Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Madini kwa mwaka wa fedha 2016/2017.

WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nitoe shukurani nyingi kwa Wabunge wote kwa sababu maswali yalikuwa ni mengi sana mliyoyauliza kwa kuongea na maswali mengi sana mmeyauliza kwa maandishi na ikifika saa mbili usiku leo, tutakuwa yote tumeyajibu na tumeya-bind kama hivi, mpaka wale waliouliza kabla hatujakwenda mapumziko tayari tumeshayajibu. Kwa hiyo, niombe kwa ruhusa yako jibu la kila mtu tutaliweka kwa maandishi na tutawasambazia Wabunge wote kupitia ofisi ya Bunge. Hiyo inaonesha jinsi ambavyo ufanisi ulivyo mkubwa kwenye Wizara ya Nishati na Madini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile napenda kutoa shukurani kwamba yote mliyoyasema tumeyazingatia na tutayafanyia kazi kwa sababu maswali yanafanana fanana na ushauri unafanana fanana, ni vizuri nijibu kwa pamoja na ili mpatemwelekeo wa Taifa linakwenda wapi. Kwanza nianze na suala la Zanzibar, ndugu zangu wa Zanzibar hakuna suala lingine tena kwa sababu sheria imeshawaruhusu mnaweza mkatafuta mafuta wenyewe na mkayaendeleza nyie wenyewe. Hakuna anayewagandamiza, lakini niwaeleze mambo sasa ya kitaalam kuhusiana na hayo mafuta. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala ambalo itabidi mkae na majirani zenu na ndiyo maana inabidi utafiti ufanyike, ijulikane mna gesi kiasi gani, mna mafuta kiasi gani na yako wapi. Hilo swali hilo, yako wapi? Huku upande wa Msumbiji na Tanzania itabidi Tanzania na Msumbiji tukae chini kwa sababu gesi ile na mafuta haikuheshimu mpaka wa Ruvuma. Ziwa Tanganyika itabidi tukae pamoja na Kongo kwa sababu mafuta na gesi iliyomo pale haijaheshimu ule mpaka wa katikati ya ziwa. Kwa hiyo, ni vizuri ndugu zangu kama nchi moja ni lazima kwanza tujue mafuta hayo na gesi iko wapi, geographic location, halafu tukitoka pale tunakwenda kwa wataalam wanaojua, kuna the law of the sea ambayo ina define continental shelf na margin ya kila nchi. Kwa hiyo niwaachie hapo, inabidi bado tushirikiane.
Mheshimiwa Naibu Spika, nije upande wa umeme, Naibu Waziri ameongelea, watu wanasema tuwe na vyanzo vingi. Ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge na Watanzania ni kwamba Wizara inavijua, imeshavipigia mahesabu na hiyo ndiyo inaitwa energy mix au energy matrix. Tunakuwa na uhakika wa umeme kupatikana kwa sababu tutazalisha umeme kutoka kwenye gesi asilia, kwenye makaa ya mawe na kwenye maporomoko. Tutazalisha umeme kutoka kwenye jua, kwenye upepo, kwenye joto ardhi, kwenye bio-energies yaani biomass na biogas. Umeme wa joto ardhi, tumetengeneza ramani Tanzania tunajua joto ardhi iko wapi na ndiyo maana tunataka kuanza kuchoronga pale Ziwa Ngozi, Mbeya. Tunachotafuta sasa hivi ni kujua ukubwa wa volume ya ile steam inaweza ikazungusha turbine ya ukubwa gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaambie kwamba, vyanzo vipo, vinatosha na tunavifahamu. Hata speed ya upepo wa Singida tumeshapiga mahesabu, speed yake ni kali, ni mita tisa kwa sekunde moja ambayo inaruhusu kuweka mitambo ya kuzalisha umeme wa upepo na upande wa jua vile vile tumetengeneza ramani tunajua sehemu ambazo tunaweza tukapata umeme mwingi sehemu za Singida, Shinyanga na Dodoma. Kwa hiyo, kitaalam tuko vizuri tunajua kwamba umeme utapatikana wa uhakika.
