Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumshukuru Mungu wangu kwa kunipa nafasi ya kusimama mbele ya Bunge lako Tukufu. Pia nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa William Vangimembe Lukuvi pamoja na timu yake kwa kazi nzuri anayoifanya, hakika Mheshimiwa Lukuvi anatosha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuchangia juu ya Wakala wa Taifa wa Utafiti wa Nyumba na Vifaa vya Ujenzi. Nadhani wakala ilianzishwa kwa ajili ya kuwasaidia wananchi na hasa wale wenye kipato kidogo; lakini ofisi za wakala ziko Dar es Salaam, wakala hana ofisi wilayani, mikoani lakini wananchi wenye shida ya kujenga nyumba zenye gharama nafuu wako wilayani, wako vijijini, wako mikoani. Sasa sijui ofisi hii inafanya nini Dar es Salaam na hata katika wilaya zetu hatujawahi kuwaona wala kusikia habari zao, tunazisoma habari za kwenye vitabu tu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niwaombe wakala hawa waje Dodoma; Dodoma tuna mahitaji makubwa ya kujenga nyumba za gharama nafuu na hasa kwa matofali haya ya kufungamana; vijana wapo watapata ajira kutokana na kazi hii ya kufyatua hayo matofali, watajenga nyumba za kudumu, nzuri ambazo hazitawasumbua kujenga tena baada ya kipindi kifupi. Naomba wafanye kazi hiyo Dodoma kama mkoa wa mfano na wananchi watafaidika na shughuli watakazozifanya. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie pia pale alipoachia Zainab kuchangia kwamba mabaraza yetu yanahudumiwa na Wizara tatu; Mabaraza ya Kata yapo chini ya TAMISEMI, Mabaraza ya Wilaya yapo chini ya Wizara ya Ardhi, lakini mwananchi anapokata rufaa anakwenda Wizara ya Sheria na Katiba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Tume ya Kurekebisha Sheria waliwahi kufanya kazi hii na walileta mapendekezo Serikalini, sasa Waziri atatuambia mapendekezo yalifanyiwa kazi? Mabaraza yetu ya Kata hawana mafunzo, hawana hata vitabu rejea yaani ukiwaambia warejee kwenye kesi ambayo iliwahi kutokea hawana pa kurejea. Kwa hiyo, wanafanya kazi kutokana na mazoea na akili ya mtu inavyomtuma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nadhani kuna haja ya Sheria namba tano kufanyiwa marekebisho makubwa. Pia hawa Wajumbe wa Baraza hata ukisema Mwenyekiti anapokwenda kwenye eneo la tukio la baraza hawana ulinzi hawa watu. Kwa hiyo, wananchi wanaweza wakawafanyia fujo na kuwapiga hata kuwafanyaje wanavyoweza kwa sababu hawana ulinzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe pia Mahakama ya Ardhi wapangiwe muda wa kumaliza kesi. Mahakama ya Rufaa zingine wamepangiwa muda wa kumaliza kesi; kesi 200 kwa mwaka, lakini Mahakama ya Ardhi hatujui na hawajapangiwa muda wa kukamilisha kesi zao na kusikiliza kesi kwa sababu Mahakama ya Ardhi kuna kesi nyingi sana zinazosubiriwa kule. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, Maafisa wa Ardhi na wa Mipango Miji; hapa ndiyo kuna majipu ya kutumbuliwa. Mheshimiwa Lukuvi hapa ndiyo kuna majipu yaliyoiva kwa sababu Maafisa Ardhi wanagawa ardhi eneo ambalo wanajua ni eneo la wazi, wanagawa ardhi eneo ambalo wanajua watajenga shule, wanagawa ardhi maeneo ambayo ni ya soko; lakini wanafanya makusudi na ndiyo maana watu wanavunjiwa bila sababu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu alievunjiwa analeta hati yake kuonesha kwamba anamiliki kihalali eneo hilo, lakini Maafisa Mipango Miji wapo, Maafisa Ardhi wapo. Nikimsikia Mheshimiwa Waziri amewatumbua hawa watu nitafurahi sana kwa sababu wapo ambao wanafanya makusudi na kuwapa wananchi hasara. