Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Zainabu Nuhu Mwamwindi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. ZAINABU N. MWAMWINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi jioni ya leo niweze kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli, tingatinga letu.
Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote, naomba nianze kama Waheshimiwa Wabunge wenzangu walivyoanza kwa kumshukuru Mwenyezi Mungu, Mungu mwenye rehema ambaye ametuwezesha leo na mimi Zainabu Mwamwindi kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya
Muungano nawakiilisha wazazi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli. Ni hotuba ambayo ilikuwa ina mashiko mazuri na makubwa sana, ni hotuba ambayo ilisheheni kila kitu na ni hotuba ambayo siyo tu kwamba sisi Wabunge wa CCM ndiyo tunaipongeza au tunasema kwamba ilikuwa ni hotuba nzuri bali ndiyo ukweli uliojitokeza siku Mheshimiwa Rais alipokuja kutufungulia au kutuzindulia Bunge letu la Jamhuri ya Muungano. Hotuba hii siyo sisi tu, hotuba hii kuanzia wale wengi wanaoishi vijijini waliipongeza sana. Pia wasomi baadhi yao waliipongeza hotuba hii lakini na wale ambao wanaishi mjini nao pia waliipongeza hotuba ya Mheshimiwa Rais. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwenye macho haambiwi tizama na mwenye masikio haambiwi sikia, Mheshimiwa Magufuli Watanzania kumchagua hatukufanya kosa. Pia niseme tu kwamba Watanzania kukichagua Chama cha Mapinduzi ndiyo usahihi wenyewe, ni chama
ambacho wamekiona kina sera nzuri, Ilani inayotekelezeka lakini pia ndiyo Chama kinachosema ukweli, hilo ni sahihi kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kuchangia hotuba ya Mheshimiwa Rais. Katika hotuba yake, aliongea kwa uchungu na Wabunge wengi wamechangia sina sababu ya kurudia lakini niseme yako mambo muhimu ambayo alikuwa ameyakazia sana, alikazia sana suala la maji.
Kule Tosamaganga, Kata ya Kalenga ambayo ina vijiji vitatu na vitongoji sita ule mradi wa maji ni wa mwaka 1974 miundombinu imechakaa. Nitoe ombi kwa Serikali ya CCM, Serikali sikivu, Serikali ambayo ina huruma na wananchi isaidie mradi huu. Tosamaganga ni sehemu ambayo imetoa viongozi wengi sana ambao wanalitumikia taifa hili. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 1974 wakati mradi wa maji unawekwa kule Tosamaganga ulizingatia uwepo wa watu waliokuwepo kwa wakati ule. Sasa Tosamaganga imekuwa na idadi kubwa sana ya watu hivyo maji hayatoshelezi kutokana na wananchi kuongezeka kwa kiwango kikubwa. Tosamaganga pia ina shule nyingi sana ambazo watoto wanasoma pale. Imezungukwa na mito lakini kuna mlima mkubwa, watoto wanashuka kwenda kufuata maji kule wengine wanatumbukia. Hivi karibuni amekufa mtoto mmoja wa kiume anaitwa Onesmo kwa sababu alikuwa amekwenda kufua siku ya Jumamosi, kwa bahati mbaya nguo yake ikateleza kwenye maji wakati anaifuatilia akazama kwenye maji. Kwa hiyo, bomba za Tosamaganga pamoja na vijiji vyake maji hayatoki kabisa. Kwa hiyo, namuomba Waziri wa Maji uiangalie Tosamaganga kwa jicho la huruma, maji yale hayatoshelezi.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia nikuombe Mheshimiwa Waziri, kule Unyangwila na Irangi, wale watu wameanza wao kwa nguvu zao kuchimba mtaro kwa ajili ya kutafuta maji na wameshafikisha kilomita tatu na nusu lakini hawajui watapata wapi mabomba na maji kwenda
kuyafikia ni kilomita sita na nusu. Mheshimiwa Waziri nakuomba katika ufalme wako iangalie Tosamaganga na Kalenga. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wakati akiwa Mbunge Marehemu Dkt. William Mgimwa, alikuwa ameahidi kupeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Ipamba, ni Hospitali Teule ya Wilaya ya Iringa. Hospitali ile ni kubwa kwani inatoa huduma kwa wananchi wanaotoka maeneo mbalimbali katika Mkoa wa Iringa na pengine hata Mikoa ya jirani lakini cha kusikitisha hakuna gari la wagonjwa. Nikuombe sana Mheshimiwa Waziri wa Afya, hebu tazama Hospitali Teule ya Ipamba ili waweze kupatiwa gari la wagonjwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mara yangu ya kwanza leo nimeshuhudia Mbunge akilidanganya Bunge Tukufu. Mbunge wa Iringa Mjini amesimama hapa kwa kujiamini kabisa, akizungumzia habari ya Iringa Mjini yeye kama mwakilishi wa wananchi wa Iringa.
Amezungumzia mradi wa maji wa Iringa Mjini na kujidai kwamba Iringa Mjini maji yanapatikana kwa kiwango cha asilimia 98 lakini akasema Iringa kuna barabara za lami, akaenda mbali zaidi akasema taa Iringa Mjini zinawaka bila shida barabarani. Mheshimiwa Mbunge
amelidanganya Bunge lako Tukufu. Naomba tumwogope Mungu, Mchungaji Msingwa ni Mchungaji na nafikiri ana hofu ya Mungu lakini anapozungumzia vitu hata anaposema tunajikomba ndiyo tuna haki sisi tumsifu Rais wetu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, Iringa Mjini mpaka sasa maji ni asilimia 95, ni mradi ambao ulianzishwa na Mheshimiwa Monica Mbega wakati wa kipindi chake na hata wakati wa uzinduzi wa mradi huu alikuja Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nne. Mbunge wa Iringa Mjini, Mheshimiwa Peter Msingwa hakushiriki katika uzinduzi wa mradi huu kwa sababu mradi huu alikuwa hautaki na hakuukubali. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, la pili la barabara vilevile Mheshimiwa Msigwa amezikuta barabara za lami zikiwa tayari zipo. Ni mradi uliotoka Serikali Kuu na siyo yeye. Taa za barabarani ni package ya mradi wa barabara…
NAIBU SPIKA: Muda wako umeisha Mheshimiwa Mwamwindi naomba ukae.