Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa afya njema na kuweza kupata fursa ya kuchangia Wizara ya Ardhi, Maendeleo ya Makazi. Naomba nianze kuchangia Wizara hii, kwenye suala zima la migogoro.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala hili la migogoro niseme tu Mheshimiwa Lukuvi amepata pongezi nyingi, lakini kwa Mkoa wa Dodoma kwa kweli kazi bado anayo. Nasema kazi bado anayo kwa sababu Mheshimiwa Lukuvi, atasema mambo kadhaa nitakayoyazungumza hapa hayahusiani na Wizara yake, lakini yeye ndiye tunajua Wizara yake inahusika na suala zima la makazi, bila ardhi makazi hayapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Manispaa yetu ya Dodoma, kuna kitu ambacho kinataka kuja kutengenezwa kinachofanana na kinachokuja kutengenezwa hapa KDA. Sisi Dodoma tuna msalaba unaitwa CDA, hii CDA ilianzishwa mnamo mwaka1973 kwa madhumuni na malengo ya kwenda kuhamisha Makao Makuu ya Serikali kuja Manispaa ya Dodoma ama Mkoa wa Dodoma. Yapata leo miaka 43 makao makuu yapo ya chama tu, ya Serikali hayapo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize Serikali mko hapa team nzima, huyo Waziri Mkuu yuko hapa mwakilishi wake, lakini Wizara mbalimbali ziko hapa. Wana Manispaa ya Dodoma wanataka kujua, kama suala zima la uanzishwaji wa kitu kinachoitwa CDA, ilikuwa dhumuni lake na malengo yake ni kwa ajili ya kuleta, Makao Makuu Dodoma imeshindikana, kwa nini hii CDA isirudi Dar es Salaam ambako ndiko kuna makao makuu ya nchi? Badala yake kuendelea kuwatesa na hao Watanzania wasio kuwa na hatia yoyote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, CDA ilikuja ili ipange mji wetu vizuri, igawe viwanja vyetu lakini pili, iweze kuwapatia wananchi wa Manispaa ya Dodoma ardhi, waweze kuiendeleza, waweze kupata makazi yaliyo bora. Leo wananchi wa Manispaa ya Dodoma, hawana ardhi ambayo wamemilikishwa na CDA badala yake wamegeuzwa kuwa watumwa ndani ya wilaya yao, wanaitwa wavamizi kila kunapokucha wanabomolewa nyumba zao. Inasikitisha sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi, wananchi hawa bila huruma CDA imekuja tangu mwaka 1973 kuna watu walikuwepo tangu mwaka 1959 kabla hata ya Uhuru. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Njedengwa pale walienda kuwavunjia watu wakampa eneo mtu mmoja tu, anaitwa Maimu, wakavunja nyumba 127, wakampatia maekari mtu mmoja anaitwa Maimu pale. Wananchi wetu wakawaacha hewani, wanateseka halafu leo wanataka kuendelea kuwashawishi Watanzania wa Manispaa ya Dodoma wabaki na CDA, hawaitaki CDA chukueni pelekeni kwenu, mnakoona kunafaa. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro hii nimeona hapa kwenye kitabu cha Mheshimiwa Waziri, migogoro iliyoripotiwa ni migogoro miwili tu, (d) center na (c)center, si kweli. Nami nimshukuru Mheshimiwa Waziri hili begi lake alilonipa nimeweka haya ma-document ya CDA, ya wananchi haya, yako humu yamejaa haya humu, haya nimemletea. Mimi hili begi kazi yake nitakuwa nabeba makablasha ya wananchi, wanaoandika barua kwenye Ofisi zenu hamuwajibu, mnaitetea CDA, mnaenda mnakaa kwenye vikao vya Bodi ya CDA mnawaangamiza Watanzania wa Manispaa ya Dodoma, wamewakoseeni nini? Kwa nini mnawanyanyasa hawa watu kiasi hiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wapimieni ardhi, wapeni ramani zenu, wapeni waende wakajenge, watu wanahangaika barabarani wanauza machungwa akinamama wajane, wana watoto wanasomesha, wanakwenda wanajijengea nyumba zao, mnaenda mnawavunjiwa, mnawaambia wavamizi. Mnachotaka ni nini, kuwaua? Waueni basi tujue moja kama hamuwataki, watu hao hao ndiyo wanaendelea kuwasitirini ninyi kupata kura, halafu bado mnaleta blabla hapa, za kuendelea kuwanyanyasa namna hiyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, safari hii mlipiga magoti na kupiga push up mwaka 2015 mwaka jana, 2020 nahisi mtaruka kichura chura. Kwa sababu hawa watu hawako tayari kuendelea na mateso haya na mwakilishi wa Waziri Mkuu aliyeko hapa, wananchi wa Kata zote 41 za Manispaa ya Dodoma, wanahitaji kukutana na ofisi ya Waziri Mkuu, ili waeleze manyanyaso na mateso wanayoyapata na hawa watumishi wa CDA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, CDA haisimamiwi na mtu yeyote ipo tu ina-hang hapo, inajifanyia mambo inavyotaka, inafunga ofisi tarehe 2 Februari, wamefunga ofisi eti kisa mfagizi kafiwa na mume wake, sisi mbona huwa hatuahirishi Bunge hapa mama yangu Stella amefiwa, mbona hatujaahirisha Bunge ili twende tukamzike mama yake Stella. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini mume wa mfagizi wa CDA kafiwa wamefunga ofisi ambayo inahudumia zaidi ya watu 40,000 kweli ni mateso gani mnayowatesa hawa watu. Wana kikao tu cha kawaida cha kikazi wanafunga ofisi eti wamekwenda kwenye kikao, hawa watu kwa nini mnawaendekeza kiasi hiki? Hiki kiburi mnawapa ninyi Serikali. Laiti mngeamua kuwasimamia na mkawaambia lengo na madhumuni ya kuanzishwa kwa CDA wangeshika adabu, wangefuata Kanuni na taratibu za nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wetu wanakwenda wanachukua ardhi zao, wakichukua ardhi badala ya kwenda kuwafanyia maboresho ya ardhi pale wawapimie watu mahali walipo, hawawapimii mahali wanawaambia tunapima upya. Wanawafukuza kwenye maeneo yao, wanaenda wanapima vile viwanja, wakipima viwanja wanawalipa fidia laki tano, kiwanja kinaenda kuuzwa milioni tano ama milioni nane, mwananchi gani anaenda kupata hiyo milioni nane ya kununua kiwanja. Ardhi umemkuta nayo mwenyewe, wana mashamba yao yaliyokuwa enzi na enzi, walikuwa wanayatumia kulima ardhi ya Dodoma hii haiongezeki inapungua, ila watu tunaongezeka. Kwa hiyo, ni lazima CDA muiambie na itambue, kwamba wanahitaji siku ngapi wakamilishe upimaji wa ardhi Manispaa ya Dodoma wafungashe vilago vyao waende wanakotaka kwenda, sisi Dodoma hapa tumechoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hawawezi kufanya hiyo kazi, Mheshimiwa Lukuvi na Waziri Mkuu, wananchi wa Dodoma watakachokuja kukifanya wasije wakaleta lawama, wamechoka kunyanyaswa na mateso ya CDA. Hilo nimemaliza kwenye CDA, naomba lifanyiwe kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wangu wanataka kukutana na Waziri Mwenye dhamana na Ofisi ya Waziri Mkuu, kwa sababu Wabunge wa Majimbo hususani Jimbo la Dodoma Mjini, mmekuwa mkiwafunga midomo wasisemee suala la CDA. Alianza hapa Malole mwaka juzi mkamfunga zipu, eti ooh usiongee kwani ni ya nani, kama ni ya kwenu si mseme, kama na ninyi mnanufaika humo semeni. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Migogoro ya Swagaswaga ambayo najua iko kwa Mheshimiwa Maghembe, lakini suala lile la Swagaswaga, Mkungunero Dagram A mgogoro wa uliopo katika mpaka wa Chemba na Kiteto. Tunahitaji mpaka ule Waziri akautatue. Bunge la mwezi wa Pili, wazee wa watu walitoka Wilaya ya Chemba, wakaja kumwona Mheshimiwa Waziri wakamwelezea hali halisi iliyoko pale kati ya mgogoro wa Chemba na Kiteto, Mheshimiwa Waziri hata ile wakawapa maneno matamu, wakawarudisha wazee wa watu na wakawaahidi Waziri Mkuu anakwenda. Mpaka leo Waziri Mkuu hajawahi kukanyaga, wala harufu tu ya kusikia kwamba atakuja kwenda haipo, kwa nini wanawadharau hawa wananchi. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama hawawezi kushughulikia, wawambie wajichukulie hatua wenyewe watajua nini cha kufanya huko, mpaka wasubiri watu wafe ndio wataona ving‟ora na magari 42 yanafukuzana yanakwenda kuangalia maiti za watu kule. Kwa nini mnafanya namna hii ninyi? Wananchi wa Dodoma wamewakoseeni nini? Tuambieni kama kuna makosa ambayo tumewakosea tuwaombeni radhi, ili na sisi tuweze kupata haki ya kuhudumiwa na Serikali ya Chama cha Mapinduzi, kama maeneo mengine.
Maeneo mengine umefanya, Dodoma kwetu wewe ni sifuri na mbaya zaidi ulikuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma hii, usichokijua ni nini wewe Mheshimiwa Lukuvi, kipi usijchokijua kwa Dodoma hii ambayo umekaa kimya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante ni mzuka tu! Suala la nyumba huko Swagaswaga na wapi huko niwaombe tu mwende wananchi wale, wazee wa watu wanalalamika huko, dharau hawazihitaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Nyumba, wakati Kamati zinaundwa nilikuwa mjumbe wa Kamati hiyo kabla sijabadilishwa, nilikwenda kuona nyumba zinazojengwa na Shirika la Nyumba, nyumba zile sijui maana yake tulipoziona zilikuwa hazijaisha lakini tukaambiwa zikiisha zitakuwa nzuri, sasa sijui zinakuwaje nzuri kabla ya kwisha sijaelewa, chumba kinachokwenda kuwekwa mtu pale ukiweka kitanda cha futi tatu na nusu, utaweka na meza ndogo ya kuwekea mafuta ya kupaka, labda na kitana na dawa ya mswaki. Chumba huwezi kuweka kitanda cha tano kwa sita, nani siku hizi analeta biashara ya mbanano kwenye vyumba, vyumba vya kulala havina hadhi…
MWENYEKITI: Mheshimiwa ahsante sana.
MHE. KUNTI Y. MAJALA Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.