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la hati ya umiliki wa ardhi ipo hata kwa Serikali zetu. Safari hii ripoti ya CAG, Halmashauri zetu walipata hati za mashaka kutokana na halmashauri zetu kutokuwa na hati miliki ya maeneo yao. Nimwombe Mheshimiwa Waziri hili lifanyiwe kazi haraka sana ili halmashauri zetu wawe na hati za kumiliki mali hasa ya ardhi katika maeneo yao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi Dodoma, Dodoma tuna suala la Mkungunero halikuhusu sana lakini linakuhusu kwa sababu wewe ndiye Waziri wa Ardhi. Mkungunero pale vita vilishawahi kutokea, watu wakapigana, watu watatu wakauawa. Wananchi wa Mkungunero walishaandika barua kwa Waziri Mkuu, Mawaziri waliopita kabla yake walikwenda Mkungunero, tulikwenda nao, lakini mgogoro wa Mkungunero haujakwisha mpaka leo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mgogoro mkubwa kati ya Hifadhi ya Mkungunero na vijiji 17 vya Chemba na Kondoa. Sasa hivi wananchi wa Kondoa hawawaruhusu Maafisa Wanyamapori kufanya kitu pale. Kilomita 50 tu tuliomba ili wananchi waweze kulima, lakini imekuwa kazi miaka nenda rudi, miaka nenda rudi hili suala halijakwisha. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimwombe Mheshimiwa Waziri suala la Mkungunero liishe sasa. Tumewaalika Mawaziri wa Maliasili, Waziri Mkuu alikwenda, yeye mwenyewe tunamwomba aende ili suala la Mkungunero na wananchi liishe Vijiji 17 wanagombea ardhi pale, wanaomba kilomita 50 tu waweze kulima. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nirudi Dodoma Mjini, suala la CDA na Manispaa tumechoka nalo, wananchi wamechoka nalo. Inawezekana limetuchosha kwa sababu CDA hamuwapi fedha za kutosha, wanabomoa nyumba za watu bila fidia, wanachukua ardhi za watu bila fidia, wanalipa fidia kwa ardhi waliyotwaa kwa tathmini ya mwaka 2002, 2005 sio haki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimsihi na nimwombe Mheshimiwa Lukuvi anajua sana suala la CDA na suala la ardhi ya manispaa, Mheshimiwa Rais alipokuja hapa wakati wa kampeni alisema CDA, Ofisi ya Waziri Mkuu pamoja na halmashauri watakaa na kushughulikia suala la ardhi ya Manispaa ya Dodoma, nimsihi sana na Waziri wa TAMISEMI kama hayupo Naibu wake yupo na Mheshimiwa Jenista yupo, niwaombe sana washughulikieni suala la CDA.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Dodoma wanaipenda sana Serikali ya Chama cha Mapinduzi na ndiyo maana tunapata kura nyingi, lakini sasa hili la CDA halijashughulikiwa, namsihi sana Mheshimiwa Waziri ashughulikie hili suala la CDA. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini lipo la Kongwa, Kata ya Dabalo na Kata ya Segala wana ugomvi mkubwa sana na watu wa Kongwa mpaka kati ya Kata ya Dabalo na Segala na watu wa Kongwa, ni mgogoro wa muda mrefu. Wananchi wameacha kulima pale kwa ajili ya mgogoro ule unaoendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni mkoa mmoja lakini mgogoro ule umedumu kwa muda mrefu hakuna namna ya kumaliza mgogoro ule. Nakusihi ndugu kwa ndugu hawaongei, ndugu kwa ndugu wanatafutana, ndugu kwa ndugu wamekasirikiana kwa sababu ya mgogoro uliopo pale Kata ya Dabalo, Kata ya Segala na Wilaya ya Kongwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, najua Mheshimiw;a Waziri ana uwezo huo,aumetatua migogoro mingi katika nchi yetu, huu mgogoro hautamshinda, nimwombe na ikiwezekana twende pamoja kwani kuna shida gani, twende pamoja mimi na yeye Mheshimiwa Lukuvi tukamalize suala hili, tukamalize mgogoro wa wananchi. Mimi nipo tayari, Mheshimiwa Lukuvi anajua kwamba nipo tayari kwenda pamoja naye.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie sasa suala la National Housing. National Housing wamefanya kazi kubwa na inayoonekana. Kabla ya mwaka 2007/2008 National Housing walikuwa wanapata ruzuku kutoka Serikalini, lakini baada ya kuingia Mkurugenzi Mchechu, National Housing imebadilika kwa kiasi kikubwa. Wanajenga nyumba mijiniā€¦
Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja lakini wapunguzieni VAT ili tununue nyumba za National Housing.