Mheshimiwa Naibu Spika, nije kwenye suala la tunakokwenda. Haya mahesabu tukienda hatuendi kwa kubahatisha. Wizara hii ya Nishati na Madini ni lazima uchanganye sayansi, uchanganye na uchumi ndiyo utakwenda vizuri. Tumeshasema tuna maendeleo tunataka kuwa nchi ya kipato cha kati. Kuingia kwenye kipato cha kati kinaanzia dola 1,045, sisi tumesema tunataka kuanzia dola 3,000. Kwa hiyo, mwaka 2015 kama tutakuwa na GDP per capita ya dola 3,000 na sasa hivi GDP yetu ni karibu dola bilioni 50, iko inayumba yumba kidogo pale na tukichukulia kwamba tunazaliana kwa kiwango cha asilimia nne, kwa hiyo kufika mwaka 2025 huenda tutakuwa kati ya watu milioni 65 au milioni 70.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mahesabu tunachukulia milioni 70 ukipiga mahesabu ya GDP per capita 3,000 ni lazima GDP yetu iwe na bilioni zaidi ya 200, ndiyo linakuja suala la umeme sasa. Kuendesha huo uchumi unahitaji umeme mwingi na ndiyo maana unaona bajeti ya hii Wizara imejiwekeza kupatikana umeme mwingi, kwa hiyo ndugu zangu hivi vitu vinakwenda kwa mahesabu siyo kwa nadharia na ndiyo maana speech yangu ilikuwa imejaa takwimu, haikujaa malalamiko na matusi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, halafu kwenye dunia ya sasa ni lazima tufanye biashara ya umeme. Ndiyo maana tunajenga huu msongo wa kilovolt 400 kutoka kwenye mpaka wa Zambia na kwenye mpaka wa Kenya. Tunataka kuuziana umeme, hakuna sababu wewe kununua umeme wa bei mbaya hapa wakati Ethiopia wana umeme wa bei nafuu, huko ndiko tunakokwenda.
Mheshimiwa Naibu Spika, Ethiopia na nchi za Afrika Mashariki, nchi 11 tumeshawekeana mkataba tutatumia umeme wa maji ambao ni senti saba kwa unit moja. Kwa hiyo, suala la kutumia umeme wa mafuta tena ni historia kwa hii nchi. Kwa nini mtu atuuzie umeme wa bei mbaya wakati transmission line tunatoa umeme Ethiopia kuja huku. Kwa hiyo, ndiyo maana ya kuweka hizi na ndiyo maana kila Jumapili umeme unakatika kwa sababu tunajenga msongo mkubwa wa kusafirisha umeme, ni heri uumie sasa upate faraja baadaye. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa kuendesha haya yote tunaitaka TANESCO mpya. Wengine wanasema TANESCO igawanywe imekuwa kubwa sana. Ndugu zangu kwenye dunia ya nishati, TANESCO ni kitu kidogo kabisa hamna kitu. Kwa sababu kama alivyosema Naibu Waziri, uwezo wetu wote wa umeme ni megawatts 1,500. Kampuni moja India inazalisha umeme na kuuza zaidi ya megawatts 100,000, sasa wewe utagawa kampuni yenye megawatts 1,500 unakuwa unagawana umaskini tu pale.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, watu wanaopata huduma ya TANESCO bado ni wachache. Kwa hiyo, mabadiliko ya TANESCO ni kwamba inakwenda yenyewe inajibadilisha na sehemu zingine za TANESCO zinazikwa, zinakufa, ndiyo maana sasa hivi uzalishaji wa umeme uko wazi, kuwa mtu yeyote anaweza kuzalisha umeme na anaweza akamuuzia mtu yoyote bila kupitia TANESCO.
Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia ule mradi tunavyokwenda kufika mwaka 2025, kama ulivyo na simu ya tigo, ya voda, ya nini, TANESCO ya mwaka 2025 itakuwa ni hiyo hiyo. Unachagua nani akuuzie umeme kama ilivyo nchi zingine duniani na wote wamekwenda huko na wengine bahati nzuri wamekulia huko, kwa hiyo TANESCO inabadilika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, uwekezaji mpya nakiri kwamba kuna mikataba mibovu, sasa dawa yake tunatengeneza vigezo vya kuwekeza kuleta ushindani. Tarehe 30 hii document itakuwa tayari, itasambazwa dunia nzima na tutawaambia kwamba tunataka Lindi tunataka megawatt 300, je, wewe Kampuni hii unatupatia ofa ipi? Tunataka makampuni yashindane na hii itatoa haya mambo ya rushwa na mambo ya kupata mikataba mibaya. Kwa hiyo, ndugu zangu ngojeni tarehe 30 na kuonyesha kwamba sisi tuko wazi kabisa, World Bank, African Development Bank wote wamehusishwa kutengeneza hii document, ushindani. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, usafirishaji ameshaueleza, usambazaji vile vile tunakokwenda ikiwa hawa wakandarasi wa REA wanasambaza umeme vijijini, kwa nini watu binafsi wasisambaze umeme badala ya kutegemea tu TANESCO? Ndiyo hiyo nasema mabadiliko TANESCO vile vile haitakuwa inasambaza umeme peke yake. Ndiyo mabadiliko hayo yanakuja na hii document siyo vitu vya kichwani tumeshaitayarisha, imeshapitishwa kwenye Cabinet.
Mheshimiwa Naibu Spika, deni la TANESCO, nakiri kwamba deni ni kubwa na upande mmoja ni mikataba mibovu, kuna wizi, kuna rushwa na uongozi dhaifu. Ndugu zangu Watanzania niwaeleze, mtu asije akaueleza ubora wa kampuni yoyote ambayo inauzia TANESCO umeme sasa hivi, haipo. Labda kama awe ametumwa kuishabikia lakini tukisema ukweli mbele ya Mwenyezi Mungu mikataba yote siyo mizuri. Sasa nimechukua hapa mifano, utasikia mwingine anaimba SONGAS, SYMBION. SONGAS capacity charge kwa mwezi tulikuwa tunawalipa dola za Marekani milioni nne nukta sita, SYMBION milioni mbili nukta nne, IPTL milioni mbili nukta sita, AGGREKO milioni mbili, hakuna ambayo ina manufaa makubwa kwetu. Kwa hiyo, ndugu zangu ninachowaomba Wabunge msitumiwe, msishabikie mkaja hapa kutetea Kampuni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini uongozi wa TANESCO sasa hivi unabadilika, kila baada ya miezi mitatu tunafanya tathmini. Ukitaka kubaki Meneja wa TANESCO ni lazima kila baada ya miezi mitatu tukutathmini. Umekusanya fedha kiasi gani za Shirika? Umeunganisha wateja wapya kiasi gani? Umekuwa na ubunifu wa kutatua matatizo ya umeme kwenye eneo gani na kwa kiasi gani?. Tathmini ya pili inakuja tarehe 1 Juni, moja ilishafanyika watu wakaanguka, mwezi wa Sita tarehe moja inafanyika, tarehe 1 Septemba inafanyika. Kwa hiyo, kila miezi mitatu. Kwa hiyo, ukitaka kuwa Meneja TANESCO inabidi ujitume kweli kweli. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, suala la nguzo. Ni kweli kwamba nguzo tumesema TANESCO haipaswi kum-charge mtu. Ni tatizo la ukosefu wa fedha, tunakubali hilo lakini ni suala la mpito, huko tunakokwenda TANESCO ni lazima iwafuate wateja. Huwa nawaeleza ni mfano kama wa mtu anayenunua daladala kufanya biashara ya kusafirisha watu, halafu anakwenda kumwomba yule mtu atakayetumia daladala nipatie hela niongeze ninunue daladala, maana yake ndiyo hiyo ya TANESCO kuomba nguzo. Kwa hiyo, hiki ni kitu cha mpito ndugu zangu, yatakwisha.