Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

Hon. Bahati Khamis Kombo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Mwaka wa Fedha 2025/2026

MHE. BAHATI KHAMIS KOMBO: Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Rais Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa ambayo ametufanyia Watanzania.

Mheshimiwa Spika, naomba kuchangia kwa ufupi kama ifuatavyo nikianza na mafanikio makubwa ambayo tumeyapata katika sekta zote, nani kama Samia? Niwaombe Watanzania wote wasisikilize matapeli wa kisiasa, tulikuwa na shida ya usafiri kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma, leo tunatumia saa chache tu tumefika Dodoma.
Mheshimiwa Spika, lililobaki kwa sasa tuangalie usafiri wa majini kwa zile sehemu ambazo hawajapata usafiri wa marine.

Mheshimiwa Spika, tuipongeze Serikali kwa kupata umeme na pia tubadilishe miundombinu ili wananchi waweze kufanya biashara zao vizuri.

Mheshimiwa Spika, naunga mkono hoja.