleka magari yao ya halmashauri TEMESA; lakini wakishapeleka huko TEMESA wanaigeuza shamba la bibi. Wakishapeleka magari yao na yakishakuwa yamefika na kwamba wamepewa huduma, wakishamaliza kupewa huduma tu wanaondoka na magari yao, lakini taasisi yetu ya TEMESA hailipwi. Ninaomba taasisi za Serikali zilipe madeni yao wanayodaiwa na TEMESA. Tunajua kwamba TEMESA inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa vifaa kama vile vipuri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Serikali basi ione haja ya kuweza kuwapatia mtaji TEMESA ili waweze kununua spare wenyewe bila kutegemea spare kutoka kwa wafanyabiashara, maana sasa hivi wanachukua spare kutoka kwa wafanyabiashara. Wafanyabiashara hawa wakishawapa spare inawezekana hizo spare wanawapa nzima, inawezekana hizo spare fake, kwa hiyo wakija kutengeneza baada ya siku kadhaa gari za Serikali zinaharibika. Kwa hiyo tunaiomba Serikali iwape mtaji TEMESA ili waweze kujiendesha na wao kwa ajili ya kuendesha shughuli zao.

Mheshimiwa Spika, tumeona taarifa ya Kamati pia inaeleza juu ya wananchi wengi ambao wanadai fidia. Serikali yetu Tukufu, Mheshimiwa Waziri kijana, Naibu wake Waziri pamoja na Katibu Mkuu wetu mwanamke Mheshimiwa Aisha, tuchukue basi hatua na jitihada za haraka kuhakikisha kwamba wananchi wetu waliopisha maeneo kwa ajili ya ujenzi wa barabara nao wanalipwa fidia ili nao waweze kupisha maendeleo ya nchi yetu na ujenzi wa barabara. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sina mengi zaidi, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)