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nguzo za ndugu zangu wa Iringa, nimekwenda Iringa nimewatembelea, twendeni na vigezo. Kama mtu ana kiwanda cha nguzo aende TANESCO, ni lazima viwango vya TANESCO tuvikidhi. Hatuwezi kununua nguzo tu kwa kusema kwamba, haya mambo ya ubora hayana uzalendo, kwa sababu mambo yakiharibika mtawageuka tena TANESCO. Kwa hiyo, kama kuna mtu ana uwezo wa kuuza nguzo aje nguzo zake zifanyiwe tathmini na nguzo hizo tutanunua hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, umeme vijijini, REA Awamu ya II hadi sasa hivi ndugu zangu, jana Hazina imeweka bilioni 80.2. Hadi jana Serikali imeshatoa asilimia 80 ya fedha za REA Awamu ya II. Kwa hiyo, huko kwenu mtaona mabadiliko wakandarasi watakavyokwenda kasi, hamna kisingizio na nimemuuliza REA MD anasema hizo akizipata, Wakandarasi wanalipwa na nia yetu ni kazi za REA awamu ya II zote zikamilike ikifika Juni mwaka huu. Awamu ya III, mmeona tumeongeza. Sasa ndugu zangu, tuna shilingi bilioni 534.4 na Hazina kwa kuwa makusanyo yetu yamekuwa mazuri, nina uhakika fedha zote hizo zitapatikana. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mbali ya hiyo wengine hawakujua kwamba mbali ya hizi fedha, mnazopitisha humu Wizara nayo tunasumbuka, tunazunguka duniani kutafuta fedha. Msidhani ni za bajeti tu! Ndiyo maana Jumatatu msiponiona hapa nitakuwa nimekimbia kwenda kuwatafutia fedha. Mambo yakienda vizuri na tunayejadiliana naye mwingine anataka kumwaga milioni 200 REA, dola sio shilingi! Huko huwa tuna majadiliano kwenye dola tu sio shilingi tena. Kwa hiyo, akimwaga hizo 200 jamani mtakuwa wapi? Sasa tatizo kama hutaki bajeti hii ipite, basi sasa hata hiyo 200 usahau. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, solar kwa watu wa visiwani, nataka kuwahakikishia watu wa visiwani tumeshafanya uamuzi na REA, REA wameshaleta kwangu kwa maandishi kwamba visiwa vyote vilivyoko ndani ya mipaka ya Tanzania vitapata umeme wa jua – solar uzuri wa hii, hii tunaongea tayari tuna pesa, unajua huku Nishati na Madini tunaongea kitu cha uhakika. Tuna hela, wala hatulalamiki ooh! fulani katunyima hela ah ah! Tuna hela! Sasa uzuri wa hizi solar vijijini tunaomba Wabunge mtusaidie vijana waliosoma VETA wanaweza kwenda pale REA waone namna wanavyoweza kuwatumia. Wale vijana wenye utaalam, kuna fedha wanaweza wakapewa pale. Nendeni REA vijana wajikite kwenye huu umeme, tutatoa ajira, tutatoa na fedha na REA huwa inatoa fedha kuwawezesha watu.
Mheshimiwa Naibu Spika, Wakandarasi nimekaa nao vikao karibu viwili, wale wabovu wote hawatapata miradi tena niseme transformer za TANELEC mimi mwenyewe nilienda pale siyo kwamba waliosema hapa ndiyo wamegundua hilo, ni mimi nilienda pale. Ila wengine tuna kawaida ya kukaa kimya tunafanya vitu kimya kimya, kwa hiyo aliyeongea mambo ya TANELEC hapa siyo yeye wa kwanza, wa kwanza ni mimi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nimewaeleza TANESCO na REA kwamba REA Awamu ya III tujitahidi kutumia transformer zetu kwa sababu wenye share kwenye TANELEC ni TANESCO na NDC nao wana share. Hata hivyo, ndugu zangu tatizo ni Sheria yetu ya Manunuzi, kwa hiyo tunaomba Sheria ya Manunuzi iweke sehemu kwamba ni lazima vitu vya ndani vitumike. Kibaya cha Sheria ya Manunuzi hata kama mtu anataka kula rushwa, kudanganya anakimbilia hiyo sheria na nyie ndiyo mliipitisha humu mliokuwemo, mimi sikuwepo hapa wakati huo. Kwa nini mlipitisha hii sheria? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja mafuta, wengi wamelalamika, lakini Waheshimiwa Wabunge na Watanzania tulisema usimamizi ni mbovu. Sasa hivi TPDC tumeitoa kwenye shughuli ya kufanya biashara, kutafuta mafuta na gesi, wakati huo huo inasimamia makampuni mengine. Kwa hiyo, tumeanzisha PURA (Petroleum Upstream Regulatory Agency). Hii ndiyo itasimamia mikataba yote, kila kitu hata TPDC yenyewe itasimamiwa, itapitia mikataba, itaweka ma-auditor, kwa hiyo, nadhani hapo tutakuwa tumepiga hatua na udhaifu huo utakuwa umetoweka. