Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. OMAR A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namshukuru Mungu kutuamsha salama. Na mimi naomba nitoe ushauri wangu kwenye Wizara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa namshukuru Mheshimiwa Lukuvi kwa maamuzi yake mazito ya kubomoa lile ghorofa kubwa pale mjini, ila napenda kumshauri Mheshimiwa Waziri asiishie hapo, azidi kupambana kwa kuwa majengo ambayo hayana ubora yatakuwa mengi sana, hivyo katika kuokoa maisha ya watu, napenda kuhimiza wataalam wetu wasikae ofisini, waende site na kukagua kila hatua ya ujenzi inayojengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumshauri Mheshimiwa Waziri kuangalia watumishi wake kwa karibu zaidi ili kuhakikisha migogoro ya ardhi inapungua kwa kiwango kikubwa. Malalamiko ya ardhi yanasababishwa na watumishi wa Wizara ya Ardhi kwa uuzaji holela maeneo ya wazi, utoaji wa hati mara mbili mbili ambayo siyo ya kujengea. Tukirekebisha hili, hali hii ya migogoro mijini na vijijini itakwisha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu migogoro ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji, nadhani wengi hawana elimu ya sheria especially wafugaji. Utakuta mfugaji mmoja ana ng‟ombe 5,000. Kwa idadi hii lazima atagombana na wakulima kwa kuwa eneo lake haliwezi kumtosha. Elimu ya sheria ya kuwa na idadi ya mifugo inatakiwa itolewe sana na isimamiwe kwa makini na kwa ukaribu. Pia wafugaji wapewe elimu ya kupanda nyasi, ikiwezekana Serikali ianze kwa mashamba ya mfano. Hii itapunguza kasi ya wafugaji kuhamahama kwa kutafuta malisho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia napenda kumshauri Mheshimiwa Waziri na watumishi wake, nyumba nyingi zinazojengwa mijini hazifuati sheria ya parking, ni vizuri sheria kali ikatipitishwa kwa yeyote asiyefuata kanuni ya ujenzi mijini. Pia napenda kuishauri NHC kuangalia upya mpango wa kodi zao na hili linaweza kurekebishika kwa kupunguza kodi na linawezakana kama watasimamia vizuri ukusanyaji wa kodi za sasa hasa katika taasisi kubwa ambazo zinaongoza kwa kutolipa kodi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jedwali Na. 2 page ya 83, marejesho ya asilimia 30 ya makusanyo ya Halmashauri kwenye mkoa wa Tanga kuna Handeni tu; na sasa kuna majimbo mawili; Handeni Mjini na Handeni Vijijini. Naomba unisaidie ufafanuzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.