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, uagizwaji wa mafuta, vilevile tumeanzisha Petroleum Bulk Procurement Agency, huko nyuma ni waagizaji mafuta walikuwa wamejiweka pamoja wenyewe wanaji-regulate wenyewe, sasa tuna chombo cha Serikali na chenyewe kinafanya kazi vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, upande wa mafuta wengi sana mmeongea EWURA, unajua Waheshimiwa Wabunge kuna mihimili mitatu, unashangaa mtu anayetaka kulazimisha mhimili wake ndiyo uwe na sauti kubwa kuliko mihimili mingine. Mlishatoa pendekezo kwamba EWURA iko Maji, iko Nishati inayumbayumba sasa nyie mmetoa ushauri kwa Executive, kwa hiyo ushauri wenu tunauchukua, tunakwenda kuufanyia kazi, lakini tusije hapa tena unasema tulisema, hapana! Mnashauri nyie, sisi tuna shauri Bunge, sasa ushauri unaweza ukachukuliwa au ukakataliwa. Hiyo ni muhimu sana, ushauri unaweza ukakubaliwa au ukakataliwa! Kwa hiyo, tutalichukua hili kama Serikali tutalifanyia kazi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la vinasaba limekuwa kubwa, mmeliongelea kwa hisia, hatuwezi kuamua hapa. Naitisha na nimeongea na wengine Jumanne kwa sababu nitakuwa nimepewa kazi zingine na wakubwa zangu, lakini Jumanne tarehe 24 yaani Jumanne ya wiki ijayo, saa nne asubuhi nataka nianze kikao cha kutatua hili tatizo la EWURA na vinasaba. Hatuwezi kulitolea uamuzi hapa, tukitoa hapa litakuwa la kisiasa maana sisi wote hapa wanasiasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimeita wale wanaohifadhi mafuta, naomba watoe wawakilishi wanne wanaohifadhi mafuta, wawakilishi wanne wanaosafirisha mafuta, wawakilishi wanne wanaofanya biashara ya mafuta, waje pale Wizarani na mimi mwenyewe ndiyo nitakuwa Mwenyekiti, saa nne asubuhi Jumanne tarehe 24, tuyaongee yote waziwazi na EWURA ikae pale ijibu mapigo. Baada ya hapo ndiyo tutaona tunakwendaje, lakini suala la vinasaba hatuwezi kulifanyia uamuzi hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, gesi asilia, LNG fidia italipwa, mmeomba tusomeshe vijana, ndugu zangu fuateni mambo tuliyoyafanya tumesomesha vijana wa Lindi na Mtwara wengi sana VETA. Tumewalipia kuja mpaka hapa chuo chetu. Wakati tunaenda mimi mwenyewe nimeomba scholarships China, wamenipatia scholar 25 kila mwaka kwa miaka mitano. Tunatafuta watu wa Lindi na Mtwara, kwa hiyo watu wa Lindi na Mtwara kusema tuwasomeshe tunajitahidi, ndugu yangu hawa wengine wa China wameshachaguliwa. Kwa hiyo, kama mna vijana muwalete halafu hii LNG biashara yake sio tu ya oil and gas unataka watu ma-chemist wazuri, ma-physicist na wengineo. Kwa hiyo, bado hao tunaotaka kuwasomesha lazima wapambane na mambo ya sayansi. Unajua mambo ya sayansi tena hayana mambo ya mkoa. (Makofi/Vicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika na Waheshimiwa Wabunge sawa mmesema tutawaita, tutakaa chini, tutaongea na watu wengi wa Lindi na Mtwara, tunaongea sana labda tu hii semina niwaite tena tukae chini, ni bahati mbaya wenzenu tuliwapeleka mpaka Norway, tumewapeleka Malaysia, tumejitahidi sana. Sasa mngewabakiza wale unajua! Haya! Gesi asilia inatumika viwandani sasa hivi tunavyosema kuna viwanda 37 Dar es Salaam vinatumia gesi na vinataka gesi zaidi. Kwa hiyo, ndugu zangu tusidhani kwamba gesi haijatumika, inatumika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, gesi majumbani, tumefanya majaribio, bomba la kilometa 6.3 kutoka Ubungo mpaka Mikocheni nyumba za TPDC wale ndani ya nyumba wana mabomba mawili; bomba la maji na bomba la gesi. Tanzania ya Mheshimiwa Magufuli anayosema ya viwanda ndiyo hiyo hata nyie Wabunge tutaanza na nyie muwe na mabomba mawili la gesi na la maji. Hawa wa TPDC wananiambia kwamba kwa mwezi wanalipa shilingi 25,000 elfu kutumia gesi kupikia, chini kuliko hata mkaa. Kwa hiyo, huko ndiyo Tanzania mpya inayokuja.
Mheshimiwa Naibu Spika, Lindi na Mtwara mnajua tumeshaanza kufanya feasibility studies na huenda tutazipata hizo fedha. Mimi mwenyewe nazisimamia kuzitafuta tutapata hizo fedha, ndiyo maana mwingine akisoma kwenye bajeti anasema mbona hapa mmeweka kidogo lakini hizi fedha ni nyingi, hapana! Sisi tunategemea fedha nyingi nje siyo hii. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tuna Lindi na Mtwara mtapata. Nyie wenyewe Waheshimiwa kwa kuwa ni Madiwani nyumba mjenge zimekaa kwenye foleni vizuri, mahali ambapo bomba litapita maana bomba kulipitisha kwenye squatters ni problem kweli kweli. Kwa hiyo, huo umeme unakuja Lindi na Mtwara na Dar es Salaam ndiyo tumeombea fedha kusambaza gesi majumbani. Sasa na hii gesi haitaishia hapo, Tanzania ijayo ambayo Mheshimiwa anasema ya viwanda anasema vitu vya uhakika. Sasa hivi hili bomba kubwa linasafirisha kwa siku, 70 million cubic feet of natural gas per day, lakini capacity yake ni 784 million cubic feet of natural gas per day! Hili bomba sasa hivi likianza kufanya kazi likijaa kabisa kufanya kazi na kugundua gesi lazima tupeleke mikoani. Kwa hiyo, hata mikoa itapata hii gesi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi mengine, Kiwanda cha Mbolea cha Kilwa chenyewe kimepanga kuzalisha tani 3,800 kwa siku. Uwekezaji wake ni dola za Marekani bilioni moja nukta tisa. Sasa ndugu yangu wa Lindi ukisema tunapataje faida, kuna Kiwanda cha Mbolea kinakuja investment one point nine billion US dollars na bado unasema hujui utafaidikaje, saa zingine ndiyo maana huwa unaniona mzee nakaa kimya, nashindwa tu niseme nini sasa.
Mheshimiwa Naibu Spika, matumizi yale ya gesi siyo mengi kiasi hicho, huyu anahitaji 104 million cubic feet of natural gas per day, kwa miaka 20 anakuwa kama amekuna upele tu, hajatumia gesi yoyote, wala kule msianze kuwa na masikitiko gesi yetu, yaani hazidishi TCF moja, havushi trillioni moja ya gesi kwa miaka 20. Ndiyo maana hata wale wa Mtwara wanaweza vile vile wakaanzisha hicho kiwanda na LNG ndugu yangu ukisema huoni faida ndiyo itakuwa investment kubwa katika historia ya nchi hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, niende Dangote mmeiongelea sana, Dangote wameshindwana na TPDC bei, yeye anataka dola tano kwa unit TPDC inasema nne lakini wameshakubaliana watajenga pipe atatumia. Makaa ya mawe aliagiza South Africa mara moja tu! Tumemzuia atumie mawe ya Ngaka, gypsum nayo tumemzuia atumie gypsum za hapa.
Mheshimiwa Naibu Spika, bomba la Uganda mmeliongelea tutalifanyia kazi, finally tunafanyia kazi, wiki ijayo tutaonana tena kulijadili tena. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nije madini. Nyamongo ndugu yangu Heche tulikaa, ndiyo maana akiongea mimi natulia tu! Tuliweka Tume, tutakwenda pale itakuwa wazi. Sasa hayo yote aliyokuwa anaongea humu sijui yako kwenye ile ripoti, kwa hiyo atulie tu!
Mheshimiwa Naibu Spika, Mererani tanzanite, tunajua kuna matatizo ya kufa na kupona lakini tunalifanyia kazi vile vile. Lakini kwa tanzanite, Watanzania sisi wenyewe tuliomo humu huwa tunasema wazawa, wazawa walio na hiyo kitu ni wazawa! Ndiyo maana siku nyingine nilisema, jamani hata mzawa, mgeni wote wanaweza kuwa sio wazuri. Sasa sijui mzawa akikuibia dola kumi na Mhindi akikuibia dola kumi yupi amekuibia nyingi? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, haya kodi, katika mikataba na kodi za madini, ni kweli kwamba kuna migodi ambayo haijaanza kulipa kodi ya mapato (Corporate Tax), lakini karibu yote sasa tunaisimamia wataanza kulipa.
Vile vile Waheshimiwa mmetoa wazo la TMAA, TANSORT na TRA na hilo tunalichukua twende kulifanyia kazi. Wachimbaji wadogo, tumewapatia mlezi wao ni STAMICO, maeneo tunatoa na tutaendelea kutoa. Jumapili iliyopita nilikuwa nimekaa na watu wa World Bank watatoa karibu dola milioni 400 kuwasaidia. Kwa hiyo tunaendelea kuwasaidia sana, isipokuwa na nyie muwahimize walipe kodi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nimalizie na hili la Mheshimiwa Zitto, alisema jamani mafuta mbaani ya siku tano ndege hazitui hapa. Nimepewa hapa takwimu inaonesha hadi sasa tuna lita milioni 8,749,810, haya yanatutosha mpaka Juni, sasa huyu aliyekwambia yamebaki ya siku tano yeye mwenyewe kaleta barua anasema anayo ya siku ngapi? Anayo ya siku 16. Ndiyo mambo nasema haya mambo magumu kidogo, alimwambia ana tano, huyo huyo kaleta barua nina ya siku 16. Kwa hiyo, tunachokifanya ni kwamba tunachukua tahadhari, tunashukuru sana tutaleta mafuta mengine tuhakikishe kwamba mafuta yapo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini huyu aliyesema mafuta yake ni machafu kuna sehemu ya hifadhi ya mafuta yake TBS imekuta ni masafi. Kwa hiyo, kuna mengine ana mchafu, huku ana masafi, niwaeleze hawa wa mafuta hii ni biashara ngumu, ni lazima tunavyoijadili humu tuwe makini sana. Huyu aliyeleta ndiye amempatia PUMA, amempatia OILCOM, amempatia TOTAL, amempatia GAPCO. GAPCO ni safi, TOTAL safi, OILCOM safi, PUMA ndiyo analalamika, lakini sehemu ya shehena yake haina hiyo contamination na TBS wanaendelea kufanya utafiti na kujaribu kutafuta nini kimetokea. Lakini mafuta yapo, tunachukua tahadhari yasije yakaisha kabla, meli nyingine inakuja tarehe 13 Juni, kwa hiyo tunataka kuhakikisha tuna mafuta mengi kabla ya tarehe 13 Juni. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani nimemaliza sasa? Bunge lako lilikaa, aah! Sorry! Bado bado. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla sijatoa hoja, kuna moja hapa limebaki la hawa wa magwangala lakini nilitatua. Jamani haya mabaki kuja kukaa dunia ya karne ya 21 unang‟ang‟ana kabisa mtu apewe mabaki ya mgodi, kusema kweli haiendani, kweli! Inaweza kuwa hamna kitu humu. Ni wananchi na CHADEMA ndiyo mlimtuma...

Aliombwa? Wananchi ndiyo walimwomba. Mnyika sasa kama…
Ooh samahani, lakini unajua Mheshimiwa Mnyika, kijana wangu huwa mara nyingi kabla sijamaliza nampatia swali la kichwa. Je, nimpatie, nisimpe?
WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, haya naomba kutoa